OCD Meatu kuwaandikia barua Chadema kwamba wasifanye mikusanyiko kwa sababu kuna tishio la Ugaidi, kauli hii ya maandishi ina madhara gani kiuchumi?

Riz1:
Baba mbona unasemwa vibaya na unatukanwa sana hadi kwenye mitandao na hauchukui hatua..??
Jk:
Mwanangu, katiba ya JMWT imempa Rais mamlaka makubwa sana. Sasa nikitaka kuwachukulia hatua nitafunga wangapi..!!
Hayo ndiyo mawazo kutoka kwa kiongozi aliye komaa kisiasa na aliye kubali kuwa rais wa watanzania.

Maana hao wengine walikuwa kila siku wanatwambia kuwa urais ni mzigo mkubwa sana lkn ukifika uchaguzi wanenda kuchukua form.
 
Au wakuu mnasemaje?

Hebu soma hii.

Wakati sekretariet ya ccm_tanzania ikiwa imemaliza kutembelea mikoa kadhaa ya ikiwemo Kagera,Kigoma,na Katavi huku wakifanya mikutano ya hadhara, jeshi la polisi @tanpol limezuia mikutano ya @ChademaTz kwa kile kilichoelezwa uwepo wa tishio la Ugaidi nchini Tanzania.
Hii tuiingize kwenye maajabu 7 ya Dunia

3015333_Screenshot_20211128-090107_WhatsApp.jpg
 
Au wakuu mnasemaje?

Hebu soma hii.

Wakati sekretariet ya ccm_tanzania ikiwa imemaliza kutembelea mikoa kadhaa ya ikiwemo Kagera,Kigoma,na Katavi huku wakifanya mikutano ya hadhara, jeshi la polisi @tanpol limezuia mikutano ya @ChademaTz kwa kile kilichoelezwa uwepo wa tishio la Ugaidi nchini Tanzania.
Plpl katwambia eti wahuni bado wapo
 
Hata kama ni kudanganya hivi haiwezekani kutumia sababu nyingine zaidi ya UGAIDI. Impact ya ugaidi ni kubwa haswa wakati huu nchi inapojaribu kuimarisha mahusiano na nchi nyingine na kufufua sekta ya utalii kutoka kwenye mtikisiko.
 
Kauli ya maandishi toka jeshi la polisi inayohubiri uwepo wa matishio ya ugaidi nchini ni hatari kwa mustakabali wa uwekezaji na Mpango wa mama wa kui-brand Tanzania
Watavuna walichopanda na kwa hii barua naamini kuna kundi la watu serikalini kwa makusudi wanamhujumu mama Samia.
 
Alafu kesho utasikia kiongozi na upimbi wake anasimama jukwaani anasema Tanzania ni sehemu salama
 
Wewe ndio unaota ndoto za mchana kwa sababu ni chama kipi kingeweza kuishinda CCM katika uchaguzi uliopita ? Siasa imewashinda mnabaki kuleta visingizio tu.
Ndugu yangu Nizasasa hivi sasa mchana acha kuota ndoto za mchana sii zakweli ni za uongo
.
 
Wewe ndio unaota ndoto za mchana kwa sababu ni chama kipi kingeweza kuishinda CCM katika uchaguzi uliopita ? Siasa imewashinda mnabaki kuleta visingizio tu.
Hata slow atapingana na hoja yako ngoja apande dk45 utarudisha mrejesho humu🤔.
 
Ipo barua inasambaa mitandaoni kutoka kwa oCD Meatu ikiziia mikusanyiko ya wanachama wa Chadema Kwa sababu kwamba kipimdi hiki Kuna tishio la Ugaidi.

Yawezekana sababu hii ni ya msingi au isiwe na msingi. Lakini barua hii ambayo naamini itasambaa Dunia ina madhara makubwa KULIKO faida kwa Taifa LETU.

Naomba tujiulize maswali yafuatayo;

1. Ni kweli lipo tishio la Ugaidi nchini?

2. Kama lipo, Nani alipaswa kutangaza uwepo wa tishio ilo?

3. Kama halipo, Nani atakwenda kuiambia Dunia kwamba Tanzania ni sehemu salama kiuwekezaji na haki tishio la Ugaidi?

4. Kama tishio lipo na OCD ametangaza bila kujua Nini madhara ya kauli yake, Je ni lini viongozi wanaoteuliwa watabaki kuwa wale tu waliosomea uongozi na siyo wale waliojikuta viongozi kwa mserereko wa vyeo.

5. Ni upi msimamo wa Serikali kuhusu barua hii iliyozua taaruki mitandaoni?
Kama rais alisha sema kuna magaidi wamesha hukumiwa, hawa wana shindwaje kuongea ugoro?
 
Back
Top Bottom