OCD Kiteto atoa masaa 48 kwa wafugaji

JAMHURI

JF-Expert Member
Dec 15, 2010
449
60
MKUU wa Polisi Kiteto, SP Fadhili Luoga, ametoa masaa 48 kwa wafugaji wa jamii ya kimasai waliofanya uhalifu kujisalimisha.

Uhalifu uliofanywa ni kulisha mifugo kwenye mashamba ya wakulima, pamoja na kuwajeruhi wakulima hao.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Namelock Wilayani humo, Luoga àlisema, kitendo cha wafugaji kuwapiga wakulima bila sababu halikubaliki.

"Huwezi kuingiza mifugo kwenye shamba la mkulima kisha unamwachia maumivu..unampiga kwanini umpige? amefanya kosa gani?"alihoji Luoga

" Sasa imefikia hatua mmeanza kupigana wenyewe kwa wenyewe ni aibu... kwani juzi watu waliopigana mikuki walipigana kwa sababu gani haya ni mambo ya aibu"

Àlisema hivi sasa hakuna sababu ya kupigana kwasababu ya kugombea mabua...busara zitumike unapohitaji mabua ya mwenzako tena usubiri awe ameondoa mazao yake sio ulimkuta unapiga tu.

Katibu Tarafa ya Kibaya, Zulfa Laiza alieleza wananchi hao kuwa ameagizwa na MKUU wa Wilaya kuwa, jamii hiyo iache kutembeza mifugo barabarani kwani ina haribu barabarani.

" Nimekuja kuwapa ujumbe kutokana kwa MKUU wa Wilaya ya Kiteto kuwa, Wafugaji muache kutembeza mifugo yenu barabarani sambamba na kuchunga kwenye hifadhi ya Emboley Murtangos"

Hili ni agizo na tayari tumesha tengeneza boma kwaajili ya kuhifadhi mifugo itakayokamatwa mpaka itakapolipiwa àlisema Laiza

Tumetengezea barabara kwa gharama kubwa sana km 88 ya thamani ya 4.6 bil kwa ufadhili wa Wamarekani kwanini tuiharibu? alihoji Laiza

Kwa upande wake Michael Lepunyat Diwani wa kata ya Namelock aliridhia kukamatwa mifugo hiyo àlisema wameshatoa Elimu isipokuwa wafugaji wanakaidi.

Mwisho
 

Attachments

  • FB_IMG_1534518501674.jpg
    FB_IMG_1534518501674.jpg
    55.2 KB · Views: 31
...ni vizuri hatua zichukuliwe jamii zote ziishi kwa kutegemeana na kuheshimiana....tusiirudishe kiteto yetu ilikotoka.....asante kwa taarifa muddy
 
MKUU wa Wilaya ya Kiteto Mkoani Manyara, Mhandisi Tamain Magesa, amewataka wafugaji kutoingiza mifugo yao hifadhi ya Emboley Murtangos.

Hifadhi ya Emboley Murtangos iliamriwa na mahakama pasifanyike shughuhuli za kibinadamu baada ya mabishano kati ya wakulima na wafugaji.

Akiwasilisha agizo hilo Katibu Tarafa ya Kibaya, Zulfa Laiza kwenye mkutano wa wananchi wa Kijiji cha Namelock alisema, taarifa iliyopo wafugaji wameweka makazi yao katika hifadhi hiyo.

" Nimeambiwa kusema, wale walioweka makazi yao kwenye hifadhi ya Emboley Murtangos waondoke mara moja kwani hatua itakayofuata ni kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria"

Sambamba na agizo hilo wafugaji hao wametakiwa kutotembeza mifugo yao barabarani kwani Wilaya imejipanga kuikamata inapo onekana

Kwa upande wa wafugaji hao walionyesha kutekeleza maagizo hayo huku Diwani wa kata hiyo Michael Lepunyati akitaka sheria ifuate mkondo wake.

Mwisho.
 

Attachments

  • FB_IMG_1534522033346.jpg
    FB_IMG_1534522033346.jpg
    18.7 KB · Views: 25
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom