Obama aahirisha safari yake ya kutembelea mbuga za wanyama tanzania

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,863
34,330
[h=3]OBAMA AAHIRISHA SAFARI YAKE YA KUTEMBELEA MBUGA ZA WANYAMA TANZANIA[/h]





23157

Rais Obama ambaye ameamua kukatiza ziara yake ya kitalii Tanzania kwa ajili ya kushughulikia kwanza matatizo ya wananchi wake.
23156

Magari ya kivita 56 ambayo yatatakiwa kumsindikiza Obama katika safari yake ya kitalii Tanzania

23158

Askari walenga shabaha watakaokuwa wanamlinda na wanyama wakali
23155

Meli ya kivita itakayokuwa ufukweni ikiwa na ndege za kivita na wafanyakazi wa dharura na wauguzi.
Presidential_limo_cadillac_one_a_look_inside.jpg

Magari 14 aina ya limo ambayo yatakuwa yanatumiwa na Obama katika ziara yake Tanzania
Obama-Cadillac-limousine-2009-Inaugural-Parade.jpg
480-limousine.jpg

f15-flying-630-620x413.jpg

Ndege za kivita zitakazotumika kuhakikisha usalama wa angani

Presidential_limousine_loaded_in_aircraft.jpg

Ndege ya mizigo ambayo itasafirisha magari ya kifahari kwa ajili ya safari ya Obama


WASHINGTON –
Ikulu ya White House ya Marekani imekatiza safari ya Rais Obama na mkewe Michelle ya kutembelea mbuga ya wanaya ya mikumi iliyopo Tanzania kutokana na ukata unaoikabili serikali yake. Imeelezwa katika gazeti la Washington Post jana.

Gazeti hilo ambalo lilinukuu mipango ya siri ya safari hiyo imesema kuwa safari ya Obama na mkewe ambayo ilikuwa ifanyike baadaye mwezi huu, ingehitaji majasusi wa kumlinda rais huyo kwa njia za kipekee zaidi kuhakikisha usalama wake na mkewe.

Safari ya Rais katika mbuga za wanyama inahitaji ulinzi wa hali ya juu, silaha za hali ya juu kama siper rifles ambazo zitaweza kulenga wanyama wakali kama cheetahs, (duma, samba au wanyama wengine kama ikitokea wanataka kumsogelea au kumdhuru rais huyo.

(The safari "would have required the president's special counterassault team to carry sniper rifles with high-caliber rounds that could neutralize cheetahs, lions or other animals if they became a threat," the paper reported.)

Ikulu ya Marekani imefuta ziara hiyo ambayo rais Obama alikuwa atembelee mikumi national park kwa masaa mawili.
Hata hivyo msemaji wa Ikulu ya Marekani hakupatikana mara moja kutoa maelezo. Msemaji mwingine alisema ziara ya kutembelea Robben Island ambamo Mzee Mandela alikuwa amefungwa kwa miaka 27 ilikuwa ikipewa kipaumbele zaidi dhidi ya safari ya tanzania.


"Sababu kubwa za kufutwa kwa ziara hiyo ni kwa sababu ya ya kuwa na upungufu wa bajeti na vifaa vya kumlinda Obama katika mission yake hiyo, hivyo ikaonekana ni rahisi zaidi kutembelea Robben Island kuliko Mikumi National Park. "Alisema msemaji huyo Josh Earnest na kuongeza kuwa "ni ngumu kufanya safari zote hizo kwa pamoja."

Hii ilikuwa ni ziara ya kitalii ya kwanza kwa Rais Obama tangia amechaguliwa January 2009, safari ambayo ingeligarimu Taifa hilo kati ya dola milioni 60 hadi 100.

Mamia ya askari wa siri (secret agents) wanatakiwa kupelekwa katika sehemu ambazo Obama atatembelea pamoja na manuari ya kivita yenye kubeba ndege za kivita (Navy aircraft carrier or amphibious ship) ikiwa na wahudumu pamoja na wauguzi maalum ambao watakaa ufukweni kwa dharura yeyote itakayojitokeza.

Pamoja na hayo magari zaidi ya 56 yatapelewa kwenye nchi hizo tatu kwa njia ya ndege pamoja na vioo maalum vya kuzuia risasi (sheets of bulletproof glass) ambavyo vitazungushiwa kwenye hoteli ambayo atafikia Obama.


Kama vile ulinzi huo hautoshi, pia kuta kuwa na ndege za kivita zitakazokuwa zinazunguka katika anga ambalo Obama atakuwa amefikia na hizo ndege zitakuwa zinazunguka angani hapo kwa masaa 24 kwa kupeana zamu

("Fighter jets will fly in shifts, giving 24-hour coverage over the president's airspace")




chanzo. OBAMA AAHIRISHA SAFARI YAKE YA KUTEMBELEA MBUGA ZA WANYAMA TANZANIA - MPEKUZI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom