Utunzaji wa nywele za asili

Tumia mafuta ya mnyonyo yanapatikana katika maduka ya dawa za asili..kichupa kidogo buku
 
Mimi nina rules kadhaa nimejiwekea kwa nywele zangu natural na nimeona maendeleo kwa kweli...mwanzo ilikuwa zikirefuka tu nanyoa ili ziwe fupi iwe rahisi kuchana na kustyle...lakini nimejifunza cha kufanya ili nywele ziwe laini, zichanike vizuri na kunyooka

1. Fanya conditioning (tunaitaga steaming)
Nywele zinafubaa kwa kukosa matunzo jamani. Fanya deep conditioning kila wiki mara 1 na kila unapotaka kusuka fanya deep conditioning kabla. Deep conditioner zinauzwa madukani au unaweza kufanya ya asili kwa kutumia mix ya ndizi, parachichi, asali, yai na mafuta ya nazi.

Conditioner unakaa nayo dk 30 hadi 40 then unaosha.

2. Mafuta hayazipi nywele unyevu bali yanasaidia kuhifadhi unyevu. Kitu kinachofanya nywele zinakuwa ngumu na kupata tabu kuchanika na kunyooka ni kukosa unyevu.

Kosa tunalofanya wengi ni kudhani mafuta yatazipa nywele zetu unyevu. Unyevu unapatikana kwenye maji au kuna bidhaa zinauzwa zenye kutoa unyevu kwa nywele (Moisturizers au leave in conditioners)

Hivyo kama mzururaji juani kama mimi hakikisha kila asubuhi au jioni unanyunyizia nywele yako maji au unapaka moisturizer yako au leave in halafu unapaka mafuta ya chaguo lako kwa juu ili kuhifadhi unyevu. Achana na habari za nywele ukiweka maji zinanuka, ni myth tu labda ziwe chafu. Kama si mzururaji unaweza kufanya hivi kila baada ya siku 2 au 3...

3. Chana nywele kwa kuzigawa kwenye mafungu. Jamani mimi nilikuwa kinara wa kusema "nywele zangu hazichanikiii". Lakini tatizo lilikuwa ni kulazimisha kuzichana tu randomly mara chana imeingia hapa imetokea kule.

Gawa nywele zako hata sehemu zisizopungua 4 kisha kwa kila fungu paka leave in yako na mafuta yako, chana. Ukimaliza suka kisection chako au kibane kisivurugike hamia kwingine.

Maisha mepeeesiiiii

4. Usilale na nywele natural bila kuzisuka mabutu. Hutokufa, utaamka nazo lakini huo mfungano utakaokutana nao asubuhi utazichukia.

Zisuke mabutu nywele zako kabla hujalala hasa kwa wenye ndefu, atleast wenye fupi wanaweza kulala nazo hvohvo. Kisha jifunge kitambaa au vaa kofia.

5. Google jinsi ya kuzistyle nywele zako wewe mwenyewe. Jamani mimi naamini katika theory ya mkono mbaya. Kuna watu wana mikono mibaya kwa nywele, akikushikashika nywele zinadhoofu.

Minimize ishu za saluni, style nywele zako mwenyewe.

Na kuna styles nyingi nzuri sana kwa nywele za asili, Hebu cheki hizi hapa chini

View attachment 640374

View attachment 640375

View attachment 640918

NB:

Nimeona kuna mtu hapo juu anasema ukipaka leave in au products za Aunt Jackies nywele zako zinakuwa kama umeweka dawa; Sijui ana nywele aina gani ila kwa wenye kipilipili kile concord chenyewe naomba nipingane nae, ni nzuri, zinarahisisha uchanaji na nywele zinakuwa laini ila sio kama umeweka dawa; asije fanya watu mkawa na matarajio ya juu sana halafu mkaja kumuita muongo.

Natumia Leave In Conditioner yao inaitwa Quench, Kuna Leave-in detangler ya watoto inaitwa Knot having it(hii nilinunua tu kwa kupenda rangi ila kwakweli haina ulazima), natumia na detangler inaitwa Knot on My Watch na Defining Curl Custard yao ya Curl La La.

Hizi products ni NZURI SANA. Yani nywele unachana vizuri, ukitaka kufanya style zile za kusokota halafu unafumua zinabaki na mawimbi, ukitaka kupaka tu halafu unaacha nywele zinaonekana mawimbi yake ya asili, ni wewe tu na bei zake ni affordable sana 15000 tu.

Kwa mnaopenda kunyoosha nywele bila kutumia blow dryer angalieni video hiyo..



Wasalaam.
Samahani....Umewahi kutimia product za texture my way au una uzoefu na aunt Jackie's tuu??
 
kuna mafuta yanaitwa t444z. haya mafuta ni kiboko! kila mtu ananiuliza kama nimeweka dawa lakini wapi. ukisuka ukapaka chini ya ngozi unaweza kusahau kama hata ulisuka. yaani unafumua unapoona umeichoka style. mimi siyauzi na wala si agent wao lakini nimeyakubali. japo ni expensive kidogo ila the result is worth it. bei yake ni 60,000/=
 
Samahani....Umewahi kutimia product za texture my way au una uzoefu na aunt Jackie's tuu??

Sijawahi kuzitumia kwa kweli na mwezi uliopita nimeziona SH Amon nikatamani kuzinunua(bei rahisi sana aisee) ila nikatoka nje ya duka nikasoma reviews zake mtandaoni(sababu sikuwahi kuzisikia kokote kabla ya siku hiyo) nikaona si nzuri. Wengi wanasema ni nzuri kwa mashombeshombe wenye type 3 hair hadi 4A lakini sisi wa kipilipili kichaa si rafiki kwetu.

Kwa kuongezea, siku hizi nimehamia products za Shea Moisture and i must say zinafanya kazi bora zaidi hasa katika kustyle nywele. Unaweza zijaribu japo bei zake zimechangamka!
 
kuna mafuta yanaitwa t444z. haya mafuta ni kiboko! kila mtu ananiuliza kama nimeweka dawa lakini wapi. ukisuka ukapaka chini ya ngozi unaweza kusahau kama hata ulisuka. yaani unafumua unapoona umeichoka style. mimi siyauzi na wala si agent wao lakini nimeyakubali. japo ni expensive kidogo ila the result is worth it. bei yake ni 60,000/=
Sijawahi kutumia t444z ila kutokana na reviews za wengi walioyatumia sikubaliani na sifa utoazo. Unaweza kuwa sahihi though!
 
Sijawahi kuzitumia kwa kweli na mwezi uliopita nimeziona SH Amon nikatamani kuzinunua(bei rahisi sana aisee) ila nikatoka nje ya duka nikasoma reviews zake mtandaoni(sababu sikuwahi kuzisikia kokote kabla ya siku hiyo) nikaona si nzuri. Wengi wanasema ni nzuri kwa mashombeshombe wenye type 3 hair hadi 4A lakini sisi wa kipilipili kichaa si rafiki kwetu.

Kwa kuongezea, siku hizi nimehamia products za Shea Moisture and i must say zinafanya kazi bora zaidi hasa katika kustyle nywele. Unaweza zijaribu japo bei zake zimechangamka!
Nilijaribu kutumia leave in yao harufu yake tuu sio rafiki..ila sikuona kama inatofauti sana na ya aunt Jackie's. ( Labda kwasababu sina kipilipili kichaa ) nilitaka nipate mawazo yako maana nilihisi labda mimi ndo nina kisirani nazo. Shea moisture zimechangamka bei kama cantu??


Mimi ninatumia Bio care products na aunt Jackie's so far it works for me. Ila nime hamu hiyo shea moisture...nitapita weekend nione!
 
kuna mafuta yanaitwa t444z. haya mafuta ni kiboko! kila mtu ananiuliza kama nimeweka dawa lakini wapi. ukisuka ukapaka chini ya ngozi unaweza kusahau kama hata ulisuka. yaani unafumua unapoona umeichoka style. mimi siyauzi na wala si agent wao lakini nimeyakubali. japo ni expensive kidogo ila the result is worth it. bei yake ni 60,000/=
Good thing it works for you...ila nywele zinatofautiana at times. It's beautiful ukipata that one product that responds postively...hongera
 
Nilijaribu kutumia leave in yao harufu yake tuu sio rafiki..ila sikuona kama inatofauti sana na ya aunt Jackie's. ( Labda kwasababu sina kipilipili kichaa ) nilitaka nipate mawazo yako maana nilihisi labda mimi ndo nina kisirani nazo. Shea moisture zimechangamka bei kama cantu??


Mimi ninatumia Bio care products na aunt Jackie's so far it works for me. Ila nime hamu hiyo shea moisture...nitapita weekend nione!
Hongera ndugu...mimi ni kipilipili kile type Z..yani hata nywele ifike mgongoni inajicoil inaonekana kama kiafro kifupi. Kama ziko kama aunt jackies ntajaribu kununua leave in yake nione. Shea moisture ni 45,000 hadi 50,000 tshs ila naona zinastahili sababu hata harufu yake si mchezo na ukitumia kidogo tu inaleta matokeo.
 
Sijawahi kutumia t444z ila kutokana na reviews za wengi walioyatumia sikubaliani na sifa utoazo. Unaweza kuwa sahihi though!

sijui kwa wao wameyatumia vipi. maana hata wao wanakushauri usipake kila siku. yale mafuta hata viuwalaza vinaota nywele. plus ukitaka maximum results wana na products zingine zinazoambatana na hayo mafuta. binafsi mafuta tu yalinipa intended results. shida picha sikupiga ila nywele zillirefuka na kuwa na ubora mzuri kwa muda mchache.
 
sijui kwa wao wameyatumia vipi. maana hata wao wanakushauri usipake kila siku. yale mafuta hata viuwalaza vinaota nywele. plus ukitaka maximum results wana na products zingine zinazoambatana na hayo mafuta. binafsi mafuta tu yalinipa intended results. shida picha sikupiga ila nywele zillirefuka na kuwa na ubora mzuri kwa muda mchache.
Kumbuka si kila product inamkubali kila mtu. So tatizo sidhani kama ni matumizi yao bali product yenyewe.

Binafsi siamini product inaweza kusaidia nywele katika ukuaji au afya bali natumia products katika kustyle na muonekano pekee! Afya ya nywele inaanzia ndani.
 
Hongera ndugu...mimi ni kipilipili kile type Z..yani hata nywele ifike mgongoni inajicoil inaonekana kama kiafro kifupi. Kama ziko kama aunt jackies ntajaribu kununua leave in yake nione. Shea moisture ni 45,000 hadi 50,000 tshs ila naona zinastahili sababu hata harufu yake si mchezo na ukitumia kidogo tu inaleta matokeo.
Ziko kama aunt Jackie's... lakini kama umezoea harufu nzuri nzurii...hio ina harufu ngumu kidogo.
Ooh kama kwa hiyo bei ukitumia kidogo inaleta matokea it worth it...nitajaribu curling jelly yao.

Hahaha kipilipili type Z
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom