Nyumba zote zirudishwe serikalini

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,007
...bila kujali kama zimelipiwa au la, maana ziliuzwa katika mazingira ya kutatanisha

Posted Date::10/15/2007
Wasiolipia nyumba za serikali kunyanganywa
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

SERIKALI imetangaza kuzirejesha nyumba zake zote, ambazo zitakuwa hazijalipiwa ndani ya kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa.

Nyumba hizo ni zile ambazo ziliuzwa kwa baadhi ya wafanyakazi chini ya serikali ya awamu ya tatu.

Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge, alithibitishia jijini Dar es Salaam jana kuhusu mpango huo wa kutaka kuzirejesha nyumba ambazo hadi sasa hazijalipiwa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ndani ya Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA), kila aliyeuziwa nyumba anatakiwa kulipa fedha hizo au kumaliza deni lake.

Taarifa hiyo iliongeza kwamba, wote waliouziwa nyumba wamepewa wiki mbili kuhakikisha wanalipa fedha hizo.

"Fedha hizo zinapaswa kulipwa katika maeneo ambayo yametajwa, kupitia akaunti za benki".

Akizungumzia zaidi suala hilo, Chenge alisema pamoja na mpango mwingine wa serikali kuongeza ujenzoi wa nyumba zake, hizo ambazo ziliuzwa zitarejeshwa iwapo wahusika watashindwa kulipa na kisha kuuzwa kwa wafanyakazi wengine wenye uwezo.

Chenge alifafanua kwamba, kwa wale ambao pia watakuwa wameanza kulipa kidogo, serikali itataka kuona mipango yao ya kulipa ikoje kwa mujibu wa mikataba ili kama hatua zikichukuliwa zifanyike kwa mujibu wa makubaliano.

Alisema hatua zote zitachukuliwa kwa mujibu wa mikataba na kusisitikza kuwa wale ambao hawaanza kuliupa nyumba zitachukuliwa na kuwapa wengine wanaozihitaji wenye uwezo wa kulipa.

"Wapo ambao wanahitaji na wana uwezo wa kulipa, tunajua mishahar a yetu ni midogo, lakini tutaangalia zaidi mikataba inasemaje, ndipo tutachukua hatua," alisema Chenge.
 
mazingaombwe mengine haya,hivi nani atajua nani kalipa na nani ajalipa, hii danganya toto wasiwe wanaandika kwenye magazeti kwani ni kuwakumbusha watu msiba uliokwisha pita.
 
Wanataka kutudanganya tu, tuone kuna kitu wanafanya. Ukweli ni kwamba wao moja, wanalindana.
 
kichwa cha habari na maelezo yaliyotolewa hayaendani, wanataka kupoteza lengo tu kwa habari kama hizi.
 
Wamenunua Nyumba Oysterbay kule kwa bei cheee. I guess everybody need to return those house and rebuy again.
 
...bila kujali kama zimelipiwa au la, maana ziliuzwa katika mazingira ya kutatanisha

Bubu wee tulia kwani utafurahi siku chache kabla ya kuelekea uchaguzi 2010, nasikia muungwana kaiweka kibindoni na atakupeni kwa wakati muafaka ili apewe na ashinde kwa kishindo

Source.....speculation tu
 
Date::12/18/2008
Walionunua nyumba za serikali hatarini kupokonywa
Jackson Odoyo na Ellen Manyangu
Mwananchi

SAKATA la ununuzi wa nyumba za serikali limeibuka tena baada ya Mamlaka ya Ujenzi wa Nyumba za Serikali (TBA) kutishia kuvunja mikataba ya watumishi 4,517 ambao hawajamaliza kulipa madeni ya nyumba walizouziwa kwa mkopo.

TBA pia imesema watumishi hao wanakabiliwa na uwezekano wa kulipa asilimia tano ya thamani ya nyumba zao, ikiwa ni fidia ya kuvunja mkataba, pamoja na kulipa kodi ya pango tangu waliposaini hadi kuvunjwa kwa mikataba yao.

Idadi hiyo ni kati ya watumishi 7,159 waliouziwa nyumba za serikali na mashirika ya umma kwa mkataba wa malipo ya miaka 10 tangu zoezi hilo lilipoanza mwaka 2002.

Hatua hiyo imefikiwa na TBA baada ya watumishi hao kuchelewa kulipa kiasi cha Sh18.37 bilioni za madeni ya nyumba walizouziwa kwa mkopo.

Akizungumza na Mwananchi jana ofisini kwake, mtendaji mkuu wa mamlaka hiyo, ambayo iko chini ya Wizara ya Miundombinu, Makumba Kimweri alisema hadi sasa imesalia miaka mitatu kabla ya kumalizika kwa mikataba yao, lakini kiwango kilichokusanywa ni tofauti na matarajio yao.

Alisema matarajio ya mauzo yalikuwa ni Sh57.06 bilioni, lakini akasema: "Tangu kuanza kwa zoezi hili mwaka 2002 hadi Agosti 2008, kiasi cha fedha kilichopatikana ni Sh38 bilioni ambazo ni sawa na asilimia 67.8."

Kimweri alisema iwapo watumishi hao wataendelea kusuasua, TBA haitasita kuchukua hatua.

"Kwa wale ambao hawatalipa sheria iliyopo ni kufutiwa mikataba na kulipia asilimia tano ya thamani ya nyumba kama fidia ya kuvunja mkataba," alisema Kimweri na kuongeza:

"Mpangaji atalazimika kulipa kodi ya pango tangu alipoingia mkataba hadi mkataba huo ulipovunjwa.

"Kwa kuwa muda wa mkataba haujamalizika, TBA inaendelea kuwakumbusha watumishi ambao hawajamaliza kulipa madeni yao."

Jumla ya nyumba zilizouzwa mpaka sasa ni 7,159 na tayari mamlaka yake imejenga nyumba 910 kwa gharama ya Sh37.88 bilioni baada ya kuanzishwa kwa mamlaka hiyo.

Hata hivyo, taarifa kutoka ndani ya mamlaka hiyo zinaeleza kuwa kati ya watumishi 2,642, waliomaliza kulipa madeni ya nyumba hizo ni watumishi wa kawaida wakati wadaiwa sugu ni baadhi ya mawaziri na wabunge.

Chanzo hicho pia kilizidi kubainisha kwamba pamoja na jitihada za mamlaka hiyo kuwakumbusha wadaiwa hao mara kwa mara juu ya madeni hayo, ulipaji wao umekuwa wa kusuasua.

"Kwa mujibu wa mkataba, malipo ya nyumba hizo yanatakiwa yaanze mara moja baada ya watumishi hao kupewa nyumba, lakini mpaka sasa ni miaka saba kasi ya malipo bado si ya kuridhisha," alisema mtoa habari wetu.
 
Hizi nyumba ziliuzwa kwa utaratibu wa " Sadakalawea aminaaa.. mwenye kupata apateeeeeee.... mwenye kukosa akoseeee!
 
Back
Top Bottom