Google Diggers
JF-Expert Member
- Aug 29, 2015
- 940
- 1,123
Title inajielezea, niende kwenye mada hii. Wakati naishi nyumba ya Mama mmoja mumewe aliishatangulia mbele ya haki. Allah amlipe mema.
Watoto wa nyumba hiyo hawakunipendeza hata kidogo. Wana jeuri, dharau, majivuno, kibri na kujiona werevu na hawajui wenye shida hawafikirii hata aliyejenga nyumba yao ametangulia, na sote tutarejea.
Kila utakalofanya halikubaliki, utakapopita haparuhusiwi, utakaposhika utachafua, wana kutreat kama mtu wa chini sana wakati hawakujui, hawajui unafanyashughuli gani, una kausafiri kako parking hairuhusiwi watoto wana nongwa hao sijapata kuona. Yaani hawa siku atapangisha ntu na silaha anawafyekelea mbali
Niliishi nyumba za kupanga yapata miaka 15. Nyumba hiyo ya #9 katika makazi niliyopata kukaa ile ilikuwa moto wa kuotea mbali. .
Kazi yao kuchungulia madirishani kuwatazama wapangaji, kutunga sheria mpya kila uchao.
Ukizaliwa kwenye familia yenye uwezo wazazi wakashindwa kukulea na maadili ya kibinadamu utachekesha sana. Sina hakika kama wale vijana watamudu maisha yao. Kwa namna walivyokuwa mwiba, unajiuliza kama wanajua watatakiwa waje kuishi na familia zao, wazitunze, wapate kazi, wajenge, nk.
Usiombee kuwa na watoto kwenye nyumba za kupanga, katika mazingira yale ukaondoka kwenda kibaruani, familia yako huko nyuma unaona kabisa itakerwa, ukirudi kazini watoto wanaanza kukushitakia, Mama tumenyimwa maji, Mama tumezimiwa umeme, baba hivi mara vile.
Hivi nchi hii haina sheria kweli kuwalinda wapangaji?
Watoto wa nyumba hiyo hawakunipendeza hata kidogo. Wana jeuri, dharau, majivuno, kibri na kujiona werevu na hawajui wenye shida hawafikirii hata aliyejenga nyumba yao ametangulia, na sote tutarejea.
Kila utakalofanya halikubaliki, utakapopita haparuhusiwi, utakaposhika utachafua, wana kutreat kama mtu wa chini sana wakati hawakujui, hawajui unafanyashughuli gani, una kausafiri kako parking hairuhusiwi watoto wana nongwa hao sijapata kuona. Yaani hawa siku atapangisha ntu na silaha anawafyekelea mbali
Niliishi nyumba za kupanga yapata miaka 15. Nyumba hiyo ya #9 katika makazi niliyopata kukaa ile ilikuwa moto wa kuotea mbali. .
Kazi yao kuchungulia madirishani kuwatazama wapangaji, kutunga sheria mpya kila uchao.
Ukizaliwa kwenye familia yenye uwezo wazazi wakashindwa kukulea na maadili ya kibinadamu utachekesha sana. Sina hakika kama wale vijana watamudu maisha yao. Kwa namna walivyokuwa mwiba, unajiuliza kama wanajua watatakiwa waje kuishi na familia zao, wazitunze, wapate kazi, wajenge, nk.
Usiombee kuwa na watoto kwenye nyumba za kupanga, katika mazingira yale ukaondoka kwenda kibaruani, familia yako huko nyuma unaona kabisa itakerwa, ukirudi kazini watoto wanaanza kukushitakia, Mama tumenyimwa maji, Mama tumezimiwa umeme, baba hivi mara vile.
Hivi nchi hii haina sheria kweli kuwalinda wapangaji?