Nyumba za kupanga ni vijiji ndani ya miji

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Huku kwetu Kwamtogole nyumba za kupanga ni kiinua mgongo endelevu. Haya yalianza enzi za mkoloni, makuli wengi wa bandarini ndiyo walikuwa Baba wenye nyumba.

Siku hizi wengi hupenda kuchukua chumba na sebule. Katika chumba na sebule Hii ni nyumba inayostir familia ya takriban watu watano-sita. Baba, mama na watoto watatu. Hii ni kaya ndani ya nyumba na unaweza kukuta nyumba ina kaya sita. Nyumba moja ina watu 30-40 wanaotumia maji, choo, na umeme kila siku.

Baba wenyenyumba wangepaswa kuwa sehemu ya uongozi wa serikali ya mtaa. Hawa wana uwezo wa kutambua wapangaji na wageni wa wapabgaji wao. Ni watu muhimu katika kuzuia vitendo vya uhalifu.

Wakati wa kupiga kura, mwenyenyumba ana nafasi kubwa ya kushawishi hasa wake wa wapangaji wake wakipigie chama gani. Anajua hali zao kiuchumi, akiweka siasa kidogo amepata wapiga kura kumi ndani ya nyumba moja.

Katika mipango ya maendeleo serikali izingatie idadi ya watu huku kwetu Uswahilini ni mara kumi ya ushuani.
 
Dah hao ndio walala hoi wa third weld countries. Cheki hapo chini walala hoi wa mamtoni watu wa mbele sisi wabeba bksi. Hako ni kastudio apartment ni chumba kimoja tuu sebule hapo hapo choo ndani kwa ndani. Umeme maji kamwe haukatiki.
6b027c9ec7f86974a0db2c98ff51db3ec73e2318.jpg
4adcf7cc9aa549814e462f8ff28ccce6536ad629.jpg
5fc4c747952edc410b11dfd317d5187d6912e398.jpg
 
Namkumbuka rafiki yangu aliyeishi Mburahati mfanyakazi wa TRA. Alitembea na wake wa wapangaji wake wote. Kila akienda chooni asubuhi anashika elfu ishirini mkononi. Mwanamke atakayemkuta anafagia kule uwani anapewa 20 thou. Wanawake wakawa wanagombania zamu za usafi. Waume zao walipostuka kwanini wake zao wanagombania zamu za usafi ndio siri ilipofichuka na wapangaji wote kuhama.
 
Namkumbuka rafiki yangu aliyeishi Mburahati mfanyakazi wa TRA. Alitembea na wake wa wapangaji wake wote. Kila akienda chooni asubuhi anashika elfu ishirini mkononi. Mwanamke atakayemkuta anafagia kule uwani anapewa 20 thou. Wanawake wakawa wanagombania zamu za usafi. Waume zao walipostuka kwanini wake zao wanagombania zamu za usafi ndio siri ilipofichuka na wapangaji wote kuhama.
hatari sana hiyo
 
Kuna kipindi napanga ndani ya jiji la Dar es Salaam enzi hizo nilikua na vijipesa. Basi kuna siku nimetoka mjini nikakuta gari la kuku limeanguka watu wanajichukulia kuku. Na mimi nikachukua kuku watatu. Kufika nyumbani nikachinja 1 wale wawili nikawapa wapangaji wenzangu ila sikuwaambia kwamba nimewaokota. Wake za wapangaji wakapika kitoweo safi cha kuku, mume wa mmoja kurudi akakuta mkewe kapika kuku. Kumuuliza huyu kuku vipi wakati nimeacha hela ya dagaa? Mwanamke kasema nimepewa na ndugu DECEIVER. Heh unasemaje wewe? Jamaa kuku hakula na ndani ya siku tatu alikua amehamia kusikojulikana.
 
Kipindi hichoo napanga. Kuna mpangaji wa kike ambaye alikua hajaolewa. Wanawake wenzake wakawa wanamshuku kwamba anachukua waumenzao halafu alikua huko nyuma ni mashallah. Enzi hizo kulikua hakuna skin tight wanawake walikua wanavaa kitu inaitwa under skirt. Basi alivyo fua underskirt na kuianika nje wenzake wakaificha. Enzi hizo ukitaka kumroga mwanamke iba na umpelekee mganga nguo yake ya ndani. Eh bwanawee. Yule mwanamke hakupata amani mpaka akahama.
 
Uswahilini nakuwa napaangalia kwa jicho la tofauti sana na hizi Mamlaka za serikali kutoa huduma. Mfano hiyo nyumba moja yenye vyumba 10 ina watu 30, kila chumba kingewekwa Meter ya Luku, tuseme mfano kila siku mpangaji mmoja anatumia umeme wa elfu 1, hivyo kwa mwezi anatumia umeme wa elf 30. Au 20. Tanesco wangekusanya pesa kiasi gani kila mwezi!?
 
Enzi hizoo napanga. Kuna jamaa alikua anamtaka mke wa mpangaji mwenzie. Sasa yule mama kamwambia jamaa nitakupa mzigo humu humu ndani tena jamaa akiwepo. Tukafikiri urongo. Siku mwenye mke karudi kaambiwa kwanza akaoge kwenye mabafu yetu passport size. Mwenye mke kuingia bafuni tu mkewe kaondoka na taulo, maana yake mwenye mke hawezi kutoka mpaka apelekewe taulo au kanga na mkewe. Mtu mwingine yeyote angepeleka taulo ingekua hadithi nyingine. Basi dowezi likala mzigo wakati huko nje mwenye mali hawezi kutoka bafuni. Dowezi kala mzigo tani yake alipomaliza mke kampelekea mumewe taulo na jamaa likatoka huku mali zake zilishaliwa.
 
Uswahilini nakuwa napaangalia kwa jicho la tofauti sana na hizi Mamlaka za serikali kutoa huduma. Mfano hiyo nyumba moja yenye vyumba 10 ina watu 30, kila chumba kingewekwa Meter ya Luku, tuseme mfano kila siku mpangaji mmoja anatumia umeme wa elfu 1, hivyo kwa mwezi anatumia umeme wa elf 30. Au 20. Tanesco wangekusanya pesa kiasi gani kila mwezi!?
Shida ni hizo gharama za kuipata hio mita.Mita na nguzo vingetowela bure zijilipe zenyewe
 
Back
Top Bottom