Nyumba yangu Inavuja, Msaada wa namna ya kuziba

kipusy

JF-Expert Member
May 7, 2010
639
321
Poleni kwa msiba wa kuondokewa na Mzee wetu Kingunge Ngombale Mwiru. Nakuja kwenye mada, Nyumba yangu inavuja, mafundi hawakunitendea kazi vizuri na kusababisha nyumba kuvuja hasa kwenye misumali ilipogongelewa. Naomba msaada kwa walio wazoefu na marekebisho ya paa kuvuja NITUMIE DAWA (sealant) GANI ILI KUDHIBITI MIVUJO?

Asanteni.
 
Dah... "Kuvuja kwa nyumba" kuna maana nyingi.....hasa kwa watu wazima
 
Ina onekana wewe bahiri,hukulipa vizuri mafundi ndio maana wakafanya hovyo hovyo,ita fundi mpe kazi yeye atajua ataziba na nini hata akiziba kwa mate yake shida ni nini? Wewe si unataka paa yako isivuje?? Au unataka tukutajie hapa ili uende kununua na kuziba mwenye?
Acha hizo toa ridhiki boss!!
 
Hakuna dawa ya kuziba iliyo nzuri huwa ni dawa za kufoji tu nyingi hata ukiweka baada ya mda mfupi inatoka soln ni kufumua tu na kupiga upya. Bati za vigae tu ndo vina dawa nzuri ya kuzibia
 
Hakuna dawa ya kuziba iliyo nzuri huwa ni dawa za kufoji tu nyingi hata ukiweka baada ya mda mfupi inatoka soln ni kufumua tu na kupiga upya. Bati za vigae tu ndo vina dawa nzuri ya kuzibia

Nifumue msauzi kaka hasara kubwa sana
 
Ina onekana wewe bahiri,hukulipa vizuri mafundi ndio maana wakafanya hovyo hovyo,ita fundi mpe kazi yeye atajua ataziba na nini hata akiziba kwa mate yake shida ni nini? Wewe si unataka paa yako isivuje?? Au unataka tukutajie hapa ili uende kununua na kuziba mwenye?
Acha hizo toa ridhiki boss!!

Niliwalipa hela nzuri tu bosi, sema walikua wazugaji.
 
Back
Top Bottom