Nyumba ya Sanaa inabomolewa!

kuna vitu vinanikeraga sana, eti preserve nyumba ya sanaa for heritage, usiweke mradi wa umeme kihansi, utaua vyura, usipitishe barabara kandokando ya serengeti, utabughudhi wanyama......usipofikiria sana utagundua wazungu wanatuona sisi waafrika kama makumbusho flani hata mahitaji yetu ya kibinadamu yanapimwa katika mtazamo huo.. vunja weka vitu vya maana hao vyura wa kihansi waite wazungu wakaweke huko kwao sisi tunao wakutosha, na hiyo nyumba ya sanaa inafaida gani kwa mtanzania wa kawaida?vitu vyote vinapatikana slipway,makumbusho,bagamoyo hakuna sababu ya kuwa nazo kama uyoga kila sehemu.
Unajua jamani tusiongee kama walevi humu ndani, ndio maana hapa pakaitwa Home of Great Thinkers!

Ukiongelea Msanii wa Kuchonga vinyago, Tingatinga na wengine wanaofanana hao ni watanzania nia wa Kawaida kabisa, au sijui ulikuwa una maana ipi? Nyumba ya Sanaa ilikuwa ya muhimu sana kwao kwa ajili ya kutangaza sanaa zao, taifa kwa ujumla, vilevile kuvumbua na kukuza wasanii wachanga, Watanzania wengi wanachukulia sanaa hasa za mikono ni jambo lisilo na umuhimu, lakini nakwambia sanaa kama ya uchoraji ina thamani yake kubwa sana katika jamii.

Katika kampeni za kikwete mwaka huu alipata kuzungumzia suala la kukuza sanaa akisema kwamba katika nchi zilizoendelea maendeleo yake huletwa na wasanii sababu ndio walipa kodi wakuu, na kwama nasi tunapaswa kuiga mfano huo kwa kuwathamini wasanii: na hivi ndivyo alivyoanza!!
 
Nimepitia mawazo yote mpaka muda huu sijaona sehemu ambayo inhusiha nyumba ya sanaa na Baraza la Sanaa Tanzania(BASATA)...nimechanganyikiwa naomba msaada kabla ya kuendelea. Naomba kujua uhusiano uliopo katika ya hivyo vitu viwili, BASATA wanasemaje kuhusu issue hii yote. Na hawa wasanii sioni sehemu kuonyesha barua yao ilikuwa na baraka za BASATA....Naomba kuwasilisha.
NYUMBA YA SANAA siyo sehemu ya BASATA, ni taasisi huru iliyoundwa kwa minajili ya kusaidia na kuendeleza.

BASATA walishapelekewa hii kadhia miaka mitatu nyuma mpaka leo hawajafanya lolote. mpaka waziri alishindwa kufanya kitu ndo maana ilibidi mamlaka ya juu iingilie kati.

BASATA wangeliweza kupeleka maombi au mapendekezo ngazi za juu lakini wamekuwa wakimya ktk hili.
Kuna Kinondoni Young Artists Association ambayo ina jengo lake maeneo ya kinondoni, taasisi imezimia na majengo yanahodhiwa na watu binafsi bila hata BASATA kuingilia kati. Ukisubiri BASATA nakwambia Yesu atarejea bila anything to happen
 
Workshop ya Tingatinga pale morogoro store mhindi ananyemelea, BASATA hawana kitu cha kufanya wao wamekaa tu hawawasaidii hawa watu. Tatizo ni lile lile nani anateua baraza la sanaa na anateua kwa minajili ya nini. Ukijibu hayo maswali utapata jibu la kwa nini nyumba ya sanaa inabomolewa.

Constitution of Council
(1) The Council shall consist of–
(a) a Chairman, who shall be appointed by the President; and who shall hold office for a period of three years and not exceeding six years unless it is necessary or desirable to do so;
(b) twenty-nine other members who shall be appointed by the Minister.

sheria haiweki qualifications za hao members na huyo chairman wao, kwa hiyo wanaochaguliwa hawajui lolote kuhusu sanaa etc
 
Unajua jamani tusiongee kama walevi humu ndani, ndio maana hapa pakaitwa Home of Great Thinkers, Ukiongelea Msanii wa Kuchonga vinyago, Tingatinga na wengine wanaofanana hao ni watanzania nia wa Kawaida kabisa, au sijui ulikuwa una maana ipi? Nyumba ya Sanaa ilikuwa ya muhimu sana kwao kwa ajili ya kutangaza sanaa zao, taifa kwa ujumla, vilevile kuvumbua na kukuza wasanii wachanga, Watanzania wengi wanachukulia sanaa hasa za mikono ni jambo lisilo na umuhimu, lakini nakwambia sanaa kama ya uchoraji ina thamani yake kubwa sana katika jamii, Katika kampeni za kikwete mwaka huu alipata kuzungumzia suala la kukuza sanaa akisema kwamba katika nchi zilizoendelea maendeleo yake huletwa na wasanii sababu ndio walipa kodi wakuu, na kwama nasi tunapaswa kuiga mfano huo kwa kuwathamini wasanii: na hivi ndivyo alivyoanza!!

Nilitaka kukaa kimya lakini nadhani inabidi nikupe challenge uende pale moven pick ukawaangalie hao unawaita watanzania wa kawaida kisha pitia kwetu hapa bagamoyo utulinganishe, hicho ni kijiwe cha watu wachache kwa manufaa yao, kivunjwe ijengwe benki itafuaidishe wengi na hao kama wanataka kuuza vinyago vyao maeneo yapo mengi, waje bagamoyo tena huku wateja wengi zaidi.
 
Nadhani umefika wakati Watanzania wanatakiwa kusimama na kulaani vitendo kama hivi. Ni wakati muhimu sana kwa vijana na lazima nyumba hiyo itumike kama sehemu au idara ya wizara kamili ya Wizara ya Habari, Vijana na Michezo inayoongozwa na Nchimbi...

Sikupenda mabadiliko ya wizara hii mwaka huu kuhusiana na vijana kutoka ilivyokuwa mwanzoni ambapo ilikuwa wizara ya Kazi, Ajira na maendeleo ya vijana.
 
Hamna kitu hawa integrated hamna kitu bahari beach imedoda... world economy haijatulia watachemka.. and guess who is in bed na hawa wasomali... LOWASSA...
 
Hatujatatua tatizo la infrastructure lakini bado tunataka kujenga maghorofa kati kati ya jiji! Kuhusu heritage, nchi ambayo iko tayari kujenga airport na kupasua barabara kati ya Sengeti haiwezi kunishangaza kwa lolote. Tumeiharibu Dare es Salaam, tunakimbilia kuharibu tena Kivukoni, hako ka Nyumba ya Sanaa katatushinda kweli. Wakavunje tuu, si tunadhani maghorofa ndio maendeleo?

Amandla......
 
Ni wakati wao wa mavuno, kuanzia sasa mpaka 2013 ni mavuno. Baada ya hapo wataanza rehearsal kwa ajiri ya 2015 kwa kufanya sisi wahasibu tunachoita Window Dressing (yaani danganya toto)
 
Hiyo nyumba ya sanaa yenyewe lilikuwa wazo la mzungu. Kama kweli mnapenda sanaa na utamaduni wenu kwanini mnakataa kukaa vijijini kwenu? Hata mkipata likizo hamtaki kwenda. Kwenye majumba yenu mmepamba vitu vya kizungu. Wacheni wajenge benki tu.
 
Hiyo nyumba ya sanaa yenyewe lilikuwa wazo la mzungu. Kama kweli mnapenda sanaa na utamaduni wenu kwanini mnakataa kukaa vijijini kwenu? Hata mkipata likizo hamtaki kwenda. Kwenye majumba yenu mmepamba vitu vya kizungu. Wacheni wajenge benki tu.

Yaani hapo umetema kama mimi ninavyotema. Straight up....no sugar coating.
 
kuna vitu vinanikeraga sana, eti preserve nyumba ya sanaa for heritage, usiweke mradi wa umeme kihansi, utaua vyura, usipitishe barabara kandokando ya serengeti, utabughudhi wanyama......usipofikiria sana utagundua wazungu wanatuona sisi waafrika kama makumbusho flani hata mahitaji yetu ya kibinadamu yanapimwa katika mtazamo huo.. vunja weka vitu vya maana hao vyura wa kihansi waite wazungu wakaweke huko kwao sisi tunao wakutosha, na hiyo nyumba ya sanaa inafaida gani kwa mtanzania wa kawaida?vitu vyote vinapatikana slipway,makumbusho,bagamoyo hakuna sababu ya kuwa nazo kama uyoga kila sehemu.

Naomba kajichunguze maneno yako mazito. Nadhani haitachukua muda utasema zile hifadhi za makaburi zivunjwe kwa sababu walikwisha kufa.
 
Jamani tuwe waangalifu kidogo kuhusu ili suala. Sijajua owners wa hiyo Intergrated Property LTD ni kina nani ( niliwahi kusikia ni kina Lowassa), lakini overall as long as Nyumba ya Sanaa imeretain ownership ya jengo zima to the tune of 25%, SIONI TATIZO.

Ni lazima tu nyumba ya sanaa imake sure ground floor inapata hiyo 25% na kuweka hayo maduka ya wasanii na mambo ya usanii nk, At the same time watapata percent ya rent hayo maghorofa ya juu 25%.

Hii ni win win situation kwa sababu kama kodi za nyumba zinalipwa TZ, TRA watapata nao pesa, watu wengi watapata sehemu za biashara including mabenki Nk

Naona tunadiscuss as if Nyumba ya Sanaa imeuza kiwanja, nionavyo mimi ni kuwa Nyumba ya Sanaa imeingia Ubia kuongeza mapato
 
Yaani hapo umetema kama mimi ninavyotema. Straight up....no sugar coating.

NNgabu:

Hakuna sugar coating. Kama watu wanapenda sanaa yao, basi onyesheni. Kitu ambacho ningekubaliana na wasanii hapa ni kushindwa kabisa kuendeleza maeneo ya makazi na biashara. Eneo lile limekaa vizuri kwa sababu mzungu alipima na kuacha viwanja. Na kama toka nchi imepata uhuru watu wangekuwa wanapima viwanja basi majengo ya biashara yangejengwa sehemu nyingine kama vile Sinza, Kongowe au Tabata.
 
Hamna kitu hawa integrated hamna kitu bahari beach imedoda... world economy haijatulia watachemka.. and guess who is in bed na hawa wasomali... LOWASSA...

Duh huyo mheshimiwa yuko kila kona yani hata deal ya buku mbili hataki impite kazi kweli kweli....
 
kuna vitu vinanikeraga sana, eti preserve nyumba ya sanaa for heritage, usiweke mradi wa umeme kihansi, utaua vyura, usipitishe barabara kandokando ya serengeti, utabughudhi wanyama......usipofikiria sana utagundua wazungu wanatuona sisi waafrika kama makumbusho flani hata mahitaji yetu ya kibinadamu yanapimwa katika mtazamo huo.. vunja weka vitu vya maana hao vyura wa kihansi waite wazungu wakaweke huko kwao sisi tunao wakutosha, na hiyo nyumba ya sanaa inafaida gani kwa mtanzania wa kawaida?vitu vyote vinapatikana slipway,makumbusho,bagamoyo hakuna sababu ya kuwa nazo kama uyoga kila sehemu.

wewe na ndio maana hata jina lako umeshindwa kujipa la kutoka huko kwenu, kwa maeneo makubwa tukiyonayo tunakosa pa kuanzisha miradi mipya ila kwa kuvunja iliyopo kuweka mipya? na habari hiyo ya serengeti, tunafanya utalii kwa asili ya eneo husika sasa unavyongangania kupitisha barabara katikati hiyo biashara asilia unaifanyaje? we can do better than this what we are doing ni suala la kufikiria kiupana zaidi na sio kulazimisha jinsi hawa wageni wanavyotaka bila ya sisi kuangalia yetu zaidi. Free your mind from mental slavery kwanza. and be proud of who you are.
 
Yaani hapo umetema kama mimi ninavyotema. Straight up....no sugar coating.

Hivi hizo habari za benki ni za kiafrika? sio system za kizungu? nipe mfano wa benki za kiafrika za kiasili. acheni kuzungumza kwa urefu wa pua. kwani huduma za benki lazima ziwe hapo katikati ya mji? mbona wasije kujenga hizo benki huko bagamoyo/ chalinze kuwarahisishia huduma kama mnavyotaka vinyago vije huko?
 
Jamani tuwe waangalifu kidogo kuhusu ili suala. Sijajua owners wa hiyo Intergrated Property LTD ni kina nani ( niliwahi kusikia ni kina Lowassa), lakini overall as long as Nyumba ya Sanaa imeretain ownership ya jengo zima to the tune of 25%, SIONI TATIZO.

Ni lazima tu nyumba ya sanaa imake sure ground floor inapata hiyo 25% na kuweka hayo maduka ya wasanii na mambo ya usanii nk, At the same time watapata percent ya rent hayo maghorofa ya juu 25%.

Hii ni win win situation kwa sababu kama kodi za nyumba zinalipwa TZ, TRA watapata nao pesa, watu wengi watapata sehemu za biashara including mabenki Nk

Naona tunadiscuss as if Nyumba ya Sanaa imeuza kiwanja, nionavyo mimi ni kuwa Nyumba ya Sanaa imeingia Ubia kuongeza mapato
Mkuu unaongea kama vile huijui Bongo babuuu! unakumbuka uwanja wa mpira wa Pazi kilitokea nini?. Kweli Hotel limejengwa na baabu kubwa lakini ndio hivyo wamiliki wanakwepa kodi na sehemu yote inamilikiwa na Hotel wakiuziana kila baada ya miaka mitano. On the other hand, mchezo wa basketball umedumaa na hivi sasa upo ktk hatua za kufa kabisaaa.

Hii scandal imeanza zamani hivyo labda jikumbusheni kidogo:- Bofya
 
NNgabu:

Hakuna sugar coating. Kama watu wanapenda sanaa yao, basi onyesheni. Kitu ambacho ningekubaliana na wasanii hapa ni kushindwa kabisa kuendeleza maeneo ya makazi na biashara. Eneo lile limekaa vizuri kwa sababu mzungu alipima na kuacha viwanja. Na kama toka nchi imepata uhuru watu wangekuwa wanapima viwanja basi majengo ya biashara yangejengwa sehemu nyingine kama vile Sinza, Kongowe au Tabata.

Ujue hata hoteli ya Sheraton wakati inataka kujengwa pale palikua na viwanja vya wazi vya michezo, na kulikua na viwanja viwili vya basketball ambako timu ya Pazi ndio ilikua inafanya mazoezi na vijana wengi walikua wanajifunza mchezo wa kikapu pale bure, michuano ya basket mingi ilikua inafanyika pale kati ya timu za mashirika, jeshi wizara na hata timu ya taifa ya Misri iliwahi kucheza mechi pale na Pazi tena usiku na taa zilikuwepo miaka ile. wakaja wakubwa na sera kama hizi na kukawa na ugomvi mkubwa watu (wanamichezo) wakitetea viwanja vyao ila ikawa bure hoteli ikajengwa, Nyerere aliwahi sema mtu akikupa wazo la kipuuzi na akijua wewe unajua ni la kipuuzi na ukalikubali atakudharau maisha. What is happening ti TZ?
 
Nadhani umefika wakati Watanzania wanatakiwa kusimama na kulaani vitendo kama hivi. Ni wakati muhimu sana kwa vijana na lazima nyumba hiyo itumike kama sehemu au idara ya wizara kamili ya Wizara ya Habari, Vijana na Michezo inayoongozwa na Nchimbi...
Sikupenda mabadiliko ya wizara hii mwaka huu kuhusiana na vijana kutoka ilivyokuwa mwanzoni ambapo ilikuwa wizara ya Kazi, Ajira na maendeleo ya vijana.
Jamani mbona jumba hilo liliisha achana na biashara ya wasanii na usanii?
Mara ya mwisho nilipitia pale palikuwa ni mahali pa mvinyo wa bei mbaya, makutano ya sister-do waendeshao mb na wanabees wa mtaani. Kumuenzi JKN kulifutika tangu awamu ya pili, sema tu wengi wetu inakuwa ni vigumu kulikubali hilo na mpango wa kulipinga hatuna.
 
Back
Top Bottom