Nyumba ya Mwalimu Julius Nyerere Maduka Sita, Magomeni

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,900
30,235
NYUMBA YA MWALIMU NYERERE MAGOMENI MADUKA SITA 1955

Rafiki yangu kanipatia picha ya nyumba aliyokaa Mwalimu Nyerere Magomeni Maduka Sita.

Mwalimu Nyerere anaonekana nje ya nyumba yake akiingia ndani.

Picha ya nyumba hii nimeitafuta kwa miaka mingi bila mafanikio.

Mwalimu baada ya kutoka UNO mwaka wa 1955 waajiri wake wamishionari hawakuweza kumstahamilia wakamwambia achague siasa au kazi.

Halmashauri Kuu ya TANU chini ya Mwenyekiti wake Clement Mohamed Mtamila ikakutana nyumbani kwa Mzee Mtamila Mtaa wa Kipata na Sikukuu kujadili barua ya Mwalimu Nyerere aliyoandikiwa na mwajiri wake.

Uamuzi ulikuwa Mwalimu aache kazi.

Mwalimu akaacha kazi na kuhamia nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu si mbali sana na nyumba ya Mzee Mtamila.

Inasemekana Mwalimu aliishi na Abdul Sykes kwa miezi mitatu hadi TANU walipomtafutia nyumba hiyo hapo juu Magomeni Maduka Sita.

Nyumba hii haipo hivi sasa kwani ilivunjwa.

Picha hiyo hapo chini ya nyumba ya Mwalimu ni kiwanja ilipokuwa nyumba hii.

Picha hii iliyopigwa tarehe 15 June 2015 inaonyesha kiwanja kimezungushwa mabati kwa ajili ya ujenzi wa ghorofa.

Picha ya mwisho ni nyumba ya Abdul Sykes mbayo Mwalimu Julius Nyerere aliishi kabla ya kuhamia Magomeni.
 
Nyumba ya Julius Nyerere Magomeni Maduka Sita 1955

Screenshot_20201103-220005.jpg
 
Asante mkuu kwa historia nzuri, ila hizo picha ungeleta hapa hapa JF tumalizane na hii historia humu humu mpaka twende fcbk na wengine hatuna account huko na picha tunazitaka sasa itakuaje tena?
 
Eneo hili sitoacha kukupongeza na kujifunza kutoka kwako.

Mengine waachie wanasiasa.

Hili jengo pichani inaonyesha Mwalimu alikuwa anaingia kwenye store ya kununua mahitaji au duka. Pia inahitajika kutunzwa sana na kuwekwa bango ili watalii wa ndani na nje waitembelee.

Mzee Said hebu uende hapo utuletee picha ya hivi sasa
 
Eneo hili sitoacha kukupongeza na kujifunza kutoka kwako.

Mengine waachie wanasiasa.

Hili jengo pichani inaonyesha Mwalimu alikuwa anaingia kwenye store ya kununua mahitaji au duka. Pia inahitajika kutunzwa sana na kuwekwa bango ili watalii wa ndani na nje waitembelee.

Mzee Said hebu uende hapo utuletee picha ya hivi sasa
Yes, hata mie naona kuna kijiduka hadi mlangoni pana kibao cha cocacola, sasa hapa linakuja swali kama mwalimu alikuwa anaishi dukani? Au ni vipi?

Zaidi tunamshkuru mtoa post kwa historia nzuri japo picha imeleta utata!
 
Yes, hata mie naona kuna kijiduka hadi mlangoni pana kibao cha cocacola, sasa hapa linakuja swali kama mwalimu alikuwa anaishi dukani? Au ni vipi?
Zaidi tunamshkuru mtoa post kwa historia nzuri japo picha imeleta utata!
Ni kweli tumpe credit mzee Mohammed Said kwa kutuletea hii tafakuri ya kihistoria
 
Eneo hili sitoacha kukupongeza na kujifunza kutoka kwako.

Mengine waachie wanasiasa.

Hili jengo pichani inaonyesha Mwalimu alikuwa anaingia kwenye store ya kununua mahitaji au duka. Pia inahitajika kutunzwa sana na kuwekwa bango ili watalii wa ndani na nje waitembelee.

Mzee Said hebu uende hapo utuletee picha ya hivi sasa
Msanii hii nyumba haipo imevunjwa kuna jengo linaitwa Watumishi House.
 
Mzee nadhani kuna mengi nyuma ya pazia kuhusu uhuru wa tanganyika , kuna mzee huko tabora aitwaye (Bilali waikela ) anayo mengi sana kuhusu mwalimu na harakati hizi.

Kwa dk 10 tu alizo hojiwa na Millard ayo zinatosha kuonyesha mambo mengi yamefichwa na anamiaka 97 , uwezo wa kujieleza anao na anaeleweka ni vyema ukamtembelee.

Siku zake za kuishi ni chache(kwa fikra zetu za kibinadamu) , nafikiri itakua vyema kama tutapata mawili matatu
 
Mzee nadhani kuna mengi nyuma ya pazia kuhusu uhuru wa tanganyika , kuna mzee huko tabora aitwaye (Bilali waikela ) anayo mengi sana kuhusu mwalimu na harakati hizi

Kwa dk 10 tu alizo hojiwa na Millard ayo zinatosha kuonyesha mambo mengi yamefichwa na anamiaka 97 , uwezo wa kujieleza anao na anaeleweka ni vyema ukamtembelee

Siku zake za kuishi ni chache(kwa fikra zetu za kibinadamu) , nafikiri itakua vyema kama tutapata mawili matatu
Chizzo,
Nilisoma Nyaraka za Bilal Rehani Waikela katika Maktaba ya Muslim Student Association of the University of Dar es Salaam (MSAUD) miaka ya 1980s nikiwa mwanafunzi hapo chuoni na pia Katibu wa MSAUD.

Hizi nyaraka zilitakiwa zote zichomwe moto baada ya kumalizika mgogoro wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) na kuundwa BAKWATA.

Hii ilikuwa amri kutoka juu alivyonieleza Mzee Waikela.

Mzee Waikela yeye alikuwa katika Tume ya Mussa Kwikima iliyoundwa kutafuta suluhu ya mgogoro ule.

Mzee Waikela alizificha nyaraka zake zote pamoja na cutting za magazeti kwa miaka 20 kisha akazileta MSAUD kwa matunzo ili Waislam wajue ukweli wa mgogoro ule.

Wakati naandika kitabu cha Abdul Sykes nilisafiri hadi Tabora na nikafanya mahojiano na yeye nyumbani kwake pamoja na wazalendo wengine na wote wametangulia mbele ya haki kuhusu mchango wao katika kuunda TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Mzee Waikela akanieleza mambo mengi yaliyotokea hasa baada ya uhuru mwaka wa 1961 hadi kufikia mwaka wa 1968 EAMWS ilipovunjwa na serikali.

Waikela anasema sababu ilikuwa EAMWS chini ya uongozi wa Aga Khan, Tewa Said Tewa na Mufti Sheikh Hassan bin Ameir ilikuwa inajenga Chuo Kikuu na serikali haikupendezewa na jambo hili.

Historia hii ipo katika sehemu ya tatu na ya mwisho katika kitabu cha Abdul Sykes kilichochapwa London mwaka wa 1998.
 
Mzee nadhani kuna mengi nyuma ya pazia kuhusu uhuru wa tanganyika , kuna mzee huko tabora aitwaye (Bilali waikela ) anayo mengi sana kuhusu mwalimu na harakati hizi

Kwa dk 10 tu alizo hojiwa na Millard ayo zinatosha kuonyesha mambo mengi yamefichwa na anamiaka 97 , uwezo wa kujieleza anao na anaeleweka ni vyema ukamtembelee

Siku zake za kuishi ni chache(kwa fikra zetu za kibinadamu) , nafikiri itakua vyema kama tutapata mawili matatu
Mzee Bilal Waikela.
FB_IMG_1600756562632.jpg
 
Back
Top Bottom