Behaviourist
JF-Expert Member
- Apr 8, 2016
- 39,901
- 95,401
Lazima nyee ndoo1. Salome anamiliki gari lenye namba T......DFP?
2. Kwahiyo baada ya kufika nyumbani kwa Salome wakaamua kukamata kila aliyekuwepo humo ndani ya nyumba? Ni lazima kwani hao watu wanahusika kweli sababu tu walikuwa nyumbani kwa Salome?
After all this government will be walking a tight rope throughout the next five years with the fake mandate it has grabbed.
Sishangai huu utakuwa wakati mgumu sana kwa wote wanaopinga malaika na mashetani wake... wapinzani watazushiwa kila aina ya kesi ili wapotezwe kama si kuangamizwa wao na familia zao...Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga linafanya uchunguzi kuhusiana na tukio la jaribio la kuchoma moto nyumba ya Mbunge Mteule wa Jimbo la Shinyanga Mjini Patrobas Katambi (CCM) iliyopo mtaa wa Ushirika Mjini Shinyanga huku likiwatafuta na kuwakamata Aliyekuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA Salome Makamba na mdogo wake Timoth Makamba wakihusishwa na tukio hilo.
Akitoa Taarifa kwa Vyombo vya Habari leo Oktoba 30,2020 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya saa sita na dakika 45.
“Majira ya saa saba kasorobo, Mbunge Mteule Patrobas Katambi akiwa amelala nyumbani na ndugu zake walisikia kishindo juu ya paa la choo cha nje ambacho kipo katika eneo la uzio wa nyumba hiyo ndipo walipotoka nje na kuona moto ukiwaka juu ya paa la choo pamoja na dumu lenye mafuta aina ya petroli”,ameeleza Kamanda Magiligimba.
“Wakati wakiendelea kuzima moto huo waliona gari aina ya Toyota Klugger lenye rangi ya silver likikimbiliwa na watu wawili na kisha watu wale waliingia ndani ya gari lile na kutoweka”,amesema Kamanda Magiligimba.
Kamanda Magiligimba amesema baada ya kufanikiwa kuzima moto huo waliona gari lile lile likipita barabara ya lami ya Shinyanga – Mwanza ndipo walipoamua kulifuatilia na dereva wa gari hilo baada ya kugundua anafuatiliwa aliamua kuingia hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga na kuliacha gari hilo kisha kukimbia.
“Wakati wa kuwaweka chini ya ulinzi watu hao ilitokea purukushani ndani ya uzio wa hospitali na gari ya polisi iliyokuwa doria ilifika mapema na kufanikiwa kuwakamata watu wawili ambao ni Wilson Mhando Suluti (30) mkazi wa Bugweto na Jackson Raphael Peter (27) mkazi wa Bugweto wakiwa ndani gari hilo lenye namba za usajili T.729 DFP aina ya Toyota Klugger rangi ya Silver mali ya Salome Makamba aliyekuwa mgombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA”,amefafanua Kamanda Magiligimba.
“Ilibainika kuwa watu hao tuliowakamata wao ndiyo waliokuwa kwenye eneo la tukio kulingana na mavazi waliyovaa. Baada ya mahojiano, watu hao walikiri kuwa gari hilo ni la Salome Makamba na dereva aliyetoroka ni Timoth Makamba ambaye ni mdogo wake Salome Makamba”,ameongeza Kamanda Magiligimba.
Amesema polisi walifika nyumbani kwa Salome Makamba na kufanya upekuzi kisha kuwakamata watu wengine wawili ambao ni Justine Owesiga (35) Mkazi wa Ndala Shinyanga na Gibson Mkongwa (31) mkazi wa Iringa waliokutwa kwenye nyumba hiyo.
“Juhudi za kuwatafuta na kuwakamata Salome Makamba na Timoth Makamba ambaye ndiye dereva wa gari hilo lililotelekezwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga zinaendelea. Gari husika linashikiliwa na watuhumiwa hao wanne na watafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika”,amesema.
Amesema Salome Makamba aliachiwa jana kwa dhamana baada ya kushikiliwa na jeshi la polisi Oktoba 28,2020 kwa tuhuma za kumshambulia msimamizi wa uchaguzi kituo cha kupigia kura cha Bugweto B, Farida John na kumuumiza ambapo aliomba aone matokeo na baada ya kutoridhika nayo aliyachana na kuanza kumshambulia msimamizi huyo wa uchaguzi akiwa na wafuasi wake.
“Natoa wito kwa wanasiasa na wafuasi wao kuacha mihemko ya kisiasa inayopelekea uvunjifu wa amani badala yake wafuate sheria,kanuni na taratibu z auchaguzi na Jeshi la polisi halitasita kamwe kuchukua hatua kali za kisheria kwa mtu au watu au kikundi chochote chenye nia ya kuvuruga amani nchini”,amesema Kamanda Magiligimba.
Malunde
Hii ndyo mbinu kubwa iliyobaki Kama waliopokwa haki wakaamua kureact "maana To every action there's an equal and opposite reaction "hii reaction itashangaza wengi..natabiri kama waliopokwa Waka revenge basi gvn itafeli !!Tuombe Mungu tu.....watu wanahasira sana mtaani!!Serikali ijiandae kuwapa mabodi gadi wabunge wote wa aina hii ..watafanyiwa vitimbi sana ....lakini tunaenda kutengeneza vikundi vya kihalifu na kiasi ...kwakua kutakua na watu wengi ambao watajiona kuwa sauti zao haziwezi tena kusikilizwa....hakuna kitu kizuri kama kuwa na mfumo mzuri wa uwakilishi na upinzani katika bunge unasaidia sana nchi kiusalama ......watu ambao wangeweza kutafuta kusikilizwa kwa kufanya ualifu au kujiunga na vikundi vibaya watakuwa hawana haja ya kufanya hivyo kwakua hata kama hawakukubali wanaweza kupeleka hisia zao kwa vyama vingine na ushauri ukaifikia serikali
Pretending you did not see all the irregulaties, simply because you voted for them!, stop your nonsense.Do you have any evidence in support of your “fake mandate” claim?
While you’re entitled to your own opinion, you aren’t entitled to your own facts. I voted for them and the results reflect my will. If you didn’t vote for them, that’s fine. Ultimately, the voice of the majority must be respected!
Pretending you did not see all the irregulaties, simply because you voted for them!, stop your nonsense.
Talking about the voice of the majority?! don't think if you know what you are talking about, fake ballot papers with the names of CCM candidates already ticked where "the voice of the majority"
Sijawahi kusoma kesi yoyote ya arson na arsonist akawa reckless kiasi hata aanze kuchoma choo.
Tena cha nje.
Wapi nimesema nimeshangaa?Unashangaa nini? Are you assuming that they’re experienced arsonists?
Mtu ambaye hajawahi kuua akijaribu kuua anaweza akaishia kujeruhi na kuondoka akiamini kwamba ameshaua!
Wow! here comes another problem from you. You believe Chadema supporters were the one who burnt their own offices, simply bcoz you heard from the police! the same police who support CCM in each and everything they do, who helped you guys to store fake votes in their stations!There isn’t a shred of evidence! You know, it’s a fact that an election fraud is a crime punishable by law. If you actually caught anyone, do the right thing! Otherwise, let’s not dwell on such propaganda.
If followers of Chama Cha Demokrasia ya Matusi (Chadema) can cunningly burn down their own party office and blame the incident on CCM followers, there is no reason to believe that they cannot cunningly create fake ballot papers and blame that incident on CCM!
Wapi nimesema nimeshangaa?
Wow! here comes another problem from you. You believe Chadema supporters were the one who burnt their own offices, simply bcoz you heard from the police! the same police who support CCM in each and everything they do, who helped you guys to store fake votes in their stations!
Refer what Hai OCD said to Mbowe days before the election were conducted, the same police who hold CCM ID's in their wallets, hence when they retire they are given different post from the president, wake up man.