darcity
JF-Expert Member
- Jul 20, 2009
- 8,719
- 16,932
Ni kweli nilimaanisha hivyo...nashukuru na nimefurahi kuona mchango wako Jamii Forum ingawa umeadimika.Ulitaka asiipende dini? Wewe huna dini?
darcity nadhani ulitaka kuandika "umetelekezwa".
Kuhusu majengo ya kizamani, ni vyema wakayaacha lakini wawe wanayakarabati, ndio historia yenyewe hiyo.
Naona wenyewe wanyeji wa Pangani wamezubaa, mashamba ya nazi wanayauza badala ya kuuza nazi, na fukwe zao zote wanauwauzia wageni. Pesa wanaolea wake na kulia pilau.
Mwisho itakuwa kama Unguja, mpaka sasa nadhani 80% ya fukwe zake inamilikiwa na Wataliano,(nahi ni Vatikano au mawakala wake). Kama si wao vile, wanashambulia kimkakati.
Si Pangani tu, tufunge vibwebwe, pwani yote ya Afrika Mashariki, kwenye chimbuko la Uislam, tunaipoteza kwa Wataliano, kidogo kidogo. Historia njema ya Waislam inafutwa.
Nilikuwa huko kikazi miaka kadhaa nyuma. Unachosema ni kweli fukwe nyingi zimeuzwa na zao la nazi linaporomoka wakati mahitaji ni
mengi.