Nyumba 52 za Watumishi Zimejengwa Mwaka Huu wa Fedha

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,862
930

MHE. GODWIN MOLLEL - NYUMBA 52 ZA WATUMISHI ZIMEJENGWA MWAKA HUU WA FEDHA

Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia Wizara ya Afya imejenga nyumba za Watumishi 52 zenye thamani ya Tsh. Bilioni 3.417 katika Hospitali za Rufaa za Mikoa na Hospital za Kanda ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuboresha utoaji huduma kwa Wananchi.

Dkt. Mollel amesema hayo leo Aprili 25 Bungeni Jijini Dodoma, wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Dkt. Ritta Enespher Kabati katika Mkutano wa kumi na moja.

Amesema “Katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imejenga nyumba 52 za Watumishi zenye thamani ya Tsh. 3,417,556,981 katika Hospitali za Kanda na Hospitali za Rufaa za Mikoa ikiwemo nyumba moja katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa”

Amesema Serikali itaendelea kujenga nyumba kwa ajili ya Watumishi ili kuwapunguzia changamoto, jambo linaloongeza hamasa katika utendaji wao na kuboresha utoaji huduma kwa Wananchi.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.18.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.18.jpeg
    61.7 KB · Views: 7
  • WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.17(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.17(1).jpeg
    25.6 KB · Views: 8
  • WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.17.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-25 at 17.17.17.jpeg
    16.7 KB · Views: 7
  • WhatsApp Image 2023-04-25 at 15.55.27.jpeg
    WhatsApp Image 2023-04-25 at 15.55.27.jpeg
    33.8 KB · Views: 6
Back
Top Bottom