Kasheshe
JF-Expert Member
- Jun 29, 2007
- 4,694
- 787
Bado kuna utata katika hili swala la nyumba. Wangetwambia ni nyumba ngapi za serikali na mashirika ya umma zilizouzwa ili tujue kama hizo zilirudishwa serikalini ni asilimia ngapi ya nyumba zilizouzwa.
Kuna uwezekano kabisa hizo 128 zilizorudishwa ni aslimia ndogo sana ya nyumba zilizouzwa. Mkapa inasemekana alinunua nyumba tatu je naye karudisha? Magufuli naye aliyevalia njuga swala la kuuza nyumba karudisha ngapi? Majina yaliyowekwa hadharani ni machache mno ukilinganisha na nyumba zilizorudishwa.
Jibu ni kweli ni asilimia ndogo, lakini hiyo ndiyo ya asilimia ya nyumba zilizouzwa kinyume na taratibu walizojiwekea...
Ikumbukwe kwamba uamuzi wa kuuza nyumba za serikali hauja-be-nullified... kilichokuwa kinapingwa ni kuuza kinyume cha utaratibu huo ulikuwa umepitishwa na baraza la mawaziri la wakati huo..
Ukisoma kwa makini kidogo, utaona kwenye post yangu yenye quote ya habari leo... ina kisehemu hiki...
Takwimu zilizowasilishwa na Waziri Kawambwa kwa Bunge zinaonyesha kuwa hadi Juni mwaka huu serikali ilikuwa imeuza nyumba 7,159 na ilikuwa imepata Sh bilioni 38.6 kutokana na mauzo hayo kati ya lengo la Sh bilioni 57.
Si vyema tukurupuka kuandika tu bila kusoma post za nyuma