Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

Good job
*NYUMA YAKO – 12*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Mikono yao ya kulia niliiona ikiwa imezama kotini. Bila shaka kushikilia bunduki.
Hapa ikanilazimu nifanye maamuzi ya upesi kuokoa roho yangu.
ENDELEA
Ni upesi nikanyanyuka nikiwa nimebebelea ile ndoo ya taka, nikawatupia! Wakiwa wamedaka na kudondoka nayo chini, nikawawahi nisiwape muda wa kujiandaa. Mmoja nikampoka bunduki na kisha nikamdaka na kumwekea tundu la bunduki kichwani nikimwamuru mwingine aweke silaha yake chini.
“Fanya upesi kabla sijammwaga mwenzio ubongo!”
Huyu niliyekuwa nimemdaka alikuwa ni yule mwanaume niliyekuwa naye kwenye basi. Mwenzake, mwanaume mrefu mwenye mwili mpana, akan’tazama kwa mashaka kama mtu ajiulizaye nini cha kufanya.
“Nimesema weka silaha chini!” Nikamwamuru. “sitasema tena sasa hivi, utaokota maiti ya mwenzako!”
Basi akainama na kuweka silaha yake chini akiwa anan’tazama kwa kukodoa.
“Ninyi ni wakina nani?” nikauliza. “Kwanini mnanifuata?”
Kimya. Hamna aliyenijibu. Nikarudia tena kuwauliza mara hii nikikaza sauti zaidi, lakini haikuleta tofauti! Hakuna aliyenijibu.
“Sina muda wa kupoteza na ninyi! Kama hamtanipa majibu ya maswali yangu basi nitawamaliza maana haitakuwa hasara kwangu.”
Nilipomaliza tu hiyo kauli, bwana yule niliyekuwa nimemkaba, akawahi kuudaka mkono wangu wenye silaha, akajigeuza upesi akitaka kufanya shambulio kwa ngumi ila kwa upesi nikamkwepa, na nilipoona yule mwenzake ametwaa bunduki aliyoiweka chini, nikafanya jitihada za haraka za kumdaka mwanaume yule mwenye mustachi na kisha nikajikinga naye.
Hapo mwenzake akapata kigugumizi cha kufyatua bunduki, nikamtupia risasi mbili na kumlaza chini hajiwezi. Kisha mwanaume yule niliyemkaba nikamziraisha na kumweka begani. Ikanipasa niondoke mapema eneo hilo kwani milio ya bunduki ingewafanya vyombo vya usalama kujongea hapo muda si mrefu.

**

Saa moja usiku …

Baada ya kutoka kuoga, nilijifuta maji na kisha kumjongea mateka wangu ambaye nilikuwa nimemfungia kitini. Alikuwa bado hajarudi fahamuni hivyo nikamwagia maji na kumtaka ajibu maswali yangu kama salama ya roho yake.
Lakini mwanaume huyo hakuogopa kabisa. Akiwa anan’tazama usoni, akaniambia hatajibu swali langu hata moja. Na nikitaka nimuue pasipo kujichosha. Hapo ikabidi nitafute namna ya kumfanya aongee.
Nikamnyanyua na kumpeleka bafuni. Nikamvika mfuko wa kitambaa kichwa kizima na kuanza kumwagia maji usoni mwake kumnyima pumzi. Akahangaika sana. Lakini kila nilipouvua mfuko huo na kumuuliza, bado hakuwa tayari!
Nikamtesa sana mpaka mwishowe akawa amepoteza nguvu kabisa. Macho yalilegea na mdomo akaacha wazi akitapika maji, ila bado hakuwa amenipa majibu ya maswali yangu. Bado alikuwa na roho ngumu!
Basi nikaona nimpe mapumziko alafu tutaendelea tena muda utakaporuhusu, kwa muda huo nikawasiliana na Daniele na kumwambia yaliyotukia. Naye akaniambia hatua aliyofikia pamoja na timu yake. Siku hiyo alikuwa ameonana na Makamu wa Raisi na pia mke wa Raisi. Wote alifanikiwa kuwafanyia mahojiano lakini hakuna kikubwa alichoking’amua, zaidi mke wa Raisi alikuwa anaumwa na anatazamia kwenda kwao, Australia, kwa ajili ya mapumziko.
Na zaidi ya yote, alipata taarifa kuwa O’Neil, yule bwana aliyetupatia kiasi kidogo cha taarifa, amekutwa akiwa amekufa huko Massachusetts! Mwili wake umekutwa ukiwa mtupu na ishara ya kupitia mateso.
Habari hiyo ikanishtua kwa namna yake. Nani atakuwa amemuua O’Neil? Na je kifo chake kitakuwa na mahusiano na taarifa zile alizotupatia?
Nikamtaka Daniele afuatilie kwa undani juu ya kifo hicho kwani kitakuwa nacho kina mlango wa kutupeleka tunapopahitaji. Basi hata nilipokata simu, nikaendelea kuwaza juu ya kifo cha O’neil. Si bure mzee yule hakuwa anataka kujihusisha na haya mambo!
Lakini kifo hiko kikanipa maswali sana juu ya wauaji. Je pia watakuwa wanajua kuhusu mimi na taarifa zile za bwana O’neil?
Mara mlango ukagongwa na kuniamsha toka kwenye lindi la mawazo. Nikanyanyuka toka kitandani na kwenda mlangoni kumkuta mhudumu. Mwanamke mrembo mwenye mashavu mekundu. Aliniambia kuhusu chakula, kipo tayari kwenye hall, lakini kabla hajaenda, bwana yule niliyekuwa nimemfungia bafuni, akaanza kupiga kelele akigugumia!
Mhudumu akan’tazama kwa hofu, nami kumpoza nikamwambia huyo ni mwenzangu yu hoi anaumwa. Lakini ni wazi maneno hayo hayakumkosha mhudumu, akaenda zake akiwa na sura ya mashaka, na hata mwendo wake ukiwa wa kasi!
Muda kidogo, kama dakika mbili, mlango ukagongwa kwanguvu. Kabla sijauendea nikauliza, “Nani?” sauti ya kiume ikanijibu, “Staff!”
Taratibu nikasonga na kuchungulia nje kwa kupitia tundu mlangoni. Huko nikaona majibaba mawili wakiwa wamevalia sare za hoteli. Walikuwa ni walinzi. Hapa nikapata kujua kuwa mhudumu yule alienda kutoa taarifa juu ya sauti ile alosikia chumbani mwangu.
Nikaufungua mlango, na pasipo kuonyesha lolote usoni mwangu, nikawauliza, “naweza kuwasaidia?”
“Tumekuja kufanya ukaguzi chumbani mwako!” mmoja akajibu akinitazama machoni.
“Mtakaguaje chumba cha mteja?” nikawauliza nikiwakunjia ndita.
“Ndugu, ni jukumu letu kuhakikisha kuna usalama ndani ya hoteli. Kama unaona ni shida, basi tuwaite polisi watekeleze hilo!” akasema yule bwana aliyejielezea hapo awali. Kidogo nikafikiria na kuona ni kheri nikawaruhusu watu hao waingie ndani na kufanya ukaguzi kuliko ujio wa polisi hapo.
Basi, kama watu wanaofahamu kinachoendelea, wakanyookea bafuni, huko wakamkuta bwana yule niliyemfungia. Wakamfungua kamba toka kwenye kiti na kumweka huru. Kisha mimi wakaniweka chini ya ulinzi wakinituhumu kama mtekaji!
“Upo sawa?” Mmoja akamuuliza yule bwana waliyemwacha huru. Naye kwa uchovu akawajibu, “nipo sawa, nashukuru.”
Wakamuuliza kwanini mimi nilimfungia kule bafuni, naye akatoa maelezo ya wongo kuwa nilitaka kumuua kisa nikitaka pesa toka kwake, basi walinzi wakapiga simu polisi kutoa taarifa juu yangu.
“Huyo anawaongopea,” nikapaza sauti. “ni yeye ndiye anataka kuniua. Yeye pamoja na mwenziwe!”
Lakini nani aniamini? Mazingira yalikuwa yananisaliti na kuninyooshea kidole kuwa mimi ni muuaji. Basi tukiwa hapo, ndani ya muda mfupi tu, yule jamaa, jambazi, kwa upesi akawadhibiti walinzi wa hoteli na kuwaweka chini ya ulinzi. Alitumia bunduki niliyompokonya. Bunduki hiyo nilikuwa nimeiweka kwenye droo ya kitanda.
Alipofanikisha hilo, akaninyooshea tundu la risasi na kuniamuru niseme kile kilichonileta Ujerumani. Tena niseme upesi kabla hajanimaliza aende zake.
Nikamwambia huku nikinyoosha mkono juu, “mimi ni mtalii tu! Sitambui kwanini wanifuatilia namna hii!”
“Usinifanye mimi ni mjinga! Natambua kinachoendelea na kama uki—” hakumalizia, nikawa nimemtupia stuli iliyokuwa imesimama kando yangu. Stuli hiyo kwakuwa niliitupa kwanguvu, ikafyeka miguu yake na kumwangusha chini! Kabla hajaamka, walinzi wakamuwahi kumpokonya silaha, ila ajabu akafurukuta kwanguvu na kumtupa mlinzi mmoja kando kwa kumkandika teke zito. Na huyo mwingine akamchapa kiwiko na kisha ngumi nzito, akalala kando amezirai.
Kabla hajateka tena bunduki, nikajitupa na kuunyoosha mguu wangu kuisogezea mbali kwa teke, alafu nikaunyanyua kutaka kumkandika kifuani. Akakwepa. Akajirushia mgongo kunifuata. Akatupa ngumi yake, nikaiyeya, ya pili nikaidaka na kuiviringita! Akajizungusha na kutupa kiwiko, nacho nikakisogezea pembeni na alafu kumdaka shingo yake na kumkaba kwanguvu zangu zote.
Akatapatapa akituma viwiko vyake. Havikunipata. Ila kimoja kilitifua mbavu yangu na kunipa maumivu makali. Nikavumilia na kuendelea kumkaba. Akatupa tena kingine, hakikunipata, cha tatu kikanitifua tena. Hapo nikashindwa kuvumilia!
Bwana huyu akajichomoa toka kwenye mikono yangu na kisha akaniadhibu kwa ngumi ya shavu la kulia. Mdomo ukalowana damu. Lakini sikumruhusu achukue bunduki. Alipotaka kufanya hivyo, nikamuwahi kumvuta. Akatupa teke, nalo nikamdaka na kumvuta kwanguvu, alafu nikamrukia mgongoni na kumkaba tena. Mara hii mikono yake niliikandamizia na magoti yangu, hakuweza kufurukuta!
Akapoteza kabisa nguvu. Macho yakaanza kuelekea juu. Nikalegeza mikono yangu na kumuuliza ametumwa na nani. Kwa mbali nikamsikia akisema, “Rodolfo!” kisha akazirai!

***
 
*NYUMA YAKO – 13*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Akapoteza kabisa nguvu. Macho yakaanza kuelekea juu. Nikalegeza mikono yangu na kumuuliza ametumwa na nani. Kwa mbali nikamsikia akisema, “Rodolfo!” kisha akazirai!
ENDELEA
Basi nami sikukaa tena hapo kwakuwa polisi walikuwa njiani na mimi sikutaka kusumbuana nao. Nikawaaga wale walinzi, na kwasababu walishaona ya kuwa sina tatizo, wakaniacha nikaenda zangu. Kutoka tu ndani ya hoteli, nao polisi wakafika hapo wakitumia gari dogo. Upesi wakazama ndani.
Nikasimama hapo kutazama, punde nikaona wakitoka wakiwa wamemshikilia yula jamaa. Wakamzamisha ndani ya gari lao na kutimka. Nikashusha pumzi ndefu na kuendelea na safari yangu.
Nikajongea kwa umbali mdogo kabla sijasimamisha taksi inipeleke hoteli nyingine. Huko nikachukua chumba namba 289, na kujipumzikia kitandani nikitafakari yale yaliyotoka kujiri.
Rodolfo ni nani? Nilijiuliza hilo swali. Atakuwa ni mtu wa aina gani huyo na kwanini ametuma watu kunifuata? Hapa nikajikuta nikiamini kuwa Rodolfo atakuwa anahusika na MUNICH 2345. Hata hivyo anaweza akawa anahusika na kupotea kwa Raisi!
Nikajigeuzia upande wa kushoto nikiendelea kutafakari namna ambavyo matukio haya yalivyosukwa. Huku O’neil anauwawa kwa kuteswa huko Marekani, nami navamiwa na kutishiwa uhai! Hakika hapa palikuwa pana fumbo.
Mara simu ikaita, nikainyakua na kuiweka sikioni. Alikuwa ni Jack Pyong!
“Hey Jack, vipi?”
“Hali si nzuri, Tony!” sauti ya Jack ikaongea kwa kutetemea. Tangu nimjue Jack sikuwahi kumsikia akiongea katika namna ile. Nilihisi sauti yake imetepeta woga ndani yake.
“Kuna nini, Jack?” nikauliza nikiwa najitengeneza kitandani. Niliketi kitako na kukunja sura kulazimisha umakini.
“Sijui nini kinaendelea, Tony. Leo nimenusurika kupigwa risasi na mtu nisiyemfahamu!”
“Serious?”
“Ndio. Hapa nahofia hata kwenda nje!”
“Umetoa taarifa kazini?”
“Hapana, sijatoa. Nahofia, Tony. Nahofia kumhusu Violette!”
“Sikia, basi fanya hivi, toa taarifa makao, alafu utanambia nini watafanya!”
Simu ikakata. Hapana, nikaipiga upesi na kuibandika sikioni.
“Tony, umenielewa?”
Akacheka. “We fala umeamini nilichokuambia?” Nikanyamaza kwa hasira. Nikang’ata meno yangu nikinguruma. “Jack, unajua mambo mengine usiyaletee masikhara!”
“Wewe ukiyafanya sio masikhara sio?” akajibu kwa kebehi. Nikasonya na kumuuliza,
“Sema umenipigia nini?”
“Nataka nikupe marejesho ya kazi yako! Ile ya MUNICH 2345.”
“Enhe ni nini umepata?”
“Vitu vingi tu. Nashindwa kujua nishike lipi niache lipi!”
“We niambie vyote, nami nitajua cha kufanya…”
Basi akapendekeza kunambia kimtiririko maana moja laweza pelekea jingine, nami nikatumia akili yangu kukitunza alichoniambia na hata nikapanga kesho yake asubuhi na mapema, kwenda kuitafuta nyumba nambari 2345 ndani ya jiji hili la Munich.
Mengine utayafahamu baadae… huna haja ya kupapatika, mambo bado ni mengi mbeleni.

**

Saa tano asubuhi …

Nilifunga mlango wa taksi baada ya kukamilisha malipo yangu. Nikatengenezea koti langu mwilini na kutazama mtaa ambao nilikuwa nimeshushwa. Hapo kulikuwa na nyumba kadhaa zikiwa zimesimama kwa kufuatisha barabara hii ya lami.
Na kama nilivyokuwa nimemuelekeza dereva taksi, alikuwa amenishusha mbele ya nyumba ninayotakiwa kushukia. Nyumba yenye anwani 2345!
Nikaitazama nyumba hii kabla ya kuijongea. Ilikuwa ni nyumba tulivu isiyo na dalili ya makazi. Madirisha yake yalikuwa yamejaladiwa na vioo yakiwa hayana mapazia.
Nikanyanyua miguu mpaka mlangoni, nikagonga mlango na kutulia nikiskizia. Hamna kitu. Nikagonga tena na tena, hamna kitu! Sasa nikaanzaa kuamini kuwa humo ndani hamna watu. Nikachungulia dirishani kwa ufupi alafu nikaujaribisha kuusukuma mlango. Haukufunguka.
Nikausukuma kwa nguvu kidogo, ukatenguka na kufunguka! Taratibu nikausogeza na kuzama ndani. Nikarusha macho yangu huku na kule kwa tahadhari huku mkono wangu wa kuume ukiwa karibu na nyonga ya mguu, kwa tahadhari ya kuchoropoa silaha.
Ndani ya nyumba hii kulikuwa na samani za zamani, buibui na vumbi. Ni nyumba iliyotelekezwa, tena si karibuni. Niliingia mpaka chumbani na hata jikoni nisikute alama yoyote ya uhai au uwepo wa binadamu. Nikiwa nimerejea hapo sebuleni, kwa chini mbali ukutani, nikaona vipandevipande vya vyupa.
Nikavisogelea na kuokota kipande mojawapo na kukitazama. Kilikuwa ni kipande cha picha. Nikajaribu kuonganisha vipande kadhaa vya vyupa hivyo, nikapata kuona picha ya mwanamke mwenye nywele nyeusi na macho yalopoa.
Lakini sura yake sikuweza kuiona vema kama nilivyotaka. Vipande vingine vya chupa vilikuwa vimesagika vibaya hivyo kupoteza kabisa maana zake. Na nilipotazama vema, nikabaini kuwa katika picha hiyo, huyo mwanamke alikuwa ameketi na mtoto.
Sasa ni kheri ya picha ya huyo mwanamke, ya mtoto ndiyo ilikuwa haionekani kabisa, nyang’anyang’a! Nisingeweza kutambua lolote lile isipokuwa rangi ya nywele zake. Rangi ya dhahabu.
Basi nikapiga picha kadhaa kwa kutumia simu yangu alafu nikazama ndani kule chumbani kwa nia sasa ya kukagua makabati nione ni nini nitapata. Nikaona nguo za mtoto waa kiume, na za mwanamke. Lakini zaidi nikaona kifaa cha kusaidia kupumua kwa watu wanaosumbuliwa na tatizo la pumu!
Hapa sasa nikapata kukumbuka kuhusu kifaa hicho. Kifaa alichonionyeshea Daniele kuwa wamekiokota uwanja wa ndege wakidhania ni cha Raisi. Ina maana ile ilikuwa ni ishara au?
Nikakiweka kifaa hicho kibindoni, lakini kabla sijaendelea na kazi ya upekuzi, nikasikia gari ikisimama kwa ‘kuchuna’ breki kali huko nje. Haraka nikajongea dirisha na kutazama.
Nikaona wanaume watatu wakiwa wamevalia nguo nyeusi wakishuka toka kwenye Volkswagen modeli ya zamani. Gari hiyo kwa ubavuni ilikuwa na chapa ya samaki na maneno ya kijerumani yakimaanisha kampuni ya uvuvi.
Wanaume hao walikuwa na sura ya kazi, na nikadhani huenda wakaja mule nilipokuwapo, ila lah! Wakanyookea nyumba ya pili na kuzama humo. Sikujua walienda kufanya nini, na sikujua kwanini niliwatilia shaka. Nilihisi tu si watu wema.
Basi nikapiga moyo wangu konde na kuendelea kusaka. Sikupata cha maana, baada ya kama dakika kumi, nikaona nitoke humo ndani niende zangu nikiwa nimelenga kutafuta serikali ndogo ya eneo hilo ili nipate walau taarifa juu ya wakazi wa hapa.
Nilipotoka nikatazama ile nyumba jirani ambayo iliwameza wale watu niliokuwa nawatilia mashaka. Sikuona jambo. Muda si mrefu,, kwa mwendo wangu wa haraka, nikawa nimefika kituoni ambapo nilipanda gari nikilenga kuelekea kwenye ofisi ndogo za wilaya. Ikanichukua kama dakika kumi tu kufika hapo. Nikazama ndani na kueleza shida yangu.
Nilijitambulisha kama James Tuck toka Marekani na nimefika hapo kumuulizia ndugu yangu ambaye anakaa Munich kwani nimefika kwake sikumkuta.
Mhudumu akaniuliza kuhusu anwani yake, nikamtajia. Muda si mrefu akanielekeza mahali pa kwenda, yaani kama balozi wa mtaa, huko nitapata majibu kamili na ya uhakika.
Kwahiyo nikajiresha tena kituoni na ndani ya muda mfupi nikawa nimefika nilipoelekezwa. Nikamkuta mzee mmoja mnene mfupi akiwa anakunywa bia aliyoitunza kwenye glasi kubwa. Nikamsalimu na kumweleza shida yangu. Akaniambia ya kuwa mwanamke huyo aliyekuwa anakaa kwenye yale makazi alipotea na hakuna mtu anayejua wapi alipo hata sasa.
“Ni kama miezi mitano sasa. Taarifa pekee tuliyonayo ni kwamba jirani yake aliona gari aina ya van ikimpakia na kwenda naye, yeye pamoja na mtoto. Hakumuaga mtu yeyote, hivyo hamna anayefahamu.”
“Vipi kuhusu namba ya usajili ya van hiyo?” nikauliza.
“Hamna mtu aliyeijali,” akanijibu huyo mzee. “Nani atasumbuka na kunakili namba za magari na ingali haikuonekana kama ni tukio la shuruti?”
“Na vipi kuhusu huyo jirani? Yupo?”
Mzee akatikisa kichwa na kunambia, “naye hayupo!”
“Amehama?”
“Hakutoa taarifa kama anahama. Sijui alipoelekea.”
Nilipompeleleza zaidi nikagundua kuwa huyo jirani anayemwongelea alikuwa anakaa kwenye ile nyumba ambayo niliwaona watu wakiingia humo. Nikamuuliza, “Ina maana hapo pana wakazi wapya?”
“Ndio, kuna wanaume wa kiwanda cha mbao hapo,” akanijibu kishaa akagida fundo la bia. Lakini …
Wale wanaume mbona hawakuonekana kama wafanyakazi wa kiwanda cha mbao? Nilijikuta nikitia shaka. Mbona gari yao ilikuwa na chapa ya samaki kama ni hivyo?

**
 
*NYUMA YAKO – 14*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
“Ndio, kuna wanaume wa kiwanda cha mbao hapo,” akanijibu kishaa akagida fundo la bia. Lakini …
Wale wanaume mbona hawakuonekana kama wafanyakazi wa kiwanda cha mbao? Nilijikuta nikitia shaka. Mbona gari yao ilikuwa na chapa ya samaki kama ni hivyo?
ENDELEA
Maswali hayo yalibaki kichwani hata wakati natoka kwenye jengo hilo. Nilikuwa nawaza na nikaona endapo nikiendeleza mawazo hayo basi naweza jikuta nagongwa na gari barabarani.
Nikatembea zangu mpaka kituoni na kukwea basi. Kama nipendavyo nikaenda kukaa nyuma, kichwa nikakiegeshea kitini na huku macho yangu yakiwa yanatazama mji. Namna vitu viendavyo nyuma wakati sisi tukienda mbele.
Wakati huo pia nikiwa nawaza kumwambia Jack Pyong juu ya yale niliyoyakuta kule kwenye nyumba yenye anwani elekezi ili anambie kama kuna kingine cha kufanya baada ya hapo kama vile alivyoniahidi hapo awali.
Nikiwa katika ombwe hilo, basi likasimama na kunifanya nizingatie. Kwa macho yangu ya kipelelezi nikayarusha kutazama nani anashuka kana kwamba namjua mtu huyo, kabla sijatoa huko macho nikaona wanaume wawili wakiwa wanapanda basi. Wanaume hawa walinifanya niwatazame zaidi kwa namna walivyovaa na hata mwonekano wao maana nilihisi walikuwa wakifanania na wale niliowaona kwenye ile nyumba ya pembeni na 2345!
Wakati nikiwatazama, mmoja wao akanitazama pia tukakutana macho kwa macho! Tukatazamana kwa kama sekunde tatu kabla hajageuza uso wake kutazama kando. Mimi nikaendelea kumtazama zaidi na zaidi, na hata yeye alilitambua hilo.
Niliwakagua kwa macho yangu na kujiridhisha kuwa huenda wakawa na silaha ndani ya makoti yao. Basi nikaanza kufikiria namna ya kuwakabili kama ni mimi wananifuatilia …
Tukaenda kwa mwendo wa kama dakika sita, nikasimama na kutoa ishara kuwa nashuka kituo kinachofuata kwa kubinya kamba ya kumshtua dereva.
Hivyo tukasonga kidogo tu, na basi likaanza kupunguza mwendo kuashiria laenda kusimama. Liliposimama, nikanyanyuka na kushuka.
Hapa sio nilipotakiwa kushuka ila niliona panastahili mimi kushukia kwasababu ya uwingi wa watu. Hiyo ni kwasababu za kiusalama.
Nikazama ndani ya watu na kujichanganya lakini kwa wakati huohuo nikiwa natazama kama nyuma yangu nafuatwa. Sikuona watu. Wanaume wale hawakushuka. Nikaendelea kuzamia na kuzamia huko hata mahali ambapo sipajui alimradi kujihakikishia usalama. Nilipoona ni salama sasa, nikatulia kwenye benchi na kutoa simu yangu mfukoni, nikawasiliana na Jack.
“Jack, nimetoka kwenye ile anwani! … sijakuta mtu huko!”
“Kabisa?”
“Ndio. Ni samani za zamani na mabaki ya nguo na picha … na kifaa cha kuhemea!”
“Unaweza kun’tumia hiyo picha?”
“Sidhani kama utaielewa, ilikuwa condensed kwenye kioo, imevunjikavunjika.”
“Haionekani hata kidogo?”
“Kwa mbali, ila ni ya mwanamke tu. Ya mtoto haionekani kabisa!”
“Gosh!” Jack akalaumu. Nikamuuliza,
“Vipi, hamna namna ya pili kama ulivyonieleza?”
“Ipo, ila hiyo ya pili nilikuambia itakuwa confirmed na hiyo ya kwanza. Sikukuambia hivyo, we fala?”
“Sasa nifanyeje?”
Akanielekeza mwonekano wa mtoto, kisha akanisihi nirudi kule kwenye anwani 2345 ili nikahakikishe kama huyo mtoto alikuwa anaishi hapo kwa kutumia taarifa za majirani.
Nikamuuliza, “Jack, huyo mtoto ana nini? Kwanini yeye?”
“Sijui, Tony. Ila fanya nilichokuambia kwa maana hiyo MUNICH 2345 itakuwa ni yeye.” Aliponieleza hayo akasema, “Nipo busy na shemeji yako, baadae!” kisha akakata simu.
“Pumbavu!” nikalaani nikiiweka simu kibindoni, kisha nikatoa kile kifaa cha kuhemea ambacho nilikiokota kule kwenye anwani 2345 na kukitazama kwa umakini.
Nikagundua kifaa hicho kilikuwa kimechorwa katuni kwa kutumia ‘marker pen’ rangi ya bluu. Marker pen inayoelekea inaelekea kufifia sasa.
Mchoro huo wa katuni ulikuwa ni wa mwanaume aloyechorwa kwa mtindo wa njiti na nywele zake zikisimama kama vijiti. Nikawaza atakuwa nani huyo? Huenda akawa ni huyo mtoto ambaye Jack anamwongelea?
Sikuwaza sana juu ya hicho, nikakiweka kile kifaa kibindoni kisha nikatazama kushoto na kulia alafu nikaanza kuchukua tena hatua kutoka jengoni humo.

**
Saa tisa alfajiri …

Ngo! Ngo! Ngo! Ngo!
Punde mlango ukafunguliwa, akatoka mwanamke mzee ambaye alinikagua upesi kwa macho yake ndani ya miwani yenye lenzi kali kisha akaniuliza haja yangu.
Tulikuwa tunatumia lugha ya kijerumani.
“Tafadhali, naomba kuulizia,” nikasema kwa sauti ya upole. Mwanamke huyo akatambua, nadhani kwa lafudhi yangu, kuwa mimi mgeni. Akafungua mlango na kunikaribisha ndani.
Nilipoketi akaniuliza kama ningependelea maji ama bia. Ni tamaduni ya wajerumani kunywa bia. Nikamwambia nahitaji maji na ndani ya muda mfupi mkononi mwangu nikawa nimeshikilia glasi ya maji safi.
Kwa muda huo mdogo niliokuwa nimekaa hapo, niligundua kuwa mzee huyo anaishi mwenyewe. Nyumba ilikuwa pweke japo safi na ipo kwenye mpangilio mzuri.
Akaketi na kuniuliza wapi nilipotokea, nikamlaghai natokea Uingereza, alafu pasipo kupoteza muda nikamuuliza juu ya jirani yake, yule anaekaa kwenye anwani 2345. Hii nyumba ya huyu mzee ilikuwa ni ya tatu toka pale kwenye nyumba namba 2345.
Basi huyo mzee akajaribu kuvuta kumbukumbu, ungeliona hilo kwa macho yake, kisha akanangalia na kunieleza yale anayoyajua kuhusu jirani huyo, yaani mwanamke na mtoto wake.
Kwa mujibu wa maelezo yake nikagundua kuwa mwanamke aliyekuwa anakaa kwenye ile anwani alikuwa anaishi mwenyewe pamoja na mtoto wake wa kiume. Na pia alikuwa mgeni, kutokea Marekani.
“Mara kwa mara nilikuwa namsikia akiongea na mwanae kwa kiingereza safi, ila alikuwa anajua pia na kijerumani!”
Hapa sasa ndiyo nikaanza kujenga picha. Kama wakazi hao walikuwa ni wamarekani kwanini walikuwa wanaishi Ujerumani? Na watakuwa na mahusiano gani na Raisi aliyepotea mpaka kumpatia rafiki yake anwani ya nyumba?
Nikamdadisi huyo mzee juu ya mwonekano wa mtoto huyo aliyekuwa anakaa na huyo mama, akanieleza kuwa mwenye nywele nyekundu na mashavu makubwa na macho ya dhani ya paka.
Kwa maelezo zaidi, nikapata kujiuliza kwanini mtoto yule alichora picha ya njiti kwenye kifaa chake cha kuhemea. Yule hakuwa yeye. Sikujiuliza sana nikaaga niende zangu nikiwa sijayanywa yale maji niliyopewa.
Nilifanya hivyo kwasababu za usalama, huwezi jua anaweza akawa ametia nini. Kila mtu ni wa kumtilia mashaka kwenye ulimwengu wa kiitelijensia.
Nilipotoka , nikarusha macho kwenda kwenye ile nyumba ya kando ambayo nilikuwa nikiitilia mashaka. Ile nyumba ambayo iliwameza wale watu ambao walikuwa wakivalia nguo nyeusi. Hapo sikuona mtu, lakini kabla sijageuza shingo yangu nikamwona mtu dirishani akichungulia.
Mtu huyo upesi alitoka dirishani na kupotea!
“Hawa watu ni wakina nani?” nikajiuliza nikitembea zangu kuelekea kituoni, ila mara hii, tofauti na ya kwanza, nikahisi nafuatiliwa kwa mapema zaidi! Kwa mahesabu yangu ambayo yalikuwa sahihi, kulikuwa na gari linalokuja nyuma yangu, tena kwa kasi!
Basi nikaongeza kasi ya mwendo wangu na alafu ile kona ya kwanza nikaikata na kuanza kukimbia upesi. Na kabla gari hilo linifuatalo halijachomoza, nikawa nimejibana nyuma ya nyumba!
Nikachomoza kichwa changu kwa udogo na kuangaza. Punde lile gari likapita hapo likiwa katika mwendo wa pole. Ilikuwa ni Volkswagen modeli ya zamani. Madirishani niliwaona wanaume wakiwa wanachungulia na kurusha macho yao kutafuta jambo. Nyuso zao hazikuwa za amani.
Vuuuuuuupp! Wakapita! Lakini ikiwa imepita kama sekunde mbili tu, mara nikasikia sauti ikifoka kwa kijerumani, “Unafanya nini hapo!” kutazama alikuwa ni bwana wa kijerumani ambaye amevalia kaptula tu, kifua wazi.
Sauti yake ilikuwa kali sana, na majibu yake niliyaona punde tu maana nilisikia sauti ya gari ikivuma na mara ikaja kutuama mbele ya ile nyumba! Kutazama, nikaona mwanaume akitokea na mkono wa bunduki, akayaftua risasi mfululizo! Nilikwepa kwa kujibana kwenye nyumba. Yule mwenyeji aliyenifokea nikamwona akiwahi haraka kuzama ndani!
Kidogo nikasikia milango ya gari ikifunguliwa, hapo nikaona tena si pa kukaa. Kutazama nyuma yangu, yaani ya nyuma ya nyumba ile, kulikuwa na ukuta wa mbao, haraka nikaufata na kuukwea kama nyani!
Nilipotua upande wa pili, nikaanza kukimbia kuufuata ukuta mwingine wa nyumba niliyozamia. Kidogo, nikasikia watu wengine wakitua, walikuwa ni wanaume wawili ambao wananifukuzia! Wakaanza kurusha risasi kwa fujo! Kwa pupa!

***
 
Mkuu na mm naomba niweke kweny tag list yako
*NYUMA YAKO – 14*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
“Ndio, kuna wanaume wa kiwanda cha mbao hapo,” akanijibu kishaa akagida fundo la bia. Lakini …
Wale wanaume mbona hawakuonekana kama wafanyakazi wa kiwanda cha mbao? Nilijikuta nikitia shaka. Mbona gari yao ilikuwa na chapa ya samaki kama ni hivyo?
ENDELEA
Maswali hayo yalibaki kichwani hata wakati natoka kwenye jengo hilo. Nilikuwa nawaza na nikaona endapo nikiendeleza mawazo hayo basi naweza jikuta nagongwa na gari barabarani.
Nikatembea zangu mpaka kituoni na kukwea basi. Kama nipendavyo nikaenda kukaa nyuma, kichwa nikakiegeshea kitini na huku macho yangu yakiwa yanatazama mji. Namna vitu viendavyo nyuma wakati sisi tukienda mbele.
Wakati huo pia nikiwa nawaza kumwambia Jack Pyong juu ya yale niliyoyakuta kule kwenye nyumba yenye anwani elekezi ili anambie kama kuna kingine cha kufanya baada ya hapo kama vile alivyoniahidi hapo awali.
Nikiwa katika ombwe hilo, basi likasimama na kunifanya nizingatie. Kwa macho yangu ya kipelelezi nikayarusha kutazama nani anashuka kana kwamba namjua mtu huyo, kabla sijatoa huko macho nikaona wanaume wawili wakiwa wanapanda basi. Wanaume hawa walinifanya niwatazame zaidi kwa namna walivyovaa na hata mwonekano wao maana nilihisi walikuwa wakifanania na wale niliowaona kwenye ile nyumba ya pembeni na 2345!
Wakati nikiwatazama, mmoja wao akanitazama pia tukakutana macho kwa macho! Tukatazamana kwa kama sekunde tatu kabla hajageuza uso wake kutazama kando. Mimi nikaendelea kumtazama zaidi na zaidi, na hata yeye alilitambua hilo.
Niliwakagua kwa macho yangu na kujiridhisha kuwa huenda wakawa na silaha ndani ya makoti yao. Basi nikaanza kufikiria namna ya kuwakabili kama ni mimi wananifuatilia …
Tukaenda kwa mwendo wa kama dakika sita, nikasimama na kutoa ishara kuwa nashuka kituo kinachofuata kwa kubinya kamba ya kumshtua dereva.
Hivyo tukasonga kidogo tu, na basi likaanza kupunguza mwendo kuashiria laenda kusimama. Liliposimama, nikanyanyuka na kushuka.
Hapa sio nilipotakiwa kushuka ila niliona panastahili mimi kushukia kwasababu ya uwingi wa watu. Hiyo ni kwasababu za kiusalama.
Nikazama ndani ya watu na kujichanganya lakini kwa wakati huohuo nikiwa natazama kama nyuma yangu nafuatwa. Sikuona watu. Wanaume wale hawakushuka. Nikaendelea kuzamia na kuzamia huko hata mahali ambapo sipajui alimradi kujihakikishia usalama. Nilipoona ni salama sasa, nikatulia kwenye benchi na kutoa simu yangu mfukoni, nikawasiliana na Jack.
“Jack, nimetoka kwenye ile anwani! … sijakuta mtu huko!”
“Kabisa?”
“Ndio. Ni samani za zamani na mabaki ya nguo na picha … na kifaa cha kuhemea!”
“Unaweza kun’tumia hiyo picha?”
“Sidhani kama utaielewa, ilikuwa condensed kwenye kioo, imevunjikavunjika.”
“Haionekani hata kidogo?”
“Kwa mbali, ila ni ya mwanamke tu. Ya mtoto haionekani kabisa!”
“Gosh!” Jack akalaumu. Nikamuuliza,
“Vipi, hamna namna ya pili kama ulivyonieleza?”
“Ipo, ila hiyo ya pili nilikuambia itakuwa confirmed na hiyo ya kwanza. Sikukuambia hivyo, we fala?”
“Sasa nifanyeje?”
Akanielekeza mwonekano wa mtoto, kisha akanisihi nirudi kule kwenye anwani 2345 ili nikahakikishe kama huyo mtoto alikuwa anaishi hapo kwa kutumia taarifa za majirani.
Nikamuuliza, “Jack, huyo mtoto ana nini? Kwanini yeye?”
“Sijui, Tony. Ila fanya nilichokuambia kwa maana hiyo MUNICH 2345 itakuwa ni yeye.” Aliponieleza hayo akasema, “Nipo busy na shemeji yako, baadae!” kisha akakata simu.
“Pumbavu!” nikalaani nikiiweka simu kibindoni, kisha nikatoa kile kifaa cha kuhemea ambacho nilikiokota kule kwenye anwani 2345 na kukitazama kwa umakini.
Nikagundua kifaa hicho kilikuwa kimechorwa katuni kwa kutumia ‘marker pen’ rangi ya bluu. Marker pen inayoelekea inaelekea kufifia sasa.
Mchoro huo wa katuni ulikuwa ni wa mwanaume aloyechorwa kwa mtindo wa njiti na nywele zake zikisimama kama vijiti. Nikawaza atakuwa nani huyo? Huenda akawa ni huyo mtoto ambaye Jack anamwongelea?
Sikuwaza sana juu ya hicho, nikakiweka kile kifaa kibindoni kisha nikatazama kushoto na kulia alafu nikaanza kuchukua tena hatua kutoka jengoni humo.

**
Saa tisa alfajiri …

Ngo! Ngo! Ngo! Ngo!
Punde mlango ukafunguliwa, akatoka mwanamke mzee ambaye alinikagua upesi kwa macho yake ndani ya miwani yenye lenzi kali kisha akaniuliza haja yangu.
Tulikuwa tunatumia lugha ya kijerumani.
“Tafadhali, naomba kuulizia,” nikasema kwa sauti ya upole. Mwanamke huyo akatambua, nadhani kwa lafudhi yangu, kuwa mimi mgeni. Akafungua mlango na kunikaribisha ndani.
Nilipoketi akaniuliza kama ningependelea maji ama bia. Ni tamaduni ya wajerumani kunywa bia. Nikamwambia nahitaji maji na ndani ya muda mfupi mkononi mwangu nikawa nimeshikilia glasi ya maji safi.
Kwa muda huo mdogo niliokuwa nimekaa hapo, niligundua kuwa mzee huyo anaishi mwenyewe. Nyumba ilikuwa pweke japo safi na ipo kwenye mpangilio mzuri.
Akaketi na kuniuliza wapi nilipotokea, nikamlaghai natokea Uingereza, alafu pasipo kupoteza muda nikamuuliza juu ya jirani yake, yule anaekaa kwenye anwani 2345. Hii nyumba ya huyu mzee ilikuwa ni ya tatu toka pale kwenye nyumba namba 2345.
Basi huyo mzee akajaribu kuvuta kumbukumbu, ungeliona hilo kwa macho yake, kisha akanangalia na kunieleza yale anayoyajua kuhusu jirani huyo, yaani mwanamke na mtoto wake.
Kwa mujibu wa maelezo yake nikagundua kuwa mwanamke aliyekuwa anakaa kwenye ile anwani alikuwa anaishi mwenyewe pamoja na mtoto wake wa kiume. Na pia alikuwa mgeni, kutokea Marekani.
“Mara kwa mara nilikuwa namsikia akiongea na mwanae kwa kiingereza safi, ila alikuwa anajua pia na kijerumani!”
Hapa sasa ndiyo nikaanza kujenga picha. Kama wakazi hao walikuwa ni wamarekani kwanini walikuwa wanaishi Ujerumani? Na watakuwa na mahusiano gani na Raisi aliyepotea mpaka kumpatia rafiki yake anwani ya nyumba?
Nikamdadisi huyo mzee juu ya mwonekano wa mtoto huyo aliyekuwa anakaa na huyo mama, akanieleza kuwa mwenye nywele nyekundu na mashavu makubwa na macho ya dhani ya paka.
Kwa maelezo zaidi, nikapata kujiuliza kwanini mtoto yule alichora picha ya njiti kwenye kifaa chake cha kuhemea. Yule hakuwa yeye. Sikujiuliza sana nikaaga niende zangu nikiwa sijayanywa yale maji niliyopewa.
Nilifanya hivyo kwasababu za usalama, huwezi jua anaweza akawa ametia nini. Kila mtu ni wa kumtilia mashaka kwenye ulimwengu wa kiitelijensia.
Nilipotoka , nikarusha macho kwenda kwenye ile nyumba ya kando ambayo nilikuwa nikiitilia mashaka. Ile nyumba ambayo iliwameza wale watu ambao walikuwa wakivalia nguo nyeusi. Hapo sikuona mtu, lakini kabla sijageuza shingo yangu nikamwona mtu dirishani akichungulia.
Mtu huyo upesi alitoka dirishani na kupotea!
“Hawa watu ni wakina nani?” nikajiuliza nikitembea zangu kuelekea kituoni, ila mara hii, tofauti na ya kwanza, nikahisi nafuatiliwa kwa mapema zaidi! Kwa mahesabu yangu ambayo yalikuwa sahihi, kulikuwa na gari linalokuja nyuma yangu, tena kwa kasi!
Basi nikaongeza kasi ya mwendo wangu na alafu ile kona ya kwanza nikaikata na kuanza kukimbia upesi. Na kabla gari hilo linifuatalo halijachomoza, nikawa nimejibana nyuma ya nyumba!
Nikachomoza kichwa changu kwa udogo na kuangaza. Punde lile gari likapita hapo likiwa katika mwendo wa pole. Ilikuwa ni Volkswagen modeli ya zamani. Madirishani niliwaona wanaume wakiwa wanachungulia na kurusha macho yao kutafuta jambo. Nyuso zao hazikuwa za amani.
Vuuuuuuupp! Wakapita! Lakini ikiwa imepita kama sekunde mbili tu, mara nikasikia sauti ikifoka kwa kijerumani, “Unafanya nini hapo!” kutazama alikuwa ni bwana wa kijerumani ambaye amevalia kaptula tu, kifua wazi.
Sauti yake ilikuwa kali sana, na majibu yake niliyaona punde tu maana nilisikia sauti ya gari ikivuma na mara ikaja kutuama mbele ya ile nyumba! Kutazama, nikaona mwanaume akitokea na mkono wa bunduki, akayaftua risasi mfululizo! Nilikwepa kwa kujibana kwenye nyumba. Yule mwenyeji aliyenifokea nikamwona akiwahi haraka kuzama ndani!
Kidogo nikasikia milango ya gari ikifunguliwa, hapo nikaona tena si pa kukaa. Kutazama nyuma yangu, yaani ya nyuma ya nyumba ile, kulikuwa na ukuta wa mbao, haraka nikaufata na kuukwea kama nyani!
Nilipotua upande wa pili, nikaanza kukimbia kuufuata ukuta mwingine wa nyumba niliyozamia. Kidogo, nikasikia watu wengine wakitua, walikuwa ni wanaume wawili ambao wananifukuzia! Wakaanza kurusha risasi kwa fujo! Kwa pupa!

***
 

Similar Discussions

11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom