Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Akatabasamu pasipo kuonyesha meno. Mashavu yake yalituna na macho yake kujifinya.
“Kwasababu ndo’ sehemu ambapo nina mwenyeji!”
“Mwenyeji? Hapa Virginia?”
“Ndio.”
“Wapi huko?”
Kabla hajajibu akaingiza mrija mdomoni mwake na kufyonza juisi.
ENDELEA
Alifyonza akiwa ananitazama, na alipohakikisha hakuna alichobakiza ndani ya glasi, akajisafisha lips zake kwa ulimi kisha akasema, “Nadhani unamjua mtu huyo. Hivyo ni bora kukwambia ni nani kuliko mahali.”
“Ni nani huyo?”
“Jack. Jack Pyong.”
“Serious?”
“Yah! Yeye ndo’ mwenyeji wangu hapa.”
“Kelly, umekuwa ukijuana na Jack kwa muda gani?”
“Kwa muda kidogo …” akatazama saa yake ya mkononi. “Tony, nimekawia. Sipendi kutembea nyakati za usiku. Naomba niende sasa.”
“Usijali, nitakusogeza na gari yangu.”
Hatukukaa tena hapo, tukanyanyuka na kuendea usafiri nilokuja nao, tukajipaki na tukaanza safari ya kumpeleka kwake, huko ambapo amefikia. Tukiwa safarini nikaendeleaa kumdadisi juu yake na Jack Pyong.
“Nilijuana naye kwa muda kidogo. Ni mtu mwenye maneno mengi na mcheshi pia hivyo haikuchukua muda kuunda naye urafiki!”
Kwahiyo basi kwa mujibu wa Kelly, walikutana na Jack Pyong huko kwenye mtandao wa Facebook na kuwa marafiki. Na kwakuwa walikuwa wote ndani ya Hong Kong basi ikawa rahisi kukutana na kutambulishana. Hapa sasa nikafahamu kuwa Jack alikuwa na mengi ya kunifahamisha kuhusu Kelly. Sikutaka kumchosha mwanamke huyu kwa maswali yangu yasiyokuwa na mwisho.
Basi baada ya habari hiyo, sasa ikawa ni kama zamu ya Kelly kuniuliza mimi. Aliniuliza maswali lukuki juu ya kile kinachoendelea ndani ya Marekani, haswa kupotea kwa Raisi. Kabla sijaendelea, acha nikuweke wazi kuwa ingawa Raisi alikuwa kweli amepotea, bado serikali ya Marekani haikuwa imekiri hilo wazi.
Hii ilikuwa ni aibu kubwa kwa taifa kama la Marekani linalosifika kwa intelijensia ya hali ya juu. Ilikuwa ni dhihaka na matusi makubwa kwa taasisi zote za kiintelijensia, ni kivipi Raisi apotee? Hata mtu ukimweleza kuwa Raisi wa Marekani amepotea ni wazi atakuna kichwa chake akijiuliza inawezekanaje?
Hivyo basi, taarifa zisizo rasmi zilikuwa zikisimamia kuwa Raisi anaumwa na yupo chini ya uangalizi. Kitu ambacho kilikuwa kinyume kabisa na ukweli. Ingawa tulifanya hivyo, lakini bado minong’ono ikazagaa na watu wakiwa wananena hata huko mtaani kuwa huenda wanadanganywa. Mbona huyo Raisi anayesemekana kuumwa, haijulikani yupo hospitali gani na nini haswa kinachomsumbua?
Hivyo kwa namna moja ama nyingine sikushtushwa sana na maswali ya Kelly. Nilijitahidi kutoonyesha hisia zozote usoni, nikazidi kumpumbaza kuwa Raisi anaumwa na yupo chini ya uangalizi na uchunguzi, na si zaidi ya hapo. Niliendelea kusimamia kile ambacho tulitaka jamii iamini wakati tukihaha kuutafuta ukweli.
“Ni kweli, Tony?”
“Yah! Ni kweli. Kwanini unnauliza hivyo? Vipi, kuna lolote ulilosikia?”
“Vipi kama Raisi atakuwa amepotea?” akauliza akiwa anatazama kana kwamba mtu anayetoa masimulizi. “Hivi Marekani itafanyaje? Patakalika kweli?”
Nikatabasamu pasipo kumjibu. Punde akanisihi nisimamishe gari. “Nimeshafika!” akanishukuru na kisha akafungua mlango wa gari akiniaga. Nikamtazama aelekeapo. Alipotelea njiani nisijue ameenda wapi. Sikujali sana, nikatimka zangu.

**

‘Kuna kitu umepata?’
‘Hapana. Marshall, nadhani kuna haja ya kwenda Munich!’
Usiku huu wa saa sita nilikuwa nachat na ajenti Daniele. Nikiwa nimejilaza kitandani, yeye pamoja na timu yake walikuwa wakihaha kukusanya kila taarifa wanayoweza kupata juu ya swala hili la upotevu wa Raisi kutokana na data tulizopata toka kwa bwana O’Neil.
Hawakuwa wakilala wala kupumzika, kazi ilikuwa pevui haswa tofauti na kwa upande wangu.
‘Kuna haja ya kwenda Munich. Nadhani tunaweza kupata kitu huko Marshall!’ Daniele aliendelea kupendekeza. Na kwakweli niliona kuna haja hiyo japo bado kile kitendawili cha Munich 2345 hakikuwa kimeteguliwa.
Kidogo nikapata mawazo hapa. Ile namba 2345 ilikuwa inamaanisha nini haswa? Ni mwaka? Masaa? Ama anwani ya nyumba? Njia pekee ya kupata majibu hayo ilikuwa ni kwenda Munich, Ujerumani.
Na basi Daniele akaniambia kuwa, wakati yeye akiwa huku nchini, atahakikisha anaonana na mke wa Raisi na pia Makamu wa Raisi kwa taarifa na mahojiano zaidi. Ilikuwa ni kama vile tumegawiana majukumu. Kuchati kukaishia hapo.
Kabla sijalala nikamtafuta Jack Pyong kwa njia ya ujumbe nikimtaka afanye anachokijua kuhusu MUNICH 2345. Nikakaa kusubiri majibu, kama lisaa hivi, kimya. Nadhani alikuwa amelala au yupo busy na mchumba wake. Mwishowe nami nikalala.
Asubuhi kuamka, majira ya saa kumi na moja, nikakuta ujumbe kwenye simu yangu toka Jack Pyong.
‘Ndo nini hiyo?’ sikumjibu. Nikaona kuna haja ya kuonana naye uso kwa uso nipate kumweleza, pia kumjuza juu ya safari yangu kwenda Munich. Basi nikajiandaa na katika majira ya saa mbili asubuhi nikakutana na Jack faragha. Nikamweleza kile ninachotaka kukijua, akaniahidi atalifanyia kazi. Kwa mara ya kwanza alikuwa ameongea la maana.
Nilipomwambia kuhusu safari ya Munich, nikimshawishi twende wote, hapa akasita. “Nitamwachaje Violette? Unajua ni jana tu nimetoka kumvesha pete!”
“Jack, kumbuka hii kazi ni kubwa. Tunapigania taifa. Tafadhali fikiria mara mbili.” Kisha nikaondoka nikaenda kukutana na Mkuu wa kazi na kumweleza juu ya mipango yangu, kwenda huko Munich. Jioni ya siku hiyo akanihakikishia kwenda huko kila kitu kikiwa tayari.
Ilipofika majira ya saa moja jioni, nikawa nipo ndani ya ndege, United Airlines, nikielekea Munich, Ujerumani. Safari itakayonigharimu takribani masaa kama kumi na dakika thelathini. Nikafika Franz Josef Strauss Airport majira ya asubuhi ya saa mbili, nikajipatia chumba ndani ya MOXY Munich hotel nilipopumzikia kabla ya kuanza harakati zangu.
Nilipitiwa na usingizi nikiwa nangojea ujumbe toka kwa Jack Pyong. Nilikuja kuamka baada ya kusikia hodi mlangoni mwangu ambapo baada ya kusonya, nikajongea mlango na kuufungua. Alikuwa ni mhudumu wa kike akinijia kunieleza juu ya malazi na chakula kisha akaenda zake.
Baada ya hapo nikaoga na kutoka kwenda kutalii mji wa Munich. Kulikuwa na haja ya mimi kulijua jiji hilo kwa namna fulani kwakuwa nilitarajia kulifanyia kazi. Nikatembea mitaa kadhaa, hata kula nikala huko , chakula cha mchana na jioni. Kwenye majira ya saa mbili usiku, nikapanda usafiri wa uma nirudi hotelini.
Sikuona haja ya kupanda taksi kwasababu nilikuwa nataka kujua zaidi kuhusu jiji hilo.
Nikiwa ndani ya usafiri, nikaketi nyuma kabisa nikiwa nimepakana na mwanaume mmoja atafunaye bubblegum. Alivalia koti jeusi la ngozi na uso wake ulikuwa serious akitazama mbele. Kitu ambacho kingenifanya nimkumbuke mwanaume huyo ni namna ambavyo mustachi wake ulikuwa mpana na mrefu, na pengine macho yake ya kusinzia.
Mbali na hivyo sikumjali sana. Nilipowasili nimapotakiwa kushuka, nikanyanyuka, na yeye huku nyuma yangu akasimama, sikujali sana, nikashuka na punde naye akafanya hivyo.
Hapa niliposhukia palikuwa na umbali kidogo na hotelini. Tuseme ni kama mwendo wa dakila kumi. Na nilishukia hapa, kwa makusudi ya kuendeleea kuusoma mji kwani niliona ni vema pia endapo nikafahamu eneo linalozunguka mahali nilipofikia.
Nikatembea nikiwa nimedumbukiza mikono yangu mfukoni. Hatua zangu zikiwa pana ila za taratibu nikirusha macho kushoto na kulia.
Nikiwa katika zoezi langu hilo, kama baada ya dakika mbili, nikagundua kuna watu wawili wananifuata kwa nyuma. Wote walikuwa wanaume na sikuwaona vema kutokana ma uelekeo wa mwanga. Ila kidogo baada ya kusonga, nikamtambua mmoja wao kuwa ndiye yule niliyekaa naye kwenye usafiri wa basi. Mwanaume mwenye mustachi na koti la ngozi.
Sikujua wanataka nini kwangu, ila ni wazi niliamini dhamira yao si safi, basi nikaongeza ukubwa wa hatua zangu na mikono nikaitoa mfukoni iwe huru kwa kufanya lolote lile.
Nilipofanya hivyo nao wakajiongeza. Nikahisi hatua zao zimeongezeka na sasa wanakaribia kukimbia. Hapa nikawaza upesi, je swala langu la kukimbilia hotelini litakuwa na maana? Vipi kama hawajui ninapokaa, si n’takuwa nimewapeleka? Lakini pia nikawaza, je watakuwa ni watu wenye taarifa za ujio wangu wa kigeni katika jiji hili, nchi hii?
Watakuwa ni watu wanaohusika na kupotea kwa Raisi?
Maswali haya yakanifanya nisione stara kuwakimbia. Pengine naweza kupata kitu kitakachonisaidia na upelelezi wangu. Basi nikafanya hiyana na kujifichia ndani ya kichochoro fulani. Hapo punde nikawaona wakija, wakaduwaa kutafuta na kutazama.
Mimi nilikuwa nimejibana nyuma ya ndoo kubwa ya malighafi ya chuma nyepesi, ndoo ya kuhifadhia uchafu. Kwakuwa kichochoro hiki hakikuwa na taa, haikuwa rahisi kwao kuniona. Lakini … walianza kuhisi nitakuwa nimejifichia hapo. Nikawaona wakitazamana na mmoja akamtikisia kichwa mwenzake kisha taratibu wakaanza kusonga wakifuata ndoo niliyokuwa nyuma yake!
Mikono yao ya kulia niliiona ikiwa imezama kotini. Bila shaka kushikilia bunduki.
Hapa ikanilazimu nifanye maamuzi ya upesi kuokoa roho yangu.

**
 
*NYUMA YAKO – 12*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Mikono yao ya kulia niliiona ikiwa imezama kotini. Bila shaka kushikilia bunduki.
Hapa ikanilazimu nifanye maamuzi ya upesi kuokoa roho yangu.
ENDELEA
Ni upesi nikanyanyuka nikiwa nimebebelea ile ndoo ya taka, nikawatupia! Wakiwa wamedaka na kudondoka nayo chini, nikawawahi nisiwape muda wa kujiandaa. Mmoja nikampoka bunduki na kisha nikamdaka na kumwekea tundu la bunduki kichwani nikimwamuru mwingine aweke silaha yake chini.
“Fanya upesi kabla sijammwaga mwenzio ubongo!”
Huyu niliyekuwa nimemdaka alikuwa ni yule mwanaume niliyekuwa naye kwenye basi. Mwenzake, mwanaume mrefu mwenye mwili mpana, akan’tazama kwa mashaka kama mtu ajiulizaye nini cha kufanya.
“Nimesema weka silaha chini!” Nikamwamuru. “sitasema tena sasa hivi, utaokota maiti ya mwenzako!”
Basi akainama na kuweka silaha yake chini akiwa anan’tazama kwa kukodoa.
“Ninyi ni wakina nani?” nikauliza. “Kwanini mnanifuata?”
Kimya. Hamna aliyenijibu. Nikarudia tena kuwauliza mara hii nikikaza sauti zaidi, lakini haikuleta tofauti! Hakuna aliyenijibu.
“Sina muda wa kupoteza na ninyi! Kama hamtanipa majibu ya maswali yangu basi nitawamaliza maana haitakuwa hasara kwangu.”
Nilipomaliza tu hiyo kauli, bwana yule niliyekuwa nimemkaba, akawahi kuudaka mkono wangu wenye silaha, akajigeuza upesi akitaka kufanya shambulio kwa ngumi ila kwa upesi nikamkwepa, na nilipoona yule mwenzake ametwaa bunduki aliyoiweka chini, nikafanya jitihada za haraka za kumdaka mwanaume yule mwenye mustachi na kisha nikajikinga naye.
Hapo mwenzake akapata kigugumizi cha kufyatua bunduki, nikamtupia risasi mbili na kumlaza chini hajiwezi. Kisha mwanaume yule niliyemkaba nikamziraisha na kumweka begani. Ikanipasa niondoke mapema eneo hilo kwani milio ya bunduki ingewafanya vyombo vya usalama kujongea hapo muda si mrefu.

**

Saa moja usiku …

Baada ya kutoka kuoga, nilijifuta maji na kisha kumjongea mateka wangu ambaye nilikuwa nimemfungia kitini. Alikuwa bado hajarudi fahamuni hivyo nikamwagia maji na kumtaka ajibu maswali yangu kama salama ya roho yake.
Lakini mwanaume huyo hakuogopa kabisa. Akiwa anan’tazama usoni, akaniambia hatajibu swali langu hata moja. Na nikitaka nimuue pasipo kujichosha. Hapo ikabidi nitafute namna ya kumfanya aongee.
Nikamnyanyua na kumpeleka bafuni. Nikamvika mfuko wa kitambaa kichwa kizima na kuanza kumwagia maji usoni mwake kumnyima pumzi. Akahangaika sana. Lakini kila nilipouvua mfuko huo na kumuuliza, bado hakuwa tayari!
Nikamtesa sana mpaka mwishowe akawa amepoteza nguvu kabisa. Macho yalilegea na mdomo akaacha wazi akitapika maji, ila bado hakuwa amenipa majibu ya maswali yangu. Bado alikuwa na roho ngumu!
Basi nikaona nimpe mapumziko alafu tutaendelea tena muda utakaporuhusu, kwa muda huo nikawasiliana na Daniele na kumwambia yaliyotukia. Naye akaniambia hatua aliyofikia pamoja na timu yake. Siku hiyo alikuwa ameonana na Makamu wa Raisi na pia mke wa Raisi. Wote alifanikiwa kuwafanyia mahojiano lakini hakuna kikubwa alichoking’amua, zaidi mke wa Raisi alikuwa anaumwa na anatazamia kwenda kwao, Australia, kwa ajili ya mapumziko.
Na zaidi ya yote, alipata taarifa kuwa O’Neil, yule bwana aliyetupatia kiasi kidogo cha taarifa, amekutwa akiwa amekufa huko Massachusetts! Mwili wake umekutwa ukiwa mtupu na ishara ya kupitia mateso.
Habari hiyo ikanishtua kwa namna yake. Nani atakuwa amemuua O’Neil? Na je kifo chake kitakuwa na mahusiano na taarifa zile alizotupatia?
Nikamtaka Daniele afuatilie kwa undani juu ya kifo hicho kwani kitakuwa nacho kina mlango wa kutupeleka tunapopahitaji. Basi hata nilipokata simu, nikaendelea kuwaza juu ya kifo cha O’neil. Si bure mzee yule hakuwa anataka kujihusisha na haya mambo!
Lakini kifo hiko kikanipa maswali sana juu ya wauaji. Je pia watakuwa wanajua kuhusu mimi na taarifa zile za bwana O’neil?
Mara mlango ukagongwa na kuniamsha toka kwenye lindi la mawazo. Nikanyanyuka toka kitandani na kwenda mlangoni kumkuta mhudumu. Mwanamke mrembo mwenye mashavu mekundu. Aliniambia kuhusu chakula, kipo tayari kwenye hall, lakini kabla hajaenda, bwana yule niliyekuwa nimemfungia bafuni, akaanza kupiga kelele akigugumia!
Mhudumu akan’tazama kwa hofu, nami kumpoza nikamwambia huyo ni mwenzangu yu hoi anaumwa. Lakini ni wazi maneno hayo hayakumkosha mhudumu, akaenda zake akiwa na sura ya mashaka, na hata mwendo wake ukiwa wa kasi!
Muda kidogo, kama dakika mbili, mlango ukagongwa kwanguvu. Kabla sijauendea nikauliza, “Nani?” sauti ya kiume ikanijibu, “Staff!”
Taratibu nikasonga na kuchungulia nje kwa kupitia tundu mlangoni. Huko nikaona majibaba mawili wakiwa wamevalia sare za hoteli. Walikuwa ni walinzi. Hapa nikapata kujua kuwa mhudumu yule alienda kutoa taarifa juu ya sauti ile alosikia chumbani mwangu.
Nikaufungua mlango, na pasipo kuonyesha lolote usoni mwangu, nikawauliza, “naweza kuwasaidia?”
“Tumekuja kufanya ukaguzi chumbani mwako!” mmoja akajibu akinitazama machoni.
“Mtakaguaje chumba cha mteja?” nikawauliza nikiwakunjia ndita.
“Ndugu, ni jukumu letu kuhakikisha kuna usalama ndani ya hoteli. Kama unaona ni shida, basi tuwaite polisi watekeleze hilo!” akasema yule bwana aliyejielezea hapo awali. Kidogo nikafikiria na kuona ni kheri nikawaruhusu watu hao waingie ndani na kufanya ukaguzi kuliko ujio wa polisi hapo.
Basi, kama watu wanaofahamu kinachoendelea, wakanyookea bafuni, huko wakamkuta bwana yule niliyemfungia. Wakamfungua kamba toka kwenye kiti na kumweka huru. Kisha mimi wakaniweka chini ya ulinzi wakinituhumu kama mtekaji!
“Upo sawa?” Mmoja akamuuliza yule bwana waliyemwacha huru. Naye kwa uchovu akawajibu, “nipo sawa, nashukuru.”
Wakamuuliza kwanini mimi nilimfungia kule bafuni, naye akatoa maelezo ya wongo kuwa nilitaka kumuua kisa nikitaka pesa toka kwake, basi walinzi wakapiga simu polisi kutoa taarifa juu yangu.
“Huyo anawaongopea,” nikapaza sauti. “ni yeye ndiye anataka kuniua. Yeye pamoja na mwenziwe!”
Lakini nani aniamini? Mazingira yalikuwa yananisaliti na kuninyooshea kidole kuwa mimi ni muuaji. Basi tukiwa hapo, ndani ya muda mfupi tu, yule jamaa, jambazi, kwa upesi akawadhibiti walinzi wa hoteli na kuwaweka chini ya ulinzi. Alitumia bunduki niliyompokonya. Bunduki hiyo nilikuwa nimeiweka kwenye droo ya kitanda.
Alipofanikisha hilo, akaninyooshea tundu la risasi na kuniamuru niseme kile kilichonileta Ujerumani. Tena niseme upesi kabla hajanimaliza aende zake.
Nikamwambia huku nikinyoosha mkono juu, “mimi ni mtalii tu! Sitambui kwanini wanifuatilia namna hii!”
“Usinifanye mimi ni mjinga! Natambua kinachoendelea na kama uki—” hakumalizia, nikawa nimemtupia stuli iliyokuwa imesimama kando yangu. Stuli hiyo kwakuwa niliitupa kwanguvu, ikafyeka miguu yake na kumwangusha chini! Kabla hajaamka, walinzi wakamuwahi kumpokonya silaha, ila ajabu akafurukuta kwanguvu na kumtupa mlinzi mmoja kando kwa kumkandika teke zito. Na huyo mwingine akamchapa kiwiko na kisha ngumi nzito, akalala kando amezirai.
Kabla hajateka tena bunduki, nikajitupa na kuunyoosha mguu wangu kuisogezea mbali kwa teke, alafu nikaunyanyua kutaka kumkandika kifuani. Akakwepa. Akajirushia mgongo kunifuata. Akatupa ngumi yake, nikaiyeya, ya pili nikaidaka na kuiviringita! Akajizungusha na kutupa kiwiko, nacho nikakisogezea pembeni na alafu kumdaka shingo yake na kumkaba kwanguvu zangu zote.
Akatapatapa akituma viwiko vyake. Havikunipata. Ila kimoja kilitifua mbavu yangu na kunipa maumivu makali. Nikavumilia na kuendelea kumkaba. Akatupa tena kingine, hakikunipata, cha tatu kikanitifua tena. Hapo nikashindwa kuvumilia!
Bwana huyu akajichomoa toka kwenye mikono yangu na kisha akaniadhibu kwa ngumi ya shavu la kulia. Mdomo ukalowana damu. Lakini sikumruhusu achukue bunduki. Alipotaka kufanya hivyo, nikamuwahi kumvuta. Akatupa teke, nalo nikamdaka na kumvuta kwanguvu, alafu nikamrukia mgongoni na kumkaba tena. Mara hii mikono yake niliikandamizia na magoti yangu, hakuweza kufurukuta!
Akapoteza kabisa nguvu. Macho yakaanza kuelekea juu. Nikalegeza mikono yangu na kumuuliza ametumwa na nani. Kwa mbali nikamsikia akisema, “Rodolfo!” kisha akazirai!

***
 
*NYUMA YAKO – 12*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Mikono yao ya kulia niliiona ikiwa imezama kotini. Bila shaka kushikilia bunduki.
Hapa ikanilazimu nifanye maamuzi ya upesi kuokoa roho yangu.
ENDELEA
Ni upesi nikanyanyuka nikiwa nimebebelea ile ndoo ya taka, nikawatupia! Wakiwa wamedaka na kudondoka nayo chini, nikawawahi nisiwape muda wa kujiandaa. Mmoja nikampoka bunduki na kisha nikamdaka na kumwekea tundu la bunduki kichwani nikimwamuru mwingine aweke silaha yake chini.
“Fanya upesi kabla sijammwaga mwenzio ubongo!”
Huyu niliyekuwa nimemdaka alikuwa ni yule mwanaume niliyekuwa naye kwenye basi. Mwenzake, mwanaume mrefu mwenye mwili mpana, akan’tazama kwa mashaka kama mtu ajiulizaye nini cha kufanya.
“Nimesema weka silaha chini!” Nikamwamuru. “sitasema tena sasa hivi, utaokota maiti ya mwenzako!”
Basi akainama na kuweka silaha yake chini akiwa anan’tazama kwa kukodoa.
“Ninyi ni wakina nani?” nikauliza. “Kwanini mnanifuata?”
Kimya. Hamna aliyenijibu. Nikarudia tena kuwauliza mara hii nikikaza sauti zaidi, lakini haikuleta tofauti! Hakuna aliyenijibu.
“Sina muda wa kupoteza na ninyi! Kama hamtanipa majibu ya maswali yangu basi nitawamaliza maana haitakuwa hasara kwangu.”
Nilipomaliza tu hiyo kauli, bwana yule niliyekuwa nimemkaba, akawahi kuudaka mkono wangu wenye silaha, akajigeuza upesi akitaka kufanya shambulio kwa ngumi ila kwa upesi nikamkwepa, na nilipoona yule mwenzake ametwaa bunduki aliyoiweka chini, nikafanya jitihada za haraka za kumdaka mwanaume yule mwenye mustachi na kisha nikajikinga naye.
Hapo mwenzake akapata kigugumizi cha kufyatua bunduki, nikamtupia risasi mbili na kumlaza chini hajiwezi. Kisha mwanaume yule niliyemkaba nikamziraisha na kumweka begani. Ikanipasa niondoke mapema eneo hilo kwani milio ya bunduki ingewafanya vyombo vya usalama kujongea hapo muda si mrefu.

**

Saa moja usiku …

Baada ya kutoka kuoga, nilijifuta maji na kisha kumjongea mateka wangu ambaye nilikuwa nimemfungia kitini. Alikuwa bado hajarudi fahamuni hivyo nikamwagia maji na kumtaka ajibu maswali yangu kama salama ya roho yake.
Lakini mwanaume huyo hakuogopa kabisa. Akiwa anan’tazama usoni, akaniambia hatajibu swali langu hata moja. Na nikitaka nimuue pasipo kujichosha. Hapo ikabidi nitafute namna ya kumfanya aongee.
Nikamnyanyua na kumpeleka bafuni. Nikamvika mfuko wa kitambaa kichwa kizima na kuanza kumwagia maji usoni mwake kumnyima pumzi. Akahangaika sana. Lakini kila nilipouvua mfuko huo na kumuuliza, bado hakuwa tayari!
Nikamtesa sana mpaka mwishowe akawa amepoteza nguvu kabisa. Macho yalilegea na mdomo akaacha wazi akitapika maji, ila bado hakuwa amenipa majibu ya maswali yangu. Bado alikuwa na roho ngumu!
Basi nikaona nimpe mapumziko alafu tutaendelea tena muda utakaporuhusu, kwa muda huo nikawasiliana na Daniele na kumwambia yaliyotukia. Naye akaniambia hatua aliyofikia pamoja na timu yake. Siku hiyo alikuwa ameonana na Makamu wa Raisi na pia mke wa Raisi. Wote alifanikiwa kuwafanyia mahojiano lakini hakuna kikubwa alichoking’amua, zaidi mke wa Raisi alikuwa anaumwa na anatazamia kwenda kwao, Australia, kwa ajili ya mapumziko.
Na zaidi ya yote, alipata taarifa kuwa O’Neil, yule bwana aliyetupatia kiasi kidogo cha taarifa, amekutwa akiwa amekufa huko Massachusetts! Mwili wake umekutwa ukiwa mtupu na ishara ya kupitia mateso.
Habari hiyo ikanishtua kwa namna yake. Nani atakuwa amemuua O’Neil? Na je kifo chake kitakuwa na mahusiano na taarifa zile alizotupatia?
Nikamtaka Daniele afuatilie kwa undani juu ya kifo hicho kwani kitakuwa nacho kina mlango wa kutupeleka tunapopahitaji. Basi hata nilipokata simu, nikaendelea kuwaza juu ya kifo cha O’neil. Si bure mzee yule hakuwa anataka kujihusisha na haya mambo!
Lakini kifo hiko kikanipa maswali sana juu ya wauaji. Je pia watakuwa wanajua kuhusu mimi na taarifa zile za bwana O’neil?
Mara mlango ukagongwa na kuniamsha toka kwenye lindi la mawazo. Nikanyanyuka toka kitandani na kwenda mlangoni kumkuta mhudumu. Mwanamke mrembo mwenye mashavu mekundu. Aliniambia kuhusu chakula, kipo tayari kwenye hall, lakini kabla hajaenda, bwana yule niliyekuwa nimemfungia bafuni, akaanza kupiga kelele akigugumia!
Mhudumu akan’tazama kwa hofu, nami kumpoza nikamwambia huyo ni mwenzangu yu hoi anaumwa. Lakini ni wazi maneno hayo hayakumkosha mhudumu, akaenda zake akiwa na sura ya mashaka, na hata mwendo wake ukiwa wa kasi!
Muda kidogo, kama dakika mbili, mlango ukagongwa kwanguvu. Kabla sijauendea nikauliza, “Nani?” sauti ya kiume ikanijibu, “Staff!”
Taratibu nikasonga na kuchungulia nje kwa kupitia tundu mlangoni. Huko nikaona majibaba mawili wakiwa wamevalia sare za hoteli. Walikuwa ni walinzi. Hapa nikapata kujua kuwa mhudumu yule alienda kutoa taarifa juu ya sauti ile alosikia chumbani mwangu.
Nikaufungua mlango, na pasipo kuonyesha lolote usoni mwangu, nikawauliza, “naweza kuwasaidia?”
“Tumekuja kufanya ukaguzi chumbani mwako!” mmoja akajibu akinitazama machoni.
“Mtakaguaje chumba cha mteja?” nikawauliza nikiwakunjia ndita.
“Ndugu, ni jukumu letu kuhakikisha kuna usalama ndani ya hoteli. Kama unaona ni shida, basi tuwaite polisi watekeleze hilo!” akasema yule bwana aliyejielezea hapo awali. Kidogo nikafikiria na kuona ni kheri nikawaruhusu watu hao waingie ndani na kufanya ukaguzi kuliko ujio wa polisi hapo.
Basi, kama watu wanaofahamu kinachoendelea, wakanyookea bafuni, huko wakamkuta bwana yule niliyemfungia. Wakamfungua kamba toka kwenye kiti na kumweka huru. Kisha mimi wakaniweka chini ya ulinzi wakinituhumu kama mtekaji!
“Upo sawa?” Mmoja akamuuliza yule bwana waliyemwacha huru. Naye kwa uchovu akawajibu, “nipo sawa, nashukuru.”
Wakamuuliza kwanini mimi nilimfungia kule bafuni, naye akatoa maelezo ya wongo kuwa nilitaka kumuua kisa nikitaka pesa toka kwake, basi walinzi wakapiga simu polisi kutoa taarifa juu yangu.
“Huyo anawaongopea,” nikapaza sauti. “ni yeye ndiye anataka kuniua. Yeye pamoja na mwenziwe!”
Lakini nani aniamini? Mazingira yalikuwa yananisaliti na kuninyooshea kidole kuwa mimi ni muuaji. Basi tukiwa hapo, ndani ya muda mfupi tu, yule jamaa, jambazi, kwa upesi akawadhibiti walinzi wa hoteli na kuwaweka chini ya ulinzi. Alitumia bunduki niliyompokonya. Bunduki hiyo nilikuwa nimeiweka kwenye droo ya kitanda.
Alipofanikisha hilo, akaninyooshea tundu la risasi na kuniamuru niseme kile kilichonileta Ujerumani. Tena niseme upesi kabla hajanimaliza aende zake.
Nikamwambia huku nikinyoosha mkono juu, “mimi ni mtalii tu! Sitambui kwanini wanifuatilia namna hii!”
“Usinifanye mimi ni mjinga! Natambua kinachoendelea na kama uki—” hakumalizia, nikawa nimemtupia stuli iliyokuwa imesimama kando yangu. Stuli hiyo kwakuwa niliitupa kwanguvu, ikafyeka miguu yake na kumwangusha chini! Kabla hajaamka, walinzi wakamuwahi kumpokonya silaha, ila ajabu akafurukuta kwanguvu na kumtupa mlinzi mmoja kando kwa kumkandika teke zito. Na huyo mwingine akamchapa kiwiko na kisha ngumi nzito, akalala kando amezirai.
Kabla hajateka tena bunduki, nikajitupa na kuunyoosha mguu wangu kuisogezea mbali kwa teke, alafu nikaunyanyua kutaka kumkandika kifuani. Akakwepa. Akajirushia mgongo kunifuata. Akatupa ngumi yake, nikaiyeya, ya pili nikaidaka na kuiviringita! Akajizungusha na kutupa kiwiko, nacho nikakisogezea pembeni na alafu kumdaka shingo yake na kumkaba kwanguvu zangu zote.
Akatapatapa akituma viwiko vyake. Havikunipata. Ila kimoja kilitifua mbavu yangu na kunipa maumivu makali. Nikavumilia na kuendelea kumkaba. Akatupa tena kingine, hakikunipata, cha tatu kikanitifua tena. Hapo nikashindwa kuvumilia!
Bwana huyu akajichomoa toka kwenye mikono yangu na kisha akaniadhibu kwa ngumi ya shavu la kulia. Mdomo ukalowana damu. Lakini sikumruhusu achukue bunduki. Alipotaka kufanya hivyo, nikamuwahi kumvuta. Akatupa teke, nalo nikamdaka na kumvuta kwanguvu, alafu nikamrukia mgongoni na kumkaba tena. Mara hii mikono yake niliikandamizia na magoti yangu, hakuweza kufurukuta!
Akapoteza kabisa nguvu. Macho yakaanza kuelekea juu. Nikalegeza mikono yangu na kumuuliza ametumwa na nani. Kwa mbali nikamsikia akisema, “Rodolfo!” kisha akazirai!

***
Kazi kazi
 

Similar Discussions

11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom