SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,430
- 23,748
- Thread starter
- #21
*NYUMA YAKO – 18*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.
ENDELEA
Nilifahamu ndani ya msitu ule sitakosa ninachotaka. Nikakimbia upesi na kufanya jitihada za kuangaza macho yangu nikitumia stadi niliyonayo juu ya madawa ya asili. Tulifunzwa hii. Tulifunzwa namna ya kudumu na kumudu kwenye hali mbalimbali kama hizi.
Ndani ya muda mfupi, nikapata kuona kichaka chenye majani membamba na ncha kana kwamba sindano. Nikajongea hapo na kuchuma majani kadhaa na kuyatia mdomoni kutafuna alafu nikaanza kurudi upesi kule kwa yule mwanamama na mwanaye.
Nilipofika majani mdomoni mwangu yalikuwa tayari yashalainika vya kutosha. Nilikunja sura kwa uchungu wake mithili ya shubiri. Nikayatema na kumpachika yule mtoto eneo lake la jeraha alafu nikachana sehemu ya shati langu kutengeneza bandeji, nikamfungia hapo kichwani na kumweka mtoto huyo begani tuendelee na safari.
Tukiwa tunatembea, nikapata sasa wasaa wa kumuuliza maswali kadhaa. Niliona huu ni muda muhimu wa kufanya hivyo maana lolote linaweza kutokea muda wowote. Basi likitokea, angalau niwe nimetimiza robo ya haja yangu.
“Wewe ni nani? Kwanini watu hawa wamekuteka?” Niliuliza nikimtazama mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa ukakamavu. Alikuwa na ushupavu ndani yake.
Akanitazama na kunyamaza kwanza akipiga hatua. Alipovuta pumzi ndefu ndipo akanijibu pasipo kunitazama, “Nilidhani utakuwa unanijua ndo’ maana ukaja kuntafuta.” Kisha akaniuliza, “Ajenti, umekujaje kumtafuta mtu ambaye humjui?”
“Umejuaje kama mimi ni ajenti?”
Akatabasamu. “Anayeweza kuyafanya yote haya, ni raia wa kawaida?” kabla sijanena akaendelea kunena, “Umefanya kazi kweli kujua wapi nilipo. Hata sasa kuwa hai unastahili pongezi.”
Nikamtazama na pasipo kuongea nikarudisha macho yangu mbele tuendako nikitarajia mwanamke huyo ataendelea kunena.
“Mimi ni raia wa kawaida kabisa. Ni mmarekani ninayeishi Ujerumani pamoja na mwanangu. Sina shida nyingine na mtu!”
“Huku Ujerumani unafanya nini? Na kwanini Ujerumani?”
“Una maswali mengi sana. Sidhani kama nipo kwenye mood ya kukata kiu chako. Pengine baadae nikiwa nimetulia.”
“Wamekufanya lolote ulipokuwa chini yao?”
Akatikisa kichwa. “wasingeweza kunifanya kitu.”
Nikamtazama kwa maulizo pasipo kusema kitu. Nadhani yeye mwenyewe akajiongeza na kunijibu swali langu la kimya. “Bado wananihitaji. Mimi ni asset kwao. Hawawezi kunidhuru.”
“Unamaanisha nini wewe ni asset?”
“Nimekuambia una maswali mengi. Najua. Tutakapotulia nitakuambia, pengine nitakata kiu chako.”
“Hauwezi ukanambia hata machache?”
“Naitwa Britney. Ni raia wa Marekani. Nadhani hayo yanakutosha.”
Sikutaka kusumbuana naye. Niliona ninyamaze kimya, kweli hayupo kwenye mood, japo kifuani mwangu nilikuwa nalaumu sana kutokujua kinachoendelea ingali tulipokuwa kitu chochote kingeweza kujiri.
Tukatembea kwa kama dakika kumi, akantazama kisha asiseme kitu akatazama zake mbele. Nadhani alikuwa anajiuliza maswali kichwani. Baada ya sekunde kadhaa, akasema, “Naomba umtazame mwanangu. Yeye ndo’ kitu pekee nilichonacho kwa sasa.” Kisha akasimama na kun’tazama. Nami nikasimama. Akaniambia, “Niahidi hilo … niahidi mtoto wangu atakuwa salama.”
“Nakuahidi,” nikasema kwa sauti ya kutikisika. Akaniuliza, “Unaniahidi?”
“Ndio, nakuahidi,” saa hii nikasema kwa kujiamini. Basi akaridhika tukaendelea na safari. Akaniambia kama tukitembea kwa takribani robo saa tutakuwa tumefika barabarani.
Tukatembea kwa kama dakika sita, yeye mwenyewe akaanza kuongea. “Nimemkumbuka sana mama yangu,” sauti yake ilikuwa ya mtu anayekaribia kulia.
“Kama ningalifuata alichonambia, nisingalikuwa hapa.”
Nikamtazama nisimsemeshe kitu. Nilihofia maneno yangu yangeweza kumkatiza. Nilimwacha afanye vile alivyokuwa anataka.
Akavuta makamasi mepesi kisha akaendelea, “Sasa nimekuwa mkimbizi nisiye na makazi. Toka kwenye kamera za mwanga mpaka kujificha chini ya uvungu na nyuma ya milango. Ama kweli maisha huweza badilika ndani ya sekunde moja tu!
Ndani ya sekunde moja mtu akawa kilema. Akapoteza alivyovipata kwa masaa. Ndani ya muda huo mchache akawa amebadili mwelekeo wa maisha yake.”
Nikaendelea kumtazama pasipo kutia neno. Niliona uso wake ukiwa umebadilika rangi kuwa mwekundu. Alikifikicha pua yake na kumwaga tena maneno, “Hakuna anayejua kesho yake, sio? … mimi sikudhani kama siku moja ntakuja kuwa na familia. Sikuwa nawaza hilo jambo kabisa, labda kwasababu ya aina ya maisha niliyoyachagua.
Maisha yalonifanya ninyooshewe kidole kila nilipopita nikionekana laana, mchafu na niliyelaaniwa. Sikutaka mwanangu aje kushea laana yangu. Ashindwe kupita mtaani kwasababu ya mama yake. Ni adhabu. Najua ukubwa wa adhabu hiyo maana nimeibeba mgongoni kwa muda mrefu. Inachosha na kuumiza.
Watamani kukaa mbali na walimwengu ambao ni wepesi wa kuhukumu na wachoyo wa fadhila. Lakini ajenti, wawezaa kukaa mbali na dunia?”
Aliniuliza akintazama. Nikamtikisa kichwa kukataa pasipo kutia neno. Basi akatabasamu kwa mbali na kisha akakaa kimya kidogo. Tukatembea kwa kama dakika moja asinene jambo ila nikiamini ataendelea tu kusema.
Nilihisi ana kitu kifuani. Atajihisi mwepesi endapo atakitoa.
Akajifuta machozi na mikono ya sweta lake alafu akatazama juu kwenye matawi ya miti, pembeni na kisha mbele.
“Hata kama niki –”
“Shhh!” nikamzuia upesi nikimwonyeshea ishara ya kidole mdomoni. Kuna kitu nilihisi. Tulisimama tukatulia tuli na kutazama kushoto na kulia. Masikio yangu yalinambia nimesikia sauti ya watu wakiteta. Na sikuwa nimekosea, lah! Nyuma yetu kwa umbali, tukawaona wanaume wawili waliokuwa wamevalia nguo nyeusi na mikononi mwao wana bunduki ndefu!
Wanaume hawa hawakuwa na usafiri, bali wakitumia miguu yao.
Haraka nikamtaka Britney akimbie na mie kabla sijafungua miguu yangu nikafyatua risasi kuwalenga wanaume wale kuwapumbazisha kwa muda kidogo.
Tukakimbia na kukimbia. Nao wale wanaume wakawa wanaendelea kutukimbiza, wakawa pia wanatupa risasi wakijaribu kunilenga.
Nikiwa nimembebelea mtoto, nikakimbia kwa kasi na kwanguvu mpaka kumwacha Britney nyuma. Si kwamba alikuwa anakimbia taratibu, hapana! Na wala hakuonekana mtu anayehitaji msaada. Alikuwa anajimudu kukimbia.
Hatukudumu muda mrefu mbioni, nikasikia risasi ya karibu zaidi na kisha sauti ya kike ikilalama! Kutazama, nikamwona Britney akidondoka chini!
“Shit!” nikamsikia mmoja wale wajamaa wanaotukimbiza akilaani, kisha kwa punde akamlaumu mwenzake kwa kumfyatulia risasi Britney. Hapa nikatumia nafasi hiyo upesi kuwamiminia risasi na kuwalaza chini.
Nikamtazama Britney. Alikuwa amelengwa kwenye shina la nyuma la shingo. Risasi ilivunja uti wake wa mgongo! Ilikuwa ngumu kwake kupona. Damu zilimtiririka. Macho yake yalimwaga machozi akinishika kwanguvu na kung’ata meno yake.
“Ajenti, mtazame vema mwanangu,” akasema akikwamakwama. Kisha akaninong’oneza, “Naitwa Juliette Simpson. Natumai utakuwa unanijua.” Alafu akajifia.
Akafa mbele ya macho yangu. Akafa mwanaye akiwa bado hajitambui.
Nikawaendea wale wanaume niliowaua na kuwapekua. Sikuwakuta na kitu zaidi ya bunduki na risasi kadhaa. Nikazichukua. Nilipomrudia Britney ambaye kabla hajafa alinipa jina lingine, naye nikampekua kama ana kitu. Alikuwa mtupu.
Nikapata maswali juu ya nini cha kufanya. Haraka nikatoa simu yangu na kumchukua picha kadhaa, nashukuru simu yangu haikuwa simu inayoingiza maji.
Nikiwa nimempiga picha mbili tu, nikasikia tena sauti ya watu, hiyo ikawa ishara kuwa sitakiwi kukaa hapo tena. Nikaanza kukimbia. Huko nyuma nikasikia, “Yule!” na vishindo vya watu vikinifuata kwa kasi!
Nikakimbia sana lakini nguvu zangu hazikuwa kama za hapo awali, nilichoka mno. Kumbeba mtu kwa muda wote ule huku nikikimbia na kutembea haikuwa jambo jepesi. Hivyo basi nikaanza kupunguza kasi ya mwendo wangu na kupelekea wale maadui wanikaribie zaidi!
Wakatupa risasi kadhaa. Nashukuru miti ilinikinga. Nilisikia zikipasua na kugotea mitini. Nilipoona maji yanazidi kupiku unga, nazidi kukaribiwa na hali ni mbaya, nikakimbilia mtoni na kujitosea humo!
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.
***
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Tulipofika pakavu, nikamtazama mtoto na kubaini alikuwa amejigonga kwenye jiwe ingali tu mtoni. Na kwa namna alivyokuwa anatoka damu, inabidi ifanyike namna upesi ya kumsaidia, la sivyo alikuwa anatuacha!
Nikamwambia mama yake, “gandamizia mahali pa jeraha, nakuja!” mimi nikaenda kutafuta majani yatakayoweza kumsaidia jerahani.
ENDELEA
Nilifahamu ndani ya msitu ule sitakosa ninachotaka. Nikakimbia upesi na kufanya jitihada za kuangaza macho yangu nikitumia stadi niliyonayo juu ya madawa ya asili. Tulifunzwa hii. Tulifunzwa namna ya kudumu na kumudu kwenye hali mbalimbali kama hizi.
Ndani ya muda mfupi, nikapata kuona kichaka chenye majani membamba na ncha kana kwamba sindano. Nikajongea hapo na kuchuma majani kadhaa na kuyatia mdomoni kutafuna alafu nikaanza kurudi upesi kule kwa yule mwanamama na mwanaye.
Nilipofika majani mdomoni mwangu yalikuwa tayari yashalainika vya kutosha. Nilikunja sura kwa uchungu wake mithili ya shubiri. Nikayatema na kumpachika yule mtoto eneo lake la jeraha alafu nikachana sehemu ya shati langu kutengeneza bandeji, nikamfungia hapo kichwani na kumweka mtoto huyo begani tuendelee na safari.
Tukiwa tunatembea, nikapata sasa wasaa wa kumuuliza maswali kadhaa. Niliona huu ni muda muhimu wa kufanya hivyo maana lolote linaweza kutokea muda wowote. Basi likitokea, angalau niwe nimetimiza robo ya haja yangu.
“Wewe ni nani? Kwanini watu hawa wamekuteka?” Niliuliza nikimtazama mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa ukakamavu. Alikuwa na ushupavu ndani yake.
Akanitazama na kunyamaza kwanza akipiga hatua. Alipovuta pumzi ndefu ndipo akanijibu pasipo kunitazama, “Nilidhani utakuwa unanijua ndo’ maana ukaja kuntafuta.” Kisha akaniuliza, “Ajenti, umekujaje kumtafuta mtu ambaye humjui?”
“Umejuaje kama mimi ni ajenti?”
Akatabasamu. “Anayeweza kuyafanya yote haya, ni raia wa kawaida?” kabla sijanena akaendelea kunena, “Umefanya kazi kweli kujua wapi nilipo. Hata sasa kuwa hai unastahili pongezi.”
Nikamtazama na pasipo kuongea nikarudisha macho yangu mbele tuendako nikitarajia mwanamke huyo ataendelea kunena.
“Mimi ni raia wa kawaida kabisa. Ni mmarekani ninayeishi Ujerumani pamoja na mwanangu. Sina shida nyingine na mtu!”
“Huku Ujerumani unafanya nini? Na kwanini Ujerumani?”
“Una maswali mengi sana. Sidhani kama nipo kwenye mood ya kukata kiu chako. Pengine baadae nikiwa nimetulia.”
“Wamekufanya lolote ulipokuwa chini yao?”
Akatikisa kichwa. “wasingeweza kunifanya kitu.”
Nikamtazama kwa maulizo pasipo kusema kitu. Nadhani yeye mwenyewe akajiongeza na kunijibu swali langu la kimya. “Bado wananihitaji. Mimi ni asset kwao. Hawawezi kunidhuru.”
“Unamaanisha nini wewe ni asset?”
“Nimekuambia una maswali mengi. Najua. Tutakapotulia nitakuambia, pengine nitakata kiu chako.”
“Hauwezi ukanambia hata machache?”
“Naitwa Britney. Ni raia wa Marekani. Nadhani hayo yanakutosha.”
Sikutaka kusumbuana naye. Niliona ninyamaze kimya, kweli hayupo kwenye mood, japo kifuani mwangu nilikuwa nalaumu sana kutokujua kinachoendelea ingali tulipokuwa kitu chochote kingeweza kujiri.
Tukatembea kwa kama dakika kumi, akantazama kisha asiseme kitu akatazama zake mbele. Nadhani alikuwa anajiuliza maswali kichwani. Baada ya sekunde kadhaa, akasema, “Naomba umtazame mwanangu. Yeye ndo’ kitu pekee nilichonacho kwa sasa.” Kisha akasimama na kun’tazama. Nami nikasimama. Akaniambia, “Niahidi hilo … niahidi mtoto wangu atakuwa salama.”
“Nakuahidi,” nikasema kwa sauti ya kutikisika. Akaniuliza, “Unaniahidi?”
“Ndio, nakuahidi,” saa hii nikasema kwa kujiamini. Basi akaridhika tukaendelea na safari. Akaniambia kama tukitembea kwa takribani robo saa tutakuwa tumefika barabarani.
Tukatembea kwa kama dakika sita, yeye mwenyewe akaanza kuongea. “Nimemkumbuka sana mama yangu,” sauti yake ilikuwa ya mtu anayekaribia kulia.
“Kama ningalifuata alichonambia, nisingalikuwa hapa.”
Nikamtazama nisimsemeshe kitu. Nilihofia maneno yangu yangeweza kumkatiza. Nilimwacha afanye vile alivyokuwa anataka.
Akavuta makamasi mepesi kisha akaendelea, “Sasa nimekuwa mkimbizi nisiye na makazi. Toka kwenye kamera za mwanga mpaka kujificha chini ya uvungu na nyuma ya milango. Ama kweli maisha huweza badilika ndani ya sekunde moja tu!
Ndani ya sekunde moja mtu akawa kilema. Akapoteza alivyovipata kwa masaa. Ndani ya muda huo mchache akawa amebadili mwelekeo wa maisha yake.”
Nikaendelea kumtazama pasipo kutia neno. Niliona uso wake ukiwa umebadilika rangi kuwa mwekundu. Alikifikicha pua yake na kumwaga tena maneno, “Hakuna anayejua kesho yake, sio? … mimi sikudhani kama siku moja ntakuja kuwa na familia. Sikuwa nawaza hilo jambo kabisa, labda kwasababu ya aina ya maisha niliyoyachagua.
Maisha yalonifanya ninyooshewe kidole kila nilipopita nikionekana laana, mchafu na niliyelaaniwa. Sikutaka mwanangu aje kushea laana yangu. Ashindwe kupita mtaani kwasababu ya mama yake. Ni adhabu. Najua ukubwa wa adhabu hiyo maana nimeibeba mgongoni kwa muda mrefu. Inachosha na kuumiza.
Watamani kukaa mbali na walimwengu ambao ni wepesi wa kuhukumu na wachoyo wa fadhila. Lakini ajenti, wawezaa kukaa mbali na dunia?”
Aliniuliza akintazama. Nikamtikisa kichwa kukataa pasipo kutia neno. Basi akatabasamu kwa mbali na kisha akakaa kimya kidogo. Tukatembea kwa kama dakika moja asinene jambo ila nikiamini ataendelea tu kusema.
Nilihisi ana kitu kifuani. Atajihisi mwepesi endapo atakitoa.
Akajifuta machozi na mikono ya sweta lake alafu akatazama juu kwenye matawi ya miti, pembeni na kisha mbele.
“Hata kama niki –”
“Shhh!” nikamzuia upesi nikimwonyeshea ishara ya kidole mdomoni. Kuna kitu nilihisi. Tulisimama tukatulia tuli na kutazama kushoto na kulia. Masikio yangu yalinambia nimesikia sauti ya watu wakiteta. Na sikuwa nimekosea, lah! Nyuma yetu kwa umbali, tukawaona wanaume wawili waliokuwa wamevalia nguo nyeusi na mikononi mwao wana bunduki ndefu!
Wanaume hawa hawakuwa na usafiri, bali wakitumia miguu yao.
Haraka nikamtaka Britney akimbie na mie kabla sijafungua miguu yangu nikafyatua risasi kuwalenga wanaume wale kuwapumbazisha kwa muda kidogo.
Tukakimbia na kukimbia. Nao wale wanaume wakawa wanaendelea kutukimbiza, wakawa pia wanatupa risasi wakijaribu kunilenga.
Nikiwa nimembebelea mtoto, nikakimbia kwa kasi na kwanguvu mpaka kumwacha Britney nyuma. Si kwamba alikuwa anakimbia taratibu, hapana! Na wala hakuonekana mtu anayehitaji msaada. Alikuwa anajimudu kukimbia.
Hatukudumu muda mrefu mbioni, nikasikia risasi ya karibu zaidi na kisha sauti ya kike ikilalama! Kutazama, nikamwona Britney akidondoka chini!
“Shit!” nikamsikia mmoja wale wajamaa wanaotukimbiza akilaani, kisha kwa punde akamlaumu mwenzake kwa kumfyatulia risasi Britney. Hapa nikatumia nafasi hiyo upesi kuwamiminia risasi na kuwalaza chini.
Nikamtazama Britney. Alikuwa amelengwa kwenye shina la nyuma la shingo. Risasi ilivunja uti wake wa mgongo! Ilikuwa ngumu kwake kupona. Damu zilimtiririka. Macho yake yalimwaga machozi akinishika kwanguvu na kung’ata meno yake.
“Ajenti, mtazame vema mwanangu,” akasema akikwamakwama. Kisha akaninong’oneza, “Naitwa Juliette Simpson. Natumai utakuwa unanijua.” Alafu akajifia.
Akafa mbele ya macho yangu. Akafa mwanaye akiwa bado hajitambui.
Nikawaendea wale wanaume niliowaua na kuwapekua. Sikuwakuta na kitu zaidi ya bunduki na risasi kadhaa. Nikazichukua. Nilipomrudia Britney ambaye kabla hajafa alinipa jina lingine, naye nikampekua kama ana kitu. Alikuwa mtupu.
Nikapata maswali juu ya nini cha kufanya. Haraka nikatoa simu yangu na kumchukua picha kadhaa, nashukuru simu yangu haikuwa simu inayoingiza maji.
Nikiwa nimempiga picha mbili tu, nikasikia tena sauti ya watu, hiyo ikawa ishara kuwa sitakiwi kukaa hapo tena. Nikaanza kukimbia. Huko nyuma nikasikia, “Yule!” na vishindo vya watu vikinifuata kwa kasi!
Nikakimbia sana lakini nguvu zangu hazikuwa kama za hapo awali, nilichoka mno. Kumbeba mtu kwa muda wote ule huku nikikimbia na kutembea haikuwa jambo jepesi. Hivyo basi nikaanza kupunguza kasi ya mwendo wangu na kupelekea wale maadui wanikaribie zaidi!
Wakatupa risasi kadhaa. Nashukuru miti ilinikinga. Nilisikia zikipasua na kugotea mitini. Nilipoona maji yanazidi kupiku unga, nazidi kukaribiwa na hali ni mbaya, nikakimbilia mtoni na kujitosea humo!
Nilizama maana kina kilikuwa kirefu. Risasi zikatumwa kunifuata ndani ya maji, zikanipitia kupunyua, lakini kwakuwa maji yalikuwa na nguvu na mengi ya kutosha kunipeleka, yakaniepushia na balaa!
Yakanisomba kunisafirisha.
***