Nyota inamaana gani?

Emasaku

Member
Sep 24, 2011
51
6
Salamu wanaJF, Mimi ni kijana wakiume, naombeni mnielimishe kuhusu nyota! Mtu akikwambia nyota yako haingai au inamatatizo inamaana gani? Kwa takribani miaka 3 sasa nimekuwa naplani nzuri za kimaisha, lakini cha ajabu naanza vizuri na baada ya muda si mrefu mambo yanaenda sivyo... Kila biashara ninayofanya napata hasara au nathulumiwa, nikimkopea mtu hela harudishi... Pesa ninazo dai watu inafika karibu mil. 4.
Nilisha ulizia kwa mtaamu mmoja kuhusu swala hili.... Alinipa dawa ya kuongea lakini nilipuzia na kuitupa mbali nikajifanya kumwomba mungu! Swala hili linanimiza kichwa sana, kwa muda wa miezi 2 nimekuwa nachukiwa na karibu marafiki wangu wote, hata mpenzi wangu hataki tena kuwasiliana tena na mimi japo ninamsomesha shule! Jamani naombeni ushauri wenu. Nyota yangu haingai? Nifanye nini? Au niende tena kwa wataamu wa nyota? Kama ndio wapi nitampata wa ukweli? Asante!
 
nyota ukitaka kuijua maana yake nini nenda kagoogle shehe yahaya italeta kila kitu..
 
Usipende kuamini sana watu kwenye mambo ya hela,,kumbuka PALIPO NA WATU 10 BINADAMU NI 1 TU!Habari ya nyota subiri wanajimu watakuja sasa hivi.
 
Emasaku as much as naamini kua ni kweli kila mmoja ana bahati yake
Lingine nielewalo mimi ni kwamba ukiendekeza saana hayo mambo ktk
maisha yako hamna la maana utafanya; For kila ufanyalo yaani ule, ulale,
upate pesa, ukose pesa yaani ufanye lolote utataka kuhusisha na Nyota.
It is not healthy Mkuu, mambo ya nyota fanya for leisure but yasiongoze
kabisa maisha yako.... naamini kupoteza dira ya Maisha ni rahisi ukiendekeza...
Best of Luck....
 
Emasaku as much as naamini kua ni kweli kila mmoja ana bahati yake
Lingine nielewalo mimi ni kwamba ukiendekeza saana hayo mambo ktk
maisha yako hamna la maana utafanya; For kila ufanyalo yaani ule, ulale,
upate pesa, ukose pesa yaani ufanye lolote utataka kuhusisha na Nyota.
It is not healthy Mkuu, mambo ya nyota fanya for leisure but yasiongoze
kabisa maisha yako.... naamini kupoteza dira ya Maisha ni rahisi ukiendekeza...
Best of Luck....

Thanks for your advice man! Huwa siamini haya mambo thus why mwanzo nilitupa ile dawa! Let me try again and see!
 
chemsha maharage uyaweke uvunguni kwa wiki moja kisha chuja maji yake uyaoge..........

haswaaa na kuvuata wateja zaidi kwenye biashara akishakoga apake mchanganyiko wa mafuta ya mawese,samli na nyonyo. Nyota itang'aa 24/7
 
hili swali ni very ineresting......

je wewe unaamni dini gani?
je wewe ni muumini mzuuri wa dini yako?

spirtually uko strong ki vipi?
 
Salamu wanaJF, Mimi ni kijana wakiume, naombeni mnielimishe kuhusu nyota! Mtu akikwambia nyota yako haingai au inamatatizo inamaana gani? Kwa takribani miaka 3 sasa nimekuwa naplani nzuri za kimaisha, lakini cha ajabu naanza vizuri na baada ya muda si mrefu mambo yanaenda sivyo... Kila biashara ninayofanya napata hasara au nathulumiwa, nikimkopea mtu hela harudishi... Pesa ninazo dai watu inafika karibu mil. 4.
Nilisha ulizia kwa mtaamu mmoja kuhusu swala hili.... Alinipa dawa ya kuongea lakini nilipuzia na kuitupa mbali nikajifanya kumwomba mungu! Swala hili linanimiza kichwa sana, kwa muda wa miezi 2 nimekuwa nachukiwa na karibu marafiki wangu wote, hata mpenzi wangu hataki tena kuwasiliana tena na mimi japo ninamsomesha shule! Jamani naombeni ushauri wenu. Nyota yangu haingai? Nifanye nini? Au niende tena kwa wataamu wa nyota? Kama ndio wapi nitampata wa ukweli? Asante!

You just need some life coaching and good mentoring and you'll be straight.
 
Devil is a liar...ameanza kupandikiza mawazo ya nyota moyoni mwako, ulishawishika ukaenda kwa binadamu akakupe mafanikio....lakini roho wa Mungu alikuwa nawe akakutia hofu ya Mungu ukatupa hayo matakataka.....unapaswa kujua kuwa mafanikio huja kwa kuweka mipango madhubuti, kutenda kwa bidii huku ukimtanguliza Mungu. Achana na mambo ya kuangaliwa nyota cuz huko ndipo atapokea mapepo ya umaskini na utapumbazwa na kupofuliwa to the extent unaweza kuja kuishia kuwa muuaji. WANAOUA ALBINO, WANAOUA AU KULALA NA MAMA ZAO AU DADA NA KAKA ZAO WA DAMU WALIANZA HIVI HIVI. Unatakiwa ujue kuwa hata maandiko matakatifu (bible) inasema alaanhwe yule amtegemeae mwanadamu...so acha kuisaka laana....unatakiwa uwe na imani kuwa ili mafanikio yaje lazima upitie ktk magumu na machungu flani ktk lyf na MARA ZOTE UNAPOELEKEA KUFANIKIWA NDIPO SHETANI HUINUKA KUYAVURUGA MAMBO YAKO, UKITETEREKA TU, BARAKA ZAKO NA MAFANIKIO YAKO YANAPITA PEMBENI UNABAKIA ULIPOKUWA....UNAMPA SHETANI USHINDI...so muombe sana Mungu.
 
Kafanyiwe maombi ndugu..... achana na hayo mambo ya nyota, weka imani yako kwa Yesu atakufanikisha. He never let people down.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom