kahtaan
JF-Expert Member
- Jul 11, 2009
- 18,705
- 11,273
Lakini paul kasema neno juu ya msalaba kuwa wajinga wanaona msalaba kwao hauna maana wanasahau kwamba kwa msalaba huo huo tumeokolewa...! Ivi unadhani yesu hakujua kuwa mitume watakufa? Au ulidhani alijua baada ya vifo vya mitume injili ilishia pale? Au unahisi Mungu hatendi makuuu tangu enzi za Adam mpaka sasa huku akijidhirisha kwa watu wake kwa namna aonavyo inafaa? Wewe sawa na wale wap..umbafu ambao paul anasema hujisemea moyobi kuwa hakuna Mungu. Mwisho ujue msalaba wa kristo haupo km kujumlisha ila wa mpinga kristo ndiyo kama kujumlisha...! Nakupa task moja usipodharau ifanye, simama wima tandaza mikono yako, sura au alama upatayo ndivyo msalaba wa kristo ulivyo. Barikiwa.
Teh teh teh!
Mkuu nimesimama na nimefanya ulivyosema yaani kidogo nisababishe ajali.
Duh! We mtu mbaya sana.
Sasa turudi kwenye somo.
Unasema msalaba umekuokoa!
Umekuokoa na nini! Au una maanisha DHAMBI?
Hebu jamani tokeni nje ya Box hata siku MOJA TU muuone ukweli.
Hivi kweli wewe na akili zako timamu kabisaa unakubali tena bila wsws kuwa MUNGU ALIMPENDA SAAAAANA MWANAWE WA PEKEE halafu AKAAMUA KUMTOA KAFARA YA KUUWAWA KIFO CHA LAANA ili wewe mwenye dhambi ZA KILA AINA ulizozifanya kwa ubinafsi wako AZIBEBE KIPENZI CHA MUNGU??
we kweli umefikiri hii kitu?
Kawaida ya BABA mwenye MAPENZI NA MWANAE huona NI BORA AUMIE YEYE KULIKO MWANAE sasa inakuwaje MUNGU MKUU afanye uovu wa namna hii?
Pili. Km Huyo mungu wako ana uwezo wote Kwanini ASIAMUE KUSAMEHE TU MPAKA MTU AFE MSALABANI?
Hii adhabu Alikuwa anataka KUMRIDHISHA NANI HASA??
Km ni Yeye MWENYEWE basi Ntakosea kusema lbd huyo mungu wako ana matatizo ya kichwa?
Na hebu tuone je! Biblia inasema nini kuhusu KUBEBA DHAMBI YA MTU MWINGINE??
BIBLIA INASEMA.
Mababa wasiuawe kwa ajili ya watoto wao, wala watoto wasiuwawe kwa ajili ya baba zao;- kila mtu na auawe kwa ajili ya dhambi yake mwenyewe.
Kumbukumbu 24.16
Hali kadhaalika tunasoma neno la Mungu katika kitabu cha Yeremia:
Siku zile, hawatasema tena, Baba za watu wamekula zabibu kali, na meno ya watoto wao yametiwa ganzi. Bali kila mtu atakufa kwa sababu ya uovu wake mwenyewe;- kila mtu alaye zabibu kali, meno yake yatatiwa ganzi.
Yeremia 31.29-30
-Tena Neno la Mungu linaendelea kusema katika kitabu cha Ezekieli kwa uwazi zaidi:
Lakini ninyi mwasema, Kwani yule mwana asiuchukue uovu wa baba yake?- Yule mwana atakapofanya yaliyo halali na haki, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, hakika ataishi.- Roho itendayo dhambi, ndiyo itayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe; haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake.
Ezekieli 18.19-20
Na ukitaka kuona kuwa HATA YESU MWENYEWE HAKUPENDA. KUSULUBIWA. Hebu sikiliza maneno yake Alipopata hisia kuwa kuna BIASHARA YA KIPIGANA MISUMARI MSALABANI.
MATHAYO 26:39
Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.-
SASA Yesu Anaaanguka kifudifudi na KUOMBA kwa Mungu kuwa AEPUSHWE NA ADHABU HIO.
Lkn Juu ya juhudi yoote hio ya MAOMBI huyo Babake Hakukubali na AKAAMUA BORA AKAFE TU.
Mkuu amka kabla mauti hayajakutwaa.
Karibu ktk HAKI. Karibu ktk ibada ya kweli.
Na karibu ktk mapenzi ya KWELI YA YESU.
Sio mapenzi ya kusulubiana mkuu.
Hio kitu sio mapenzi.
Hizo ni Chuki mbaya mno kwa YESU mtume wa MUNGU.