Nyimbo za maombolezo ziwe zile zinazotuimarisha badala ya kutukatisha tamaa

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,298
12,600
Tusiomboleze kama watu tusio na imani na MwenyeziMungu. Eti utasikia nyimbo MTU anaimba sasa tutakimbilia wapi, tutaishije bila yeye, tangulia tu na sisi sote tutakufa na tutaonana baadaye, kwanini Mungu umemchukua, tutafanyaje sasa, hatatokea mwingine kama wewe, nk.

Nyimbo hizi hazitufanyi tuwe imara badala yake zinatudhoofisha na kumkufuru Mungu. Zinatudumaza badala ya kutuimarisha tayari kwa kusonga mbele.

Tuimbe nyimbo za kumtakia heri huko aendako marehemu lakini sio za kutuogopesha, kutukatisha tamaa kuwa basi tumekwisha tena na kukufuru.

Wasanii wetu tunawapenda lakini taifa na familia zimeondokewa na watu wao muhimu kwa maelfu na maelfu kwa karne na karne lakini bado maisha yanaendelea hadi leo. Tuimbe nyimbo za kuwasifu na kuwaombea roho zao ziwekwe pahala pema peponi ingawa haitawasaidia sana kama kwenye uhai wao hawakuwatendea watu na mungu mazuri.
 
Msechu kawapa mrungula watu wengi humu kuupiga promo arudi kwenye trend
 
Ngoja nimsikilize MSECHU- UMETUACHA IMARA
hii ndizo kati ya nyimbo bora za maombolezo, hizi za nenda tu na sisi tunakuja ni za hovyo kabisa. Zinalegeza watu magoti washindwe kwenda mbele. Nyimbo kama hizo inafaa tukutane nazo kwenye mafundisho ya dini na nyimbo za ibada, sio kwenye misiba ya viongozi wetu wapendwa.
 
Msechu kawapa mrungula watu wengi humu kuupiga promo arudi kwenye trend
sio promo kafikiria nn aimbe. wengine wanakufuru Mungu. Tanzania ni kubwa kuliko mmoja wetu yeyote, na MwenyeziMungu ni muweza wa yote na Tanzania lazima isonge mbele.
 
Msechu kawapa mrungula watu wengi humu kuupiga promo arudi kwenye trend
Acha roho mbaya, Msechu ana pesa gani ya kuhonga? Mbona hata mimi nimemsifia humu akati hata hatufahamiani? Tujifunze kutoa pongezi kwa jambo zuri na kukosoa panapostahili.
 
Back
Top Bottom