Nyerere: Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole lakini ni kiongozi dhaifu; na upole wake na udhaifu wake unatumiwa vibaya...

Mhere Mwita

JF-Expert Member
Jan 24, 2012
235
1,275
Nimefuatilia sakata la CAG Prof Mussa Assad na spika wa Bunge Ndugai Juu ya Neno dhaifu nimeona spika Ndugai anatumiwa na Mafisadi ili kuziba hoja ya wizi wa pesa za wananchi.

Mfano mzuri Spika Ndugai hakuitaka serikali ituambie wananchi ni wapi ilipo Trillion 1.5 ambao ilikuwa ikafika trillion 2.4 mwaka 2016/2017 na Leo Imefika Trillioni 4. Ndugai hataki tujue Lugumi Enterprise amepiga Sh. 604 Milioni. #CAGReport ya Serikali Kuu Uk. 304:

Tshs 604,390,244 kwa kile kilichoelezwa ni mafunzo ya wataalamu 30 zimetolewa Serikalini kupitia Jeshi la Polisi na kupokelewa na Lugumi Enterprise lakini hakuna mafunzo yaliofanyika.

Kwenye Mamlaka ya Rufaa za koda kuna mashauri ambayo yana jumla ya Trillion 382.6 sawa na 1200% ya Bajeti ya Nchi kwa maana hiyo Ndugai anatengeneza Mgogoro ili ufichwe Uozo.

Kama neno Udhaifu ni tusi mbona mwalimu Nyerere alimuita Rais Mwinyi ni dhaifu ukiangalia kwenye kitabu cha Mwl Nyerere cha Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania cha Mwaka 1994 ukurasa wa 66 Mwl aliandika hivi Nanukuu "Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole lakini ni kiongozi dhaifu; na upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao sio wema" kwa hiyo Nyerere alimkashfu Rais Mwinyi.

Spika Ndugai Acha kutumika kuficha uozo neno dhaifu aliwezi kusababisha pesa za walipa kodi zipotee, sisi watanzania tunataka kujua pesa zetu ziko wapi.
FB_IMG_1555411058301.jpeg
IMG_20190416_141921.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
"Rais Mwinyi ni mtu mwema na mpole lakini ni kiongozi dhaifu; na upole wake na udhaifu wake unatumiwa na watu ambao sio wema

FB_IMG_1555412148359.jpg
"

Mwl Nyerere Katika Kitabu cha Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania. (1994) Haya maneno angesema leo kwa hawa miungu watu angeitwa kamati ya maadili
 
Tatizo la kutokua na Elimu bora na kukulia katika umasikini na ukapata vyeo inakua shida tuu kwa walio chini yako ni kuwanyanyasa tuu kila kukicha wakujue wewe nani na pia kuwaonea wivu waliokuzidi Elimu na ufahamu...
 
Kwa upande wangu niungane na maandiko ya baba wa Taifa letu,kuwa udhaifu si tusi,ni neno linaloelezea mapungufu ambayo yapo kwa binadamu na mapungufu hayo kikawaida yanaweza rekebishika.

Kwa swala hili la CAG na Bunge yawezekana kuna Zaidi ya hiki tunachokisikia,kwani imekuwa si kawaida kwa neno dhaifu kuchukuliwa kwa uzito mkubwa kuliko mabilioni ya pesa ambayo yameripotiwa ktk report ya CAG.
 
Kuna wakati haitakiwi kujisifu kuwa una mbio wasifu na wanaokukimbiza basi.

Awamu hii kuna watu wachache ila wanakimbiza hatare.

Kiasi kwamba unakuta Watu wanacheza sindimba ambalo hawakutaka hata kulicheza.

Maisha haya yanae changamoto ati!!!
 
Nimepitia kitabu kilichotungwa na Mwalimu Julius Kambalage Nyerere na nukuu baadhi ya kilochomo ndani ya kitabu ktk ukurasa wa 51 mimi nilitoa copy.


Anaanza " Raisi Mwinyi ni mtu mwema na mpole, lakini ni kiongozi DHAIFU, na upole wake na UDHAIFU wake unatumiwa na watu ambao wala si wema wala wapole kuhatarisha umoja na amani ya nchi yetu.

Anaendelea

Ndiyo maana naamini kuwa wananchi wote wenye nia njema tuna wajibu wa kusaidiana kukimaliza kipindi hiki cha mpito. Pamoja na makosa na UDHAIFU wake wote Raisi Mwinyi ana haki ya kusaidiwa amalize kwa amani kipindi chake kilichobakia

Naishia hapo, binafsi naona yule ambae anaona MADHAIFU yako na akakwambia huyo anakutakia mema maana kuna mtu anataka kutumia MADHAIFU ya spika kufanikisha mipango yake.

Binafisi naona CAG alikuwa sahihi sana kukumbusha bunge letu kuwa makini toka kwenye UDHAIFU ili kutojenga Taifa legelege.

Mwalimu Nyerere aliona MADHAIFU ya Mzee Mwinyi na akasimama nae nafikir spika anatakiwa kupitia huko UDHAIFU si tusi
 
Sidhani kama huwa wanakisoma kile kijitabu
Inaonekana kinae maarifa kwaajili ya watawala wa zama hizi

Kusoma ni tabia

Kweli mkuu kuna kurasa hapa inazungumzia democrasia na yanayotendekea nchi hii ni aibu
 
Hapa mwalimu anazungumzia democrasia nchini

Nilisema mwanzo kwamba kansa ya uongozi ndani ya chama cha mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona chama kizur cha upinzani kinachoweza kuiongoza Nchi yetu badala ya ccm.

Ubovu wa uongozi ndani ya ccm ndio uliofanya napendekeze uwepo wa vyama vingi vya siasa

Hapa leo tunaona Raisi Magufuli anapambana na vyama vya upinzani tena hadharani wa kushirikiana na jeshi la polisi ajabu hii

Wawe wanasoma vitabu vya wakuu wao wa chama
 
Back
Top Bottom