Nyerere Hakuwa na mapungufu, alikuwa Kiongozi Mbovu!

Humu ndani, kuna watu wakiona Hayati Julius Nyerere, the First Preisdent wa URT anasemwa vibaya basi wanakuja juu!! Kinachonikera mimi, ni wengi wao kuhusisha na imani za dini! Kwamba, mtu akisema ubaya wa Nyerere, na hasa mtu huyo akihisiwa ni Mwislamu, basi hoja ya wapofu wa hoja watachukulia ukosoaji huo ni chuki ya waislamu dhidi ya Nyerere!! Hivi ni lini Waislamu wamepata kuwa na chuki na mwalimu?! Sasa haya mambo kwamba mtu akitaja mabovu ya Mwalimu basi ni chuki za waislamu dhidi ya mwalimu yanatoka wapi?! Binafsi, am muslim, na kama utaniambia nikutajie my favorite president sitasita kumtaja Julius Nyerere. lakini pamoja na yote hayo, kama nitaambiwa nitaje top two poorest presidents ever happaned in our history, basi Nyerere ni mmoja wapo, akiwa sambamba na mwinyi! Binafsi, nikimwangalia Nyerere, ni eneo moja peke yake ambalo linaweza kumweka kama best leader! hakuwa corrupt leader ingawaje serikali yake ilikuwa very corrupt government!! Na wala si kweli kwamba Nyerere alikuwa mkali kwa corrupt leaders, vinginevyo nchi hii Mwinyi asingeikuta alipoikuta! Sana sana ki2 ambacho labda Nyerere aliweza kuzuia ni kutokuwa na State House corrupt leaders...lakini ukitoka hapo, wengi walikuwa corrupts!

Serikali ya Nyerere ilijaa watendaji ambao walikosa kabisa uwajibikaji na ndio maana Mwinyi alikuja na kitu kilichojulikana kama Fagio La Chuma! Kwanini awe na fagi la chuma wakati uwajibikaji ulikuwapo?! Serikali isiyo corrupt, haiwezi kuwa na irresponsible leaders. Ni kweli, Nyerere hakuwa corrupt leader, lakini aliendesha corrupt government na anayebisha aniambie kwanini viwanda vyote vilifia mikononi mwake!!

Ni kweli JK ni goi goi! hata Nyerere alikuwa ni goi goi kupita kiasi!! hakuwa mkali kama tunavyoaminishwa watu ambao hatukuwa na ufahamu wakati wa utawala wake. Nyerer alikuwa mkali kwa wapinzani wake wa kisiasa, and not otherwise!! Kama alikuwa mkali kweli, umasikini tulionao ulitokea wapi?! Aliwafanya nini waliokuwa wanaharibu mali za umma zaidi ya kuwahamisha?! kama sio ugoi goi tuite nini hii?!

Kulikuwa na miradi kadhaa ambayo ilianzishwa wakati wa utawala wake, na vilevile ilikufa hata kabla haijafika kokote....sasa kama sio ubadhirifu huo tuite nini?! Siwezi kumsifia kiongozi aliye msafi yeye pekee na familia yake wakati serikali yake imejaa watu irresponsible!!

Amekaa Ikulu more than 20 years lakini ametoka akiwa ameachwa barabara zimejaa mahandaki kila mahali!! Bahati mbaya sana, sehemu ambazo zilikuwa na corrupt leaders toka kwenye serikali yake ndio sehemu pekee ambazo angalau zilikuwa na barabara nzuri kidogo! Sehemu ambazo walitoka honest leaders kama yeye, ndizo zikabaki balaa tupu!!! Hiyo ndio sababu kuu iliyofanya mikoa ya kusini kuwa hoe hae zaidi kwani viongozi wake wengi walikuwa honest kama yeye...hawa ni pamoja na akina Kawawa na Nnauye! Hivyo, umaskini wa kusini haukusababishwa na Nyerere kama Nyerere, bali ulisababishwa na irresponsible central government ambayo ugawaji wa keki ya taifa haukuwa the same! ilitegemea sana sehemu husika ana power gani serikalini and how corrupt s/he is!!!

Nyerere ameondoka akiwa ameacha vyuo vikuu viwili tu, UDSM na SUA na kuishia tu ktk kujenga vyuo vya kati ambavyo hata hivyo navyo productivity yake ilikuwa chini. Chuo pekee cha kati ambacho kilikuwa kinatoa elimu ya maana labda ni Mzumbe peke yake....na sababu kuu ni kwavile kilikuwa more political! Tena hata nina mashaka kama kweli kilikuwa kinatoa elimu ya maana!! tangu lini katibu wa nini sijui mwenye miaka 45++ akaweza kuhimili mikiki mikiki ya elimu ya juu?! Tunaambiwa enzi zake elimu ilikuwa na ubora kuliko sasa!! na hii ndio tabia ya wazee....kwamba kila ki2 chao kilikuwa bora!!! Huo ubora ulisaidia nini basi katika kutatua matatizo ya uchumi wa nchi hii?! Sana sana hao tunaoambiwa walikuwa wasomi wakati wa elimu bora ndio hao hao waliogeuka kuwa corrupts wasio na haya wakati wa Mwinyi.....bisheni!!! Kama ni kweli wakati huo elimu ilikuwa bora basi vilevile ilisaidia kuzalisha BEST CORRUPT LEADERS!!! Serkali corrupt haiwezi kuwa na jeuri ya kujenga vyuo vikuu vya kutiosha kwavile haina fedha.....kutokuwa na fedha ni dalili ya serikali corrupt!!!
MATATIZO ya umeme tuliyonayo hivi sasa source yake ilikuwa enzi za mwalimu!!! Serikali ya Mwalimu haiku-forecast mahitaji ya umeme over the next 50 years!! Ni kweli, wakati wa Nyerere, haukuwa wa mgao! Sasa mgao ungetoka wapi wakati nyumba zenyewe za umeme zilikuwa chache?! Mgao ungetoka wapi wakati hakukuwa na uzalishaji mkubwa wa kuhitaji matumizi ya umeme?! Mgao ungetoka wapi wakati hata kumiliki radio ilikuwa ni anasa?! Kwahiyo, si kwamba ni uongozi bora wa Nyerere ambao ulifanya nchi isiwe na mgao/upungufu wa umeme, bali hiyo ilikuwa ni matokeo ya serikali mbovu!

Tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Huduma gani za jamii?! hizo za kufuata zahanati kilometa 50 na shule ya msingi kilometa 10?! Dar es salaam yote hii aliacha shule saba tu za sekondari (za serikali, ambazo hata hivyo hakujenga yeye)-Jangwani, Azania, Tambaza, Forodhani, Kisutu na Kibasila!!! Nani atakayethubutu kusema kwamba shule hizo zilikuwa zinakidhi mahitaji ya elimu ya sekondari jijini? Huko mikoani ndo ilikuwa balaa tupu, unaweza kukuta mkoa mzima una shule moja au mbili za serkali.....bado tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Ni serikali gani ingeshindwa kuhudumia shule chache kama hizo?!

Ubovu wa serikali ya Nyerere ni mwingi kuliko uzuri wake, otherwise, wale wanaoona kwamba mgtu akisema basi ana chuki za kidini (styupid thinking) basi anitajie hapa mazuri yaliyofanywa na serikali yake ambayo natarajia yawe mengi kuliko mabovu!

wapo watakaosema kwamba Nyerere amewezesha nchi hii kuwa na amani! Kwani aliichukuwa wakati nchi haina amani?! Sifa kama hizo anatastahili kupewa Kagame aliyechukua nchi baada ya mauaji ya kutisha nchini mwake! Anyway, waliosoma historia wanisaidie kunitajia ni vita gani vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimepata kupiganwa Tanganyika katika karne ya 19! Kama hakuna au zilikuwa si za kutisha sana, basi inawezekana Watanganyika hatuna silika ya kupigana tangu zama hizo!!

Hivyo basi, mtu anavyotaja ubovu wa Nyerere inakuwa ni ujinga uliepitiliza kusema kwamba ni chuki binafsi...Na inakuwa sio ujinga, bali ni upumbavu mtu akisema ni chuki za kidini! Nyerere kama Nyerere alikuwa was a very good person BUT NOT A GOOD LEADER! He was a good person who was a poor leader! Kutokana na hayo, sipati kigumumizi hata chembe kusema wazi kwamba SI KWAMBA NYERERE ALIKUWA NA MAPUNGUFU, BALI ALIKUWA KIONGOZI MBOVU! Ukweli wenyewe ndio huo, ukiona mgumu kuumeza, chukua maji ushushie!

Anayekataa, atoe data za mazuri yake kama kiongozi yenyewe manufaa kwa Tanzania!


Hakuna cha maana mnachotafuta zaidi ya kutafuta mchawi wa maovu yenye! Mnatafuta sababu ya kushidwa kwenu! Kama suala ni Nyerere alikwisha sema nakuwa malaika na mlitakiwa kuendeleza misingi na mambo mazuri aliyoyafanya na kuyaacha mabaya. Lakini msululu wote wa maraisi mmeishia kumlaumu bila kufanya la maana kwa watanzania zaidi ya kuuza nchi kwa wageni na kuturudisha katika utumwa. Ni kituko kuona hakuna mwananchi anayeweza kuwekeza katika nchi yake zaidi ya ninyi viongozi mliogeuka wajasiriamali na wageni kwa kigezo cha uwekezaji
 
hakuna cha maana mnachotafuta zaidi ya kutafuta mchawi wa maovu yenye! Mnatafuta sababu ya kushidwa kwenu! Kama suala ni nyerere alikwisha sema nakuwa malaika na mlitakiwa kuendeleza misingi na mambo mazuri aliyoyafanya na kuyaacha mabaya. Lakini msululu wote wa maraisi mmeishia kumlaumu bila kufanya la maana kwa watanzania zaidi ya kuuza nchi kwa wageni na kuturudisha katika utumwa. Ni kituko kuona hakuna mwananchi anayeweza kuwekeza katika nchi yake zaidi ya ninyi viongozi mliogeuka wajasiriamali na wageni kwa kigezo cha uwekezaji
excellent contribution!
 
Ninaweza kusema kwaujasiri kabisa kwamba wewe una miaka si zaidi ya 16, hujawahi kumuona nyerere akiwa hai, humjui,humfahamu wala hujawahi kuona tanzania kabla ya mwaka 1998. Huijui historia ya tanzania, na kama umewahi kuisoma umechagua kuto kuitilia maanani, hivyo hufahamu tumetoka wapi, tumepitia wapi na hata sasa tuko wapi.

Ninaweza kusema kwa ujasiri kabisa kuwa wewe simsomaji wa vitabu. Na hujawahi kusoma kitabu chochote chenyekuelezea habari ya tanganyika na uhuru wake, siasa ya ujamaa na kujitegemea, azimio la arusha, vita ya kagera, viwanda na uzalishaji tanzania wala hujui chochote kuhusu national policy za tanzania kipindi hicho wala sasa.

Nitasema tena na kwa ujasiri mkubwa, kwamba si tu kwamba wewe una umri mdogo sana kumzungumzia nyerere kama vile unamfahamu, wewe pia simfuatiliaji hata wa mambo ya sasa, current affairs za taifa hili katika nyanja zote za uchumi na hata siasa huzifahamu., kwamfano, hujui Tanzania Vision 2025 nini nini na inavitu gani. hujui NSGRP ni nini na ina clusters gani. Hufahamu kabisa hata policy zakawaida kabisa kama KILIMO KWANZA nikitu gani zina malengo gani na zinatekelezekaje? hujui hata habari za uchumi wa kimataifa wa sasa kama kwamfano MDG's nivitu gani na targets zake ni zipi huzijui., wala hufuatilii., ninasema hivi kwasababu hata argument yako ni shaky na imejengwa juu ya msingi usio informed vyakutosha.

lakini umesukumwa na mihemuko tu na kuja kuandika vitu usivyo vifahamu hapa!

lakini niwieradhi, kama unaumri mkubwa zaidi ya miaka kumi na sita, na kama umewahi kumuona mw. nyerere akiwa hai, na kama ulikuwepo tanzania kabla ya 1998, na kama umewahi kusoma habari za azimio la arusha na siasa ya ujamaa na kujitegemea na kama umewahi kujua kuhusu vita vya kagera na kama unajua kuhusu viwanda na uzalishaji wa tanzania kipindi kile., nabado ukaya andika haya uliyo yaandika., niwieradhi kwa kukudhania haya yote! kwakua umeandika kama mtoto wa miaka kumi na sita anaye mzungumzia nyerere asiye mjua!!

ninachoweza kukuambia tu ndugu yangu nikwamba tanzania hii imetoka mbali sana, na chochote unachokiona kipo sasa hivi ni matokeo ya misingi iliyo wekwa ya utaifa hapo mwanzo.

natambua yako madhaifu ya uongozi wa kipindikile pia lakini lazima unapotaka kutathmini na ku comment juu ya ufanyaji kazi wa mtu flani wakati flani, Ni muhimu ku take into consideration mazingira ya wakati huo.

Kwa haya mengi niliyo sema, Ninaomba kutokubaliana na wewe kwa sehemu kubwa, hasa pale uliposema uongozi wa nyerere ulikua corrupt, hatakama yeye hakuwa korupt, na kwamba eti hakuwa mkali kwa viongozi iresponsible, tena viwanda vilikufa mikononi mwake., ninasisitiza tena ni muhimu kuangalia mazingira ya wakati ule kabla huja nyoosha kidole ku criticise mtu kwa kitu chochote.
nevertheless, sisemi nyerere alikua malaika!
comrade,
niwieradhi.
 
Ni moja ya hoja chakavu kabisa kupata kutolewa kwenye mada hii!! Udini upo wapi? Niliyosema ambayo si kweli ni yapi? Aliyekuambia kwamba shule zote ambazo alitaifisha zilikuwa ni za Mission(bila shaka ukitaka kumaanisha za Kikristo) ni nani? Jadili hoja badala ya kuleta hoja zisizo na maana.
Ukweli woyte unaeleweka haya kama hautausema!!!!!!!!!!!!!
 
Ninaweza kusema kwaujasiri kabisa kwamba wewe una miaka si zaidi ya 16, hujawahi kumuona nyerere akiwa hai, humjui,humfahamu wala hujawahi kuona tanzania kabla ya mwaka 1998. Huijui historia ya tanzania, na kama umewahi kuisoma umechagua kuto kuitilia maanani, hivyo hufahamu tumetoka wapi, tumepitia wapi na hata sasa tuko wapi.

Ninaweza kusema kwa ujasiri kabisa kuwa wewe simsomaji wa vitabu. Na hujawahi kusoma kitabu chochote chenyekuelezea habari ya tanganyika na uhuru wake, siasa ya ujamaa na kujitegemea, azimio la arusha, vita ya kagera, viwanda na uzalishaji tanzania wala hujui chochote kuhusu national policy za tanzania kipindi hicho wala sasa.

Nitasema tena na kwa ujasiri mkubwa, kwamba si tu kwamba wewe una umri mdogo sana kumzungumzia nyerere kama vile unamfahamu, wewe pia simfuatiliaji hata wa mambo ya sasa, current affairs za taifa hili katika nyanja zote za uchumi na hata siasa huzifahamu., kwamfano, hujui Tanzania Vision 2025 nini nini na inavitu gani. hujui NSGRP ni nini na ina clusters gani. Hufahamu kabisa hata policy zakawaida kabisa kama KILIMO KWANZA nikitu gani zina malengo gani na zinatekelezekaje? hujui hata habari za uchumi wa kimataifa wa sasa kama kwamfano MDG's nivitu gani na targets zake ni zipi huzijui., wala hufuatilii., ninasema hivi kwasababu hata argument yako ni shaky na imejengwa juu ya msingi usio informed vyakutosha.

lakini umesukumwa na mihemuko tu na kuja kuandika vitu usivyo vifahamu hapa!

lakini niwieradhi, kama unaumri mkubwa zaidi ya miaka kumi na sita, na kama umewahi kumuona mw. nyerere akiwa hai, na kama ulikuwepo tanzania kabla ya 1998, na kama umewahi kusoma habari za azimio la arusha na siasa ya ujamaa na kujitegemea na kama umewahi kujua kuhusu vita vya kagera na kama unajua kuhusu viwanda na uzalishaji wa tanzania kipindi kile., nabado ukaya andika haya uliyo yaandika., niwieradhi kwa kukudhania haya yote! kwakua umeandika kama mtoto wa miaka kumi na sita anaye mzungumzia nyerere asiye mjua!!

ninachoweza kukuambia tu ndugu yangu nikwamba tanzania hii imetoka mbali sana, na chochote unachokiona kipo sasa hivi ni matokeo ya misingi iliyo wekwa ya utaifa hapo mwanzo.

natambua yako madhaifu ya uongozi wa kipindikile pia lakini lazima unapotaka kutathmini na ku comment juu ya ufanyaji kazi wa mtu flani wakati flani, Ni muhimu ku take into consideration mazingira ya wakati huo.

Kwa haya mengi niliyo sema, Ninaomba kutokubaliana na wewe kwa sehemu kubwa, hasa pale uliposema uongozi wa nyerere ulikua corrupt, hatakama yeye hakuwa korupt, na kwamba eti hakuwa mkali kwa viongozi iresponsible, tena viwanda vilikufa mikononi mwake., ninasisitiza tena ni muhimu kuangalia mazingira ya wakati ule kabla huja nyoosha kidole ku criticise mtu kwa kitu chochote.
nevertheless, sisemi nyerere alikua malaika!
comrade,
niwieradhi.

Haya maelezo mazuri sana, jamani kwa nini wenye habari na takwimu za ktosha wasiandike historia hii inayotakas kupotoshwa na watu wachache??? Wasiwasi wangu kwa kizazi kinachokuja kikili
shwa sumu ya hawa watu wachache wanaweza kuamnini. Nyerere alikuwa si mtu wa kujikweza,nilikwenda Makumbusho Butiama na kusoma tuzo mbalimbali alizopata na maelezo yake nililia sana kwa mara nyingine. Mengi hayafahamiki wala mwenyewe hakuhitaji kuyatangaza.
 
nyerere alikuwa kiongozi bora kabisa miongoni mwa viongozi wa afrika na hadi sasa,mapungufu kama walivyo binadamu wengine alikuwa nayo na mapungufu makubwa kabisa aliyokuwa nayo ni KUFIKIRI KUWA YEYE NDIYE MWENYE AKILI NA WENGINE WOOOTE NI WAJINGA mpaka akaitwa HAAMBILIKI
 
The failure of socialism economic policies can be explained as the root cause of the poverty in Tanzania.
 
huwezi sema eti baada ya miaka 50 nchi ya tatu duniani kwa kuomba omba na umasikini
na yeye Nyerere alitawala nusu ya miaka hiyo 50 halafu useme Nyerere was the best leader Afrika

that is insult to people with brain........

Acha kujisahaulisha kwamba KIZURI kilichoandaliwa kwa miaka 20 ya Nyerere kinaweza KUHARIBIWA kwa miaka 5 tu ya mrithi wake! Hastahili lawama kwa kutawala 24 yrs na leo hali bado ni hii. Mwenyewe alisema nanukuu "Mazuri yetu mnayapuuza bali ya KIJINGA ndio mnayaendeleza"
 
Sh____i type,mtakufa na udini wenu,wanafki nyie.
Nyerere amefanya mazuri mengi sana,kulko hao maghaidi wenzenu!!
 
HII DHAMBI ITAWATAFUNA MPAKA "MFUPA" WENU WA MWISHO, YA BILA KUJUA NINI NA NANI CHANZO NA WAPI TATIZO.??

Pumzika kwa Amani mwalimu.!!!!!!!!
 
Ninaweza kusema kwaujasiri kabisa kwamba wewe una miaka si zaidi ya 16, hujawahi kumuona nyerere akiwa hai, humjui,humfahamu wala hujawahi kuona tanzania kabla ya mwaka 1998. Huijui historia ya tanzania, na kama umewahi kuisoma umechagua kuto kuitilia maanani, hivyo hufahamu tumetoka wapi, tumepitia wapi na hata sasa tuko wapi.

Ninaweza kusema kwa ujasiri kabisa kuwa wewe simsomaji wa vitabu. Na hujawahi kusoma kitabu chochote chenyekuelezea habari ya tanganyika na uhuru wake, siasa ya ujamaa na kujitegemea, azimio la arusha, vita ya kagera, viwanda na uzalishaji tanzania wala hujui chochote kuhusu national policy za tanzania kipindi hicho wala sasa.

Nitasema tena na kwa ujasiri mkubwa, kwamba si tu kwamba wewe una umri mdogo sana kumzungumzia nyerere kama vile unamfahamu, wewe pia simfuatiliaji hata wa mambo ya sasa, current affairs za taifa hili katika nyanja zote za uchumi na hata siasa huzifahamu., kwamfano, hujui Tanzania Vision 2025 nini nini na inavitu gani. hujui NSGRP ni nini na ina clusters gani. Hufahamu kabisa hata policy zakawaida kabisa kama KILIMO KWANZA nikitu gani zina malengo gani na zinatekelezekaje? hujui hata habari za uchumi wa kimataifa wa sasa kama kwamfano MDG's nivitu gani na targets zake ni zipi huzijui., wala hufuatilii., ninasema hivi kwasababu hata argument yako ni shaky na imejengwa juu ya msingi usio informed vyakutosha.

lakini umesukumwa na mihemuko tu na kuja kuandika vitu usivyo vifahamu hapa!

lakini niwieradhi, kama unaumri mkubwa zaidi ya miaka kumi na sita, na kama umewahi kumuona mw. nyerere akiwa hai, na kama ulikuwepo tanzania kabla ya 1998, na kama umewahi kusoma habari za azimio la arusha na siasa ya ujamaa na kujitegemea na kama umewahi kujua kuhusu vita vya kagera na kama unajua kuhusu viwanda na uzalishaji wa tanzania kipindi kile., nabado ukaya andika haya uliyo yaandika., niwieradhi kwa kukudhania haya yote! kwakua umeandika kama mtoto wa miaka kumi na sita anaye mzungumzia nyerere asiye mjua!!

ninachoweza kukuambia tu ndugu yangu nikwamba tanzania hii imetoka mbali sana, na chochote unachokiona kipo sasa hivi ni matokeo ya misingi iliyo wekwa ya utaifa hapo mwanzo.

natambua yako madhaifu ya uongozi wa kipindikile pia lakini lazima unapotaka kutathmini na ku comment juu ya ufanyaji kazi wa mtu flani wakati flani, Ni muhimu ku take into consideration mazingira ya wakati huo.

Kwa haya mengi niliyo sema, Ninaomba kutokubaliana na wewe kwa sehemu kubwa, hasa pale uliposema uongozi wa nyerere ulikua corrupt, hatakama yeye hakuwa korupt, na kwamba eti hakuwa mkali kwa viongozi iresponsible, tena viwanda vilikufa mikononi mwake., ninasisitiza tena ni muhimu kuangalia mazingira ya wakati ule kabla huja nyoosha kidole ku criticise mtu kwa kitu chochote.
nevertheless, sisemi nyerere alikua malaika!
comrade,
niwieradhi.
Kuna watu wa kuombwa radhi katika maisha, ila katu husijethubutu kwa watu wenye mawazo na fikra mgando mithili ya JIBINI!!
 
Ebu mwacheni mzee wa watu hapumzike kwa amani jaman...inaelekea hamna kaz za kufanya eh,si bora mchukue mifagio mkafagie barabara za jiji letu la dar liwe saf,,pamba..fu..
 
kama ungelikuwepo enzi hizo za kubadilishana chumvi kwa maharagwe/mahindi lita moja vibiliti vinne/kuku moja vikaptula viwili na watu kuhama hama ktk makazi zaidi ya mara tatu(sogeza)usingelisema juu ya mapungufu ya mwl nyerere maana eneo kubwa la nchi likuwa nipoli na mapito ya wanyama.Sasa kuweka watu pamoja na kubolesha uchumi wa nchi sikazi ndogo. rest in peace mwl jk nyerere.
 
Jinga na janga jipya kwa taifa ndo wewe,utatumia nguvu nyingi sana,kumjadili nyerere lakini utaishia kuumbuka mwenyewe
 
Humu ndani, kuna watu wakiona Hayati Julius Nyerere, the First Preisdent wa URT anasemwa vibaya basi wanakuja juu!! Kinachonikera mimi, ni wengi wao kuhusisha na imani za dini! Kwamba, mtu akisema ubaya wa Nyerere, na hasa mtu huyo akihisiwa ni Mwislamu, basi hoja ya wapofu wa hoja watachukulia ukosoaji huo ni chuki ya waislamu dhidi ya Nyerere!! Hivi ni lini Waislamu wamepata kuwa na chuki na mwalimu?! Sasa haya mambo kwamba mtu akitaja mabovu ya Mwalimu basi ni chuki za waislamu dhidi ya mwalimu yanatoka wapi?! Binafsi, am muslim, na kama utaniambia nikutajie my favorite president sitasita kumtaja Julius Nyerere. lakini pamoja na yote hayo, kama nitaambiwa nitaje top two poorest presidents ever happaned in our history, basi Nyerere ni mmoja wapo, akiwa sambamba na mwinyi! Binafsi, nikimwangalia Nyerere, ni eneo moja peke yake ambalo linaweza kumweka kama best leader! hakuwa corrupt leader ingawaje serikali yake ilikuwa very corrupt government!! Na wala si kweli kwamba Nyerere alikuwa mkali kwa corrupt leaders, vinginevyo nchi hii Mwinyi asingeikuta alipoikuta! Sana sana ki2 ambacho labda Nyerere aliweza kuzuia ni kutokuwa na State House corrupt leaders...lakini ukitoka hapo, wengi walikuwa corrupts!

Serikali ya Nyerere ilijaa watendaji ambao walikosa kabisa uwajibikaji na ndio maana Mwinyi alikuja na kitu kilichojulikana kama Fagio La Chuma! Kwanini awe na fagi la chuma wakati uwajibikaji ulikuwapo?! Serikali isiyo corrupt, haiwezi kuwa na irresponsible leaders. Ni kweli, Nyerere hakuwa corrupt leader, lakini aliendesha corrupt government na anayebisha aniambie kwanini viwanda vyote vilifia mikononi mwake!!

Ni kweli JK ni goi goi! hata Nyerere alikuwa ni goi goi kupita kiasi!! hakuwa mkali kama tunavyoaminishwa watu ambao hatukuwa na ufahamu wakati wa utawala wake. Nyerer alikuwa mkali kwa wapinzani wake wa kisiasa, and not otherwise!! Kama alikuwa mkali kweli, umasikini tulionao ulitokea wapi?! Aliwafanya nini waliokuwa wanaharibu mali za umma zaidi ya kuwahamisha?! kama sio ugoi goi tuite nini hii?!

Kulikuwa na miradi kadhaa ambayo ilianzishwa wakati wa utawala wake, na vilevile ilikufa hata kabla haijafika kokote....sasa kama sio ubadhirifu huo tuite nini?! Siwezi kumsifia kiongozi aliye msafi yeye pekee na familia yake wakati serikali yake imejaa watu irresponsible!!

Amekaa Ikulu more than 20 years lakini ametoka akiwa ameachwa barabara zimejaa mahandaki kila mahali!! Bahati mbaya sana, sehemu ambazo zilikuwa na corrupt leaders toka kwenye serikali yake ndio sehemu pekee ambazo angalau zilikuwa na barabara nzuri kidogo! Sehemu ambazo walitoka honest leaders kama yeye, ndizo zikabaki balaa tupu!!! Hiyo ndio sababu kuu iliyofanya mikoa ya kusini kuwa hoe hae zaidi kwani viongozi wake wengi walikuwa honest kama yeye...hawa ni pamoja na akina Kawawa na Nnauye! Hivyo, umaskini wa kusini haukusababishwa na Nyerere kama Nyerere, bali ulisababishwa na irresponsible central government ambayo ugawaji wa keki ya taifa haukuwa the same! ilitegemea sana sehemu husika ana power gani serikalini and how corrupt s/he is!!!

Nyerere ameondoka akiwa ameacha vyuo vikuu viwili tu, UDSM na SUA na kuishia tu ktk kujenga vyuo vya kati ambavyo hata hivyo navyo productivity yake ilikuwa chini. Chuo pekee cha kati ambacho kilikuwa kinatoa elimu ya maana labda ni Mzumbe peke yake....na sababu kuu ni kwavile kilikuwa more political! Tena hata nina mashaka kama kweli kilikuwa kinatoa elimu ya maana!! tangu lini katibu wa nini sijui mwenye miaka 45++ akaweza kuhimili mikiki mikiki ya elimu ya juu?! Tunaambiwa enzi zake elimu ilikuwa na ubora kuliko sasa!! na hii ndio tabia ya wazee....kwamba kila ki2 chao kilikuwa bora!!! Huo ubora ulisaidia nini basi katika kutatua matatizo ya uchumi wa nchi hii?! Sana sana hao tunaoambiwa walikuwa wasomi wakati wa elimu bora ndio hao hao waliogeuka kuwa corrupts wasio na haya wakati wa Mwinyi.....bisheni!!! Kama ni kweli wakati huo elimu ilikuwa bora basi vilevile ilisaidia kuzalisha BEST CORRUPT LEADERS!!! Serkali corrupt haiwezi kuwa na jeuri ya kujenga vyuo vikuu vya kutiosha kwavile haina fedha.....kutokuwa na fedha ni dalili ya serikali corrupt!!!
MATATIZO ya umeme tuliyonayo hivi sasa source yake ilikuwa enzi za mwalimu!!! Serikali ya Mwalimu haiku-forecast mahitaji ya umeme over the next 50 years!! Ni kweli, wakati wa Nyerere, haukuwa wa mgao! Sasa mgao ungetoka wapi wakati nyumba zenyewe za umeme zilikuwa chache?! Mgao ungetoka wapi wakati hakukuwa na uzalishaji mkubwa wa kuhitaji matumizi ya umeme?! Mgao ungetoka wapi wakati hata kumiliki radio ilikuwa ni anasa?! Kwahiyo, si kwamba ni uongozi bora wa Nyerere ambao ulifanya nchi isiwe na mgao/upungufu wa umeme, bali hiyo ilikuwa ni matokeo ya serikali mbovu!

Tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Huduma gani za jamii?! hizo za kufuata zahanati kilometa 50 na shule ya msingi kilometa 10?! Dar es salaam yote hii aliacha shule saba tu za sekondari (za serikali, ambazo hata hivyo hakujenga yeye)-Jangwani, Azania, Tambaza, Forodhani, Kisutu na Kibasila!!! Nani atakayethubutu kusema kwamba shule hizo zilikuwa zinakidhi mahitaji ya elimu ya sekondari jijini? Huko mikoani ndo ilikuwa balaa tupu, unaweza kukuta mkoa mzima una shule moja au mbili za serkali.....bado tunaambiwa huduma za jamii zilikuwa bure! Ni serikali gani ingeshindwa kuhudumia shule chache kama hizo?!

Ubovu wa serikali ya Nyerere ni mwingi kuliko uzuri wake, otherwise, wale wanaoona kwamba mgtu akisema basi ana chuki za kidini (styupid thinking) basi anitajie hapa mazuri yaliyofanywa na serikali yake ambayo natarajia yawe mengi kuliko mabovu!

wapo watakaosema kwamba Nyerere amewezesha nchi hii kuwa na amani! Kwani aliichukuwa wakati nchi haina amani?! Sifa kama hizo anatastahili kupewa Kagame aliyechukua nchi baada ya mauaji ya kutisha nchini mwake! Anyway, waliosoma historia wanisaidie kunitajia ni vita gani vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vimepata kupiganwa Tanganyika katika karne ya 19! Kama hakuna au zilikuwa si za kutisha sana, basi inawezekana Watanganyika hatuna silika ya kupigana tangu zama hizo!!

Hivyo basi, mtu anavyotaja ubovu wa Nyerere inakuwa ni ujinga uliepitiliza kusema kwamba ni chuki binafsi...Na inakuwa sio ujinga, bali ni upumbavu mtu akisema ni chuki za kidini! Nyerere kama Nyerere alikuwa was a very good person BUT NOT A GOOD LEADER! He was a good person who was a poor leader! Kutokana na hayo, sipati kigumumizi hata chembe kusema wazi kwamba SI KWAMBA NYERERE ALIKUWA NA MAPUNGUFU, BALI ALIKUWA KIONGOZI MBOVU! Ukweli wenyewe ndio huo, ukiona mgumu kuumeza, chukua maji ushushie!

Anayekataa, atoe data za mazuri yake kama kiongozi yenyewe manufaa kwa Tanzania!

Kwani uongo? Si wewe ni mwislamu? Si haya mnamezeshwa msikitini? Sasa unakataa nini?
 
NasDaz, unashindwa kuelewa kwamba ukitafuta ubaya wa kiongozi yeyote duniani utaupata. Sitawatetea wale wanaodai kuwa Waislamu wana chuki na Nyerere kwa sababu huo ni ufinyu wa mawazo, ila nafikiri wale wote wanaomsifia Nyerere ni watu ambao wameangalia kwa makini yale aliyofanya kwenye kipindi cha uongozi wake. Mimi ni mmoja wao. Nimeona first hand umuhimu wa elimu ya bure na afya ya bure kwa sababu nimeifaidi. Nimekwenda darasani ambapo nimekuta textbooks kabatini pale darasani na kila mara daftari langu linavyomalizika nakwenda kwa mwalimu ananigawia lingine jipya naendelea na kazi yangu kama mwanafunzi. Wanaomsifia Mwalimu hawaangalii ni kiasi gani ameijaza mifuko ya watu bali wanaangalia kuwa nchi as a whole imesonga mbele kiasi gani wakati yupo. True, kuna policy zake nyingine zilitunyima maendeleo kiasi fulani lakini nitashangaa kama utamlinganisha Mwalimu na kiongozi kama Mheshimiwa wetu wa sasa ambaye anakaa kimya wakati amezungukwa na wezi wa wazi wazi. Hata watu wake kwenye chama chake mwenyewe wanamlaumu kwa mambo yanayoendelea. Usiwe na chuki kwa sababu ya wajinga wachache wanaotaka kuendeleza chuki za kidini na za kikabila. Wakati wa Nyerere usingeweza ukasikia mtu anasema wazi wazi kuwa mtu fulani hafai kwa sababu ya dini yake au kabila lake na siyo kwa sababu watu walikuwa wanapendana kuliko sasa hivi ila ni kwa kuwa viongozi waliokuweko wakati huo walikuwa wanatuonyesha kuwa taifa haliwezi kuendelea bila waTanzania kushirikiana kama wamoja. Chukia wanaomtetea kwa kutumia mbinu mbaya lakini mpe Mwalimu heshima anayostahili, please.
Sina mawazo finyu ila waislamu wanachuki na Nyerere
 
Baada ya kusoma ulichokiandika mapema nikagundua kuwa hauijui historia ya nchi yako na hili ni tatizo kwa watanzania wengi,lakini si kosa lako bali ni kosa la serkali yako kwani haijandika historia sahihi kuhusu nchi yako. Lakini unaweza kuwauliza wazazi wako kuwa wakati wanakulea wewe ni kipindi kipi kilikuwa kigumu kwao kati ya wakati ukiwa na miaka 0-15 na baada ya kuwa na miaka 15 na kuendelea.
 
Back
Top Bottom