Nyerere hakutaka kabisa kuitwa Mheshimiwa lakini aliheshimiwa, Sasa tuna waheshimiwa waliokosa Heshima

Wewe ndiyo unawadanganya watu.

Mambo ya kusema mtu sijui amekuja lini Dar, hayana msingi, na hayana uhusiano.

Mwalimu wakati wa uhuru mwaka 1961 (sikuwepo) akitangazwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza, alifika Mnazi mmoja akiwa kwenye benz. Benz hiyo ilinunuliwa na serikali ya Mwingereza. Miaka kadhaa iliyofuata alitumia benz.

Nikiwa na akili timamu, nipo shule ya msingi, nilimwona Mwalimu mwaka 1978 akiwa kwenye 110 landrover Mkoani Iringa. Mwaka 1979 nilikuwa eneo moja linaitwa Madaba, huko Ruvuma, nilimwona mwalimu akiwa kwenye 110. Watu wakawa wanaiongelea sana hiyo gari kwa sababu walikuwa hawajaona toleo hilo la landrover. Landrover zilizozoeleka zilikuwa ni 109.

Mwaka 1989, nimemwona Mwalimu akiwa kwenye landrover kijijini Butiama.

Kwa umri wako, haipendezi kuwahadaa watu.

Mwalimu alitumia benz, na huenda hata magari mengine lakini siyo eti kwa sababu ya kupenda anasa. Kwa ujumla Mwalimu aliyaishi maisha ya chini sana, maisha ya kawaida, nadiriki kusema ya chini kuliko hata tuliyokuwa tukiishi sisi.

Wanaotoka karibu na Butiama, wakaangalie pale kwenye jumba la makumbusho yake wakaone vitu alivyokuwa akivitumia, pamoja na mavazi yake. Nilipokuwa pale nilishangaa kuona hata saa alizokuwa akizivaa, kwa miaka ile ya 1980, ni zile ambazo zilikuwa zikiuzwa kule Kariakoo sh 5,000.
Alibinua royce rolls la Bei Kali katikati ya umasikini,lipo makumbusho
 
View attachment 2198283
Mwalimu View attachment 2198284

Sheikh

Sasa hizi mbuzi za siku hizi, utasikia Mheshimiwa, dakta, spika .......
Kuna siku nilikuwa na shida na Diwani wa eneo langu nilikuwa sijui kama anaitwa muheshimiwa nilipata shida Sana kumuelewa nilianza na samahani Diwani ananikatiza "mheshimiwa" Mimi sielewi naendelea na kilichonipeleka yeye kang'ang'ania "mheshimiwa" Kumbe anataka nianze na mheshimiwa ndio anisikilize, niliowakuta wananirekebisha "mheshimiwa" sio kusudi sikuelewa Hadi mtu akaniambie muite mheshimiwa Diwani , nikamwambia samahani sikujua hata hivyo sikumuita mheshimiwa, baada ya kutamka samahani ndio akanisikiliza shida yangu. Siwezi kumuita mtu mheshimiwa wakati ni kweli simuheshim
 
Nyerere alikataa kuitwa mtukufu na viongozi wote waliofanya nae kazi wanasema hivyo, hata nukuu zake zipo anazokataa utukufu.

Achana na stori za kina Mohamed Said
Nakumbuka Sana hiyo ilibidi wote tuitane ndugu, hata kwenye mikutano walikuwa wanatumia Sana neno "ndugu wananchi au ndugu mgeni rasmi
 
Wewe unatumia simulizi za watu wakati sisi wengine tumeshuhudia na kusikia kwa masikio yetu kwenye shughuli za kitaifa. Watambulishaji na wasoma risala wote walikuwa wakisema, “Mtukufu Rais…”
Hili la mtukufu wanalitumia Sana wasaka tonge siku hizi,
 
Acha kutulisha matango pori, Nyerere alipenda Kuheshimiwa ila alitaka kuku aminisha wewe kuwa hapendi kuitwa mheshimiwa , Alikwenda kazini ndani ya Merceses,kwanini hakupanda landrover kama mengine ya STG ?, aliishi kwnye surburbs ndani ya mansion , kwanini asinge ishi Magomeni kama wengine , watoto walenda shule nje ya Nchi , Urusi or Cuba , wanao jua nguo alizo vaa zilikuwa na quality kubw ana alijua quality vizuri na alifia kwnye Hospitali expensive huko London susitudanganye kwamba hakupenda kuheshimiwa .
we umelewa mapema hauko na wenzio
 
Kuna siku nilikuwa na shida na Diwani wa eneo langu nilikuwa sijui kama anaitwa muheshimiwa nilipata shida Sana kumuelewa nilianza na samahani Diwani ananikatiza "mheshimiwa" Mimi sielewi naendelea na kilichonipeleka yeye kang'ang'ania "mheshimiwa" Kumbe anataka nianze na mheshimiwa ndio anisikilize, niliowakuta wananirekebisha "mheshimiwa" sio kusudi sikuelewa Hadi mtu akaniambie muite mheshimiwa Diwani , nikamwambia samahani sikujua hata hivyo sikumuita mheshimiwa, baada ya kutamka samahani ndio akanisikiliza shida yangu. Siwezi kumuita mtu mheshimiwa wakati ni kweli simuheshim
Umenikumbusha jambo. Majuzi nikiwa kwenye kusanyiko fulani nilikutana na diwani mmoja na tukawa tunajadili mambo mawili matatu. Kwa vile nilikuwa simjui jina ikabidi nimwulize jina lake. Kwanza alianza kwa kusema "Naitwa (akataja jina lake)". Baada ya kukumbuka kwamba kataja jina bila kuanza na neno mheshimiwa ikabidi aanze upya na kusema " Naitwa mheshimiwa...." (akamalizia kwa kutaja jina). Wengi wao ni watu wa ovyo na waliolewa na tamaa ya kutaka kuheshimiwa na kila mtu.
 
 
Usiwadanganye watu. Mimi nimemwona Nyerere akiwa kwenye Landrover 110. Kaunda suti za Mwalimu Nyerere zilishonwa na fundi cherahani pale Kariakoo. Kuliwahi kuwa na makala maalum kwenye radio ya fundi cherahani aliyekuwa anashona nguo za Mwalimu.

Nyumba ya Mwalimu pale Butiama, ya kwako na yangu ni nzuri zaidi. Aliyojengewa na JWTZ alikataa kuingia. Rais Mwinyi akamsihi sana Mwalimu aingie kwenye nyumba mpya, hakuingia. Badala yake alisema, "wananiambia eti nihame kwenye nyumba hii kwa sababu ni ndogo, miaka mingi nimeishi kwenye nyumba, tukawazaa na watoto kwenye nyumba hii. Leo watotohawapo, wameondoja, itakuwaje ndogo". Waliendelea kumsihi, alipoingia kwenye nyumba hiyo, alikaa miezi 4 tu akafariki. Nenda kwenye jumba lake la makumbusho, ukaone mavazi yake, saa zake na redio, vyote ni vitu duni sana. Suti nzuri za Mwalimu ni zile mara tulipopata uhuru.

Nyumba yake yaMsasahaniilikarabatiwa na kuwa nzuri, baada ya kustaafu. Ni Serikali ndiyo iliyofanya matengenezo.

Hamuwezi elewa lolote ,nyie wakati Nyerere mpo mlikua bado maporini huko mkichunga ng'ombe hamuwezi jua ya mjini, msikiliza aliye soma Mbuyuni Primary na kusali St Peters Church, nadhani hata hamjui hapo St Peters na Mbuyuni ni wapi , mmesikia alikua anapanda gari gani kwenda kazini ? Sisi wa Toto wa Obay tuna mjua vizuri , tulieni wakuja nyie , huko Butiama mlikua mna vungwa na hizo ladrover, kwanza angepitia wapi bila hizo LandRovers 110 wakati barabara zilikuwa haziruhusu Mercedez kupita ?
 
Hakika kwa Nyerere, ila inasikitisha sana kwa viongozi wetu wa sasa...
 
Waliowahi kukutana na Mwalimu Nyerere, hawatakosa kumwelezea Mwalimu jinsi alivyojiona kuwa ni sawa na watu wengine.

Nikiwa shule ya msingi, darasa 4, nilipata nafasi kwa mara ya kwanza kushikana mkono na Mwalimu Nyerere, si pekee yangu bali tulikuwa watoto 8.

Mara ya pili nilikutana na kula naye Mwalimu Nyerere Butiama, akiwa amestaafu, nami nikiwa JKT baada ya kumaliza kidato cha 6, tukiwa tumepelekwa kwenye ujenzi wa nyumba aliyozawadiwa na jeshi baada ya kustaafu.

Maisha ya Mwalimu Nyerere kuanzia kufanya kazi kwa mikono yake, siyo kwaajili ya kupigwa picha bali kupalilia shamba la mahindi na mihogo kule Mwitongo, toka asubuhi mpaka saa 8 mchana (naiona taswira yake katika akili yangu akiwa amebeba jembe begani anarudi toka shambani akiwa amechoka), mpaka ulaji wake wa chakula, ilikuwa vigumu kuamini kuwa huyu tunayekula naye alikuwa Rais wa nchi. Sisi tuliwekewa chakula mezani, yeye akawa anakula na wajukuu zake kwenye sahani moja na bakuli moja.

Mwalimu Nyerere hakuwahi kujiona kuwa yeye ni binadamu zaidi kuliko binadamu wengine.

Mwalimu Nyerere, kuna wajinga fulani walijaribu kumwita MTUKUFU RAIS, aliwakemea na kuwakatalia kuwa hataki kabisa kuitwa MTUKUFU kwa maana mtukufu ni Mungu pekee yake. Baadaye wengine walijaribu kumwita MHESHIMIWA RAIS, Mwalimu alikataa, akawaambia kuwa wa kuheshimiwa ni wananchi. Akawaagiza kuwa aitwe NDUGU RAIS. Na hiyo ilienea kwa viongozi wake wote. Wakaitwa Ndugu Waziri, Ndugu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Mbunge, n.k. Lakini Mwalimu pamoja na kuitwa Ndugu, alipata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania. Matendo yake, maadili yale, uzalendo wake na upendo wake wa dhati kwa watu wake vilimpa heshima kubwa.

Leo tuna viongpzi waongo, wanafiki, wapenda sifa, wengine wevi na mafisadi, wala rushwa, wapora kura, wauaji, watekeji, wabambikiaji kesi, wapendelea watu, waonezi wa watu, LAKINI wanataka waitwe WAHESHIMIWA, wakati hawana heshima, na hakuna anayewaheshimu bali wanaoneshwa unafiki wa kuheshimiwa, na wao kwa sababu wana akili ndogo, wanaamini kuwa wanaheshimiwa.

Viongozi, fanyeni yaliyo ya heshima, mtapata heshima. Lakini kwa kujiita WAHESHIMIWA hamtakuwa waheshimiwa kama mnafanya mambo ya hovyo. Uue watu, uteke, ubambikie watu kesi, wewe kweli unajiona unastahili kuheshimiwa?
Sasa hivi ni ugonjwa umeingia karibu kila mahali. Utasikia " Mheshimiwa Diwani, Mheshimiwa Mama Diwani" yaani mke wa Diwani. Ukitoka kwenye siasa hata makanisani hali si shwari. Utasikia "Mheshimiwa Baba Paroko, Mheshimiwa Mchungaji n.k." . Kibaya zaidi ukisahau kuweka hiyo title wala hatakusikiliza shida yako. Utaambiwa "Kwani wewe hujui mimi naitwa Mheshimiwa Diwani? "
 
MMesikai alikua ana panda gari gani
Wewe ndiyo unawadanganya watu.

Mambo ya kusema mtu sijui amekuja lini Dar, hayana msingi, na hayana uhusiano.

Mwalimu wakati wa uhuru mwaka 1961 (sikuwepo) akitangazwa kuwa Waziri Mkuu wa kwanza, alifika Mnazi mmoja akiwa kwenye benz. Benz hiyo ilinunuliwa na serikali ya Mwingereza. Miaka kadhaa iliyofuata alitumia benz.

Nikiwa na akili timamu, nipo shule ya msingi, nilimwona Mwalimu mwaka 1978 akiwa kwenye 110 landrover Mkoani Iringa. Mwaka 1979 nilikuwa eneo moja linaitwa Madaba, huko Ruvuma, nilimwona mwalimu akiwa kwenye 110. Watu wakawa wanaiongelea sana hiyo gari kwa sababu walikuwa hawajaona toleo hilo la landrover. Landrover zilizozoeleka zilikuwa ni 109.

Mwaka 1989, nimemwona Mwalimu akiwa kwenye landrover kijijini Butiama.

Kwa umri wako, haipendezi kuwahadaa watu.

Mwalimu alitumia benz, na huenda hata magari mengine lakini siyo eti kwa sababu ya kupenda anasa. Kwa ujumla Mwalimu aliyaishi maisha ya chini sana, maisha ya kawaida, nadiriki kusema ya chini kuliko hata tuliyokuwa tukiishi sisi.

Wanaotoka karibu na Butiama, wakaangalie pale kwenye jumba la makumbusho yake wakaone vitu alivyokuwa akivitumia, pamoja na mavazi yake. Nilipokuwa pale nilishangaa kuona hata saa alizokuwa akizivaa, kwa miaka ile ya 1980, ni zile ambazo zilikuwa zikiuzwa kule Kariakoo sh 5,000.
Ndio maana nasema ulikua maporini, tulio mjini tulio kuwa tunaenda kwnye party na kukutana na kina Bhoke na Ghati na kusali St Peters na kuhudhuria dhifa za taifa Ikulu enzi hizo wote tunajua alikua anapanda Mercedez , huko porini kwenu kulikua hakuna barabara nzuri ndio maana akapanda hicho ki landrover , ila sisi mara zote St peters na tulioishana msafara wake akienda Ikulu toka msasani alikuwa kwnye Mercedez na Mbele gari yenye king'ora ilikua ni station wagon , usibishane na watoto w mjini .
Mama Magufuli huyu hapa anaongea ni kakulia mjini ana jua alicho kiongea sababu kaona kama sisi tulio kuwa tuna muona na hata hao watoto walio jipanga pale mbele tuna wajua , kamuulize Linda Binenhoult , dada yake Richars wa Big Brother kama hakua ana panga mstari pale wana salimiana na Nyerere . Huko Butihama ni Bushi apande Cidez wakati njia zina mahandaki wewe vipi? Sokoine mwenywe mlio dai mjamaa Amefia kwnye Cidiz .

 
Sasa hivi ni ugonjwa umeingia karibu kila mahali. Utasikia " Mheshimiwa Diwani, Mheshimiwa Mama Diwani" yaani mke wa Diwani. Ukitoka kwenye siasa hata makanisani hali si shwari. Utasikia "Mheshimiwa Baba Paroko, Mheshimiwa Mchungaji n.k." . Kibaya zaidi ukisahau kuweka hiyo title wala hatakusikiliza shida yako. Utaambiwa "Kwani wewe hujui mimi naitwa Mheshimiwa Diwani? "
Watu hawaelewi maana ya Mheshimiwa, Mheshimiwa haina maana ya kunyenyekewa, maana yake ni mtu aliye pewa heshima ya kututumikia au kutuwakilisha .
 
Wapumbavu na wendawazimu wengi hupendi sana kutukana maana ndicho wengi waliopungukiwa ufahamu wanachokiweza.

Nimdanganye mtu kuhusiana na Mwalimu, kwa faida gani nitakayoipata?
Nakereka kweli na hii Tania ya mtu kucomment Jambo ambalo hata halijui ila Basi acomment ujinga ili nae aonekane yupo..

Sijui tuna kizazi Cha namna gani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom