Nyerere hakutaka kabisa kuitwa Mheshimiwa lakini aliheshimiwa, Sasa tuna waheshimiwa waliokosa Heshima

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,467
40,972
Waliowahi kukutana na Mwalimu Nyerere, hawatakosa kumwelezea Mwalimu jinsi alivyojiona kuwa ni sawa na watu wengine.

Nikiwa shule ya msingi, darasa 4, nilipata nafasi kwa mara ya kwanza kushikana mkono na Mwalimu Nyerere, si pekee yangu bali tulikuwa watoto 8.

Mara ya pili nilikutana na kula naye Mwalimu Nyerere Butiama, akiwa amestaafu, nami nikiwa JKT baada ya kumaliza kidato cha 6, tukiwa tumepelekwa kwenye ujenzi wa nyumba aliyozawadiwa na jeshi baada ya kustaafu.

Maisha ya Mwalimu Nyerere kuanzia kufanya kazi kwa mikono yake, siyo kwaajili ya kupigwa picha bali kupalilia shamba la mahindi na mihogo kule Mwitongo, toka asubuhi mpaka saa 8 mchana (naiona taswira yake katika akili yangu akiwa amebeba jembe begani anarudi toka shambani akiwa amechoka), mpaka ulaji wake wa chakula, ilikuwa vigumu kuamini kuwa huyu tunayekula naye alikuwa Rais wa nchi. Sisi tuliwekewa chakula mezani, yeye akawa anakula na wajukuu zake kwenye sahani moja na bakuli moja.

Mwalimu Nyerere hakuwahi kujiona kuwa yeye ni binadamu zaidi kuliko binadamu wengine.

Mwalimu Nyerere, kuna wajinga fulani walijaribu kumwita MTUKUFU RAIS, aliwakemea na kuwakatalia kuwa hataki kabisa kuitwa MTUKUFU kwa maana mtukufu ni Mungu pekee yake. Baadaye wengine walijaribu kumwita MHESHIMIWA RAIS, Mwalimu alikataa, akawaambia kuwa wa kuheshimiwa ni wananchi. Akawaagiza kuwa aitwe NDUGU RAIS. Na hiyo ilienea kwa viongozi wake wote. Wakaitwa Ndugu Waziri, Ndugu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Mbunge, n.k. Lakini Mwalimu pamoja na kuitwa Ndugu, alipata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania. Matendo yake, maadili yale, uzalendo wake na upendo wake wa dhati kwa watu wake vilimpa heshima kubwa.

Leo tuna viongpzi waongo, wanafiki, wapenda sifa, wengine wevi na mafisadi, wala rushwa, wapora kura, wauaji, watekeji, wabambikiaji kesi, wapendelea watu, waonezi wa watu, LAKINI wanataka waitwe WAHESHIMIWA, wakati hawana heshima, na hakuna anayewaheshimu bali wanaoneshwa unafiki wa kuheshimiwa, na wao kwa sababu wana akili ndogo, wanaamini kuwa wanaheshimiwa.

Viongozi, fanyeni yaliyo ya heshima, mtapata heshima. Lakini kwa kujiita WAHESHIMIWA hamtakuwa waheshimiwa kama mnafanya mambo ya hovyo. Uue watu, uteke, ubambikie watu kesi, wewe kweli unajiona unastahili kuheshimiwa?
 
Mara ya mwisho kumuona Mwl Nyerere kwa karibu sana ilikuwa Novemba 1995 akiwa ndani ya kaunda suti yake ya maziwa maziwa kwny sherehe za kumuaga Mzee Ally Hassan Mwinyi kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar as salaam

kama kuna sehemu Nyerere alikosea basi ni kuzungukwa na Chawa mafisadi waliojifanya Wafia Ujamaa na wazalendo wa kweli kumbe ni zaid ya Majambazi ya kutumia silaha
 
Waliowahi kukutana na Mwalimu Nyerere, hawatakosa kumwelezea Mwalimu jinsi alivyojiona kuwa ni sawa na watu wengine.

Nikiwa shule ya msingi, darasa 4, nilipata nafasi kwa mara ya kwanza kushikana mkono na Mwalimu Nyerere, si pekee yangu bali tulikuwa watoto 8.

Mara ya pili nilikutana na kula naye Mwalimu Nyerere Butiama, akiwa amestaafu, nami nikiwa JKT baada ya kumaliza kidato cha 6, tukiwa tumepelekwa kwenye ujenzi wa nyumba aliyozawadiwa na jeshi baada ya kustaafu.

Maisha ya Mwalimu Nyerere kuanzia kufanya kazi kwa mikono yake, siyo kwaajili ya kupigwa picha bali kupalilia shamba la mahindi na mihogo kule Mwitongo, toka asubuhi mpaka saa 8 mchana (naiona taswira yake katika akili yangu akiwa amebeba jembe begani anarudi toka shambani akiwa amechoka), mpaka ulaji wake wa chakula, ilikuwa vigumu kuamini kuwa huyu tunayekula naye alikuwa Rais wa nchi. Sisi tuliwekewa chakula mezani, yeye akawa anakula na wajukuu zake kwenye sahani moja na bakuli moja.

Mwalimu Nyerere hakuwahi kujiona kuwa yeye ni binadamu zaidi kuliko binadamu wengine.

Mwalimu Nyerere, kuna wajinga fulani walijaribu kumwita MTUKUFU RAIS, aliwakemea na kuwakatalia kuwa hataki kabisa kuitwa MTUKUFU kwa maana mtukufu ni Mungu pekee yake. Baadaye wengine walijaribu kumwita MHESHIMIWA RAIS, Mwalimu alikataa, akawaambia kuwa wa kuheshimiwa ni wananchi. Akawaagiza kuwa aitwe NDUGU RAIS. Na hiyo ilienea kwa viongozi wake wote. Wakaitwa Ndugu Waziri, Ndugu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Mbunge, n.k. Lakini Mwalimu pamoja na kuitwa Ndugu, alipata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania. Matendo yake, maadili yale, uzalendo wake na upendo wake wa dhati kwa watu wake vilimpa heshima kubwa.

Leo tuna viongpzi waongo, wanafiki, wapenda sifa, wengine wevi na mafisadi, wala rushwa, wapora kura, wauaji, watekeji, wabambikiaji kesi, wapendelea watu, waonezi wa watu, LAKINI wanataka waitwe WAHESHIMIWA, wakati hawana heshima, na hakuna anayewaheshimu bali wanaoneshwa unafiki wa kuheshimiwa, na wao kwa sababu wana akili ndogo, wanaamini kuwa wanaheshimiwa.

Viongozi, fanyeni yaliyo ya heshima, mtapata heshima. Lakini kwa kujiita WAHESHIMIWA hamtakuwa waheshimiwa kama mnafanya mambo ya hovyo. Uue watu, uteke, ubambikie watu kesi, wewe kweli unajiona unastahili kuheshimiwa?
Acha kutulisha matango pori, Nyerere alipenda Kuheshimiwa ila alitaka kuku aminisha wewe kuwa hapendi kuitwa mheshimiwa , Alikwenda kazini ndani ya Merceses,kwanini hakupanda landrover kama mengine ya STG ?, aliishi kwnye surburbs ndani ya mansion , kwanini asinge ishi Magomeni kama wengine , watoto walenda shule nje ya Nchi , Urusi or Cuba , wanao jua nguo alizo vaa zilikuwa na quality kubw ana alijua quality vizuri na alifia kwnye Hospitali expensive huko London susitudanganye kwamba hakupenda kuheshimiwa .
 
Waliowahi kukutana na Mwalimu Nyerere, hawatakosa kumwelezea Mwalimu jinsi alivyojiona kuwa ni sawa na watu wengine.

Nikiwa shule ya msingi, darasa 4, nilipata nafasi kwa mara ya kwanza kushikana mkono na Mwalimu Nyerere, si pekee yangu bali tulikuwa watoto 8.

Mara ya pili nilikutana na kula naye Mwalimu Nyerere Butiama, akiwa amestaafu, nami nikiwa JKT baada ya kumaliza kidato cha 6, tukiwa tumepelekwa kwenye ujenzi wa nyumba aliyozawadiwa na jeshi baada ya kustaafu.

Maisha ya Mwalimu Nyerere kuanzia kufanya kazi kwa mikono yake, siyo kwaajili ya kupigwa picha bali kupalilia shamba la mahindi na mihogo kule Mwitongo, toka asubuhi mpaka saa 8 mchana (naiona taswira yake katika akili yangu akiwa amebeba jembe begani anarudi toka shambani akiwa amechoka), mpaka ulaji wake wa chakula, ilikuwa vigumu kuamini kuwa huyu tunayekula naye alikuwa Rais wa nchi. Sisi tuliwekewa chakula mezani, yeye akawa anakula na wajukuu zake kwenye sahani moja na bakuli moja.

Mwalimu Nyerere hakuwahi kujiona kuwa yeye ni binadamu zaidi kuliko binadamu wengine.

Mwalimu Nyerere, kuna wajinga fulani walijaribu kumwita MTUKUFU RAIS, aliwakemea na kuwakatalia kuwa hataki kabisa kuitwa MTUKUFU kwa maana mtukufu ni Mungu pekee yake. Baadaye wengine walijaribu kumwita MHESHIMIWA RAIS, Mwalimu alikataa, akawaambia kuwa wa kuheshimiwa ni wananchi. Akawaagiza kuwa aitwe NDUGU RAIS. Na hiyo ilienea kwa viongozi wake wote. Wakaitwa Ndugu Waziri, Ndugu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Mbunge, n.k. Lakini Mwalimu pamoja na kuitwa Ndugu, alipata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania. Matendo yake, maadili yale, uzalendo wake na upendo wake wa dhati kwa watu wake vilimpa heshima kubwa.

Leo tuna viongpzi waongo, wanafiki, wapenda sifa, wengine wevi na mafisadi, wala rushwa, wapora kura, wauaji, watekeji, wabambikiaji kesi, wapendelea watu, waonezi wa watu, LAKINI wanataka waitwe WAHESHIMIWA, wakati hawana heshima, na hakuna anayewaheshimu bali wanaoneshwa unafiki wa kuheshimiwa, na wao kwa sababu wana akili ndogo, wanaamini kuwa wanaheshimiwa.

Viongozi, fanyeni yaliyo ya heshima, mtapata heshima. Lakini kwa kujiita WAHESHIMIWA hamtakuwa waheshimiwa kama mnafanya mambo ya hovyo. Uue watu, uteke, ubambikie watu kesi, wewe kweli unajiona unastahili kuheshimiwa?

Nimeipenda hii

Sasa hivi tuna takataka siyo siri
 
Wakaitwa Ndugu Waziri, Ndugu Mkuu wa Mkoa, Ndugu Mbunge, n.k. Lakini Mwalimu pamoja na kuitwa Ndugu, alipata heshima kubwa ndani na nje ya Tanzania. Matendo yake, maadili yale, uzalendo wake na upendo wake wa dhati kwa watu wake vilimpa heshima kubwa.
Na hii ipo mpaka kwenye magazeti ya zamani hakuna sehemu mtu aliitwa Mhe.
 
images (9) - 2022-04-24T025656.720.jpeg

Ndugu Ali Hassan
 
Viongozi, fanyeni yaliyo ya heshima, mtapata heshima. Lakini kwa kujiita WAHESHIMIWA hamtakuwa waheshimiwa kama mnafanya mambo ya hovyo. Uue watu, uteke, ubambikie watu kesi, wewe kweli unajiona unastahili kuheshimiwa
Wengine wanajitangaza wenyewe kuwa ni ma-'Amiri Jeshi' wakuu.

Sijui cheo hicho ni kuwatisha watu waogope, hata haieleweki.
 
Acha kutulisha matango pori, Nyerere alipenda Kuheshimiwa ila alitaka kuku aminisha wewe kuwa hapendi kuitwa mheshimiwa , Alikwenda kazini ndani ya Merceses,kwanini hakupanda landrover kama mengine ya STG ?, aliishi kwnye surburbs ndani ya mansion , kwanini asinge ishi Magomeni kama wengine , watoto walenda shule nje ya Nchi , Urusi or Cuba , wanao jua nguo alizo vaa zilikuwa na quality kubw ana alijua quality vizuri na alifia kwnye Hospitali expensive huko London susitudanganye kwamba hakupenda kuheshimiwa .
Wewe hata kulishwa matango pori ni heshima kubwa kwako, unastahiri kulishwa..., kwa heshima ya anayeongelewa hapa, naacha ujazie mwenyewe.
 
Seriously? Wewe umezaliwa lini, mkuu?

Nchi hii ni wakuu wa nchi wawili tu waliowahi kuitwa Mtukufu Rais. Nao ni Nyerere na Mwinyi. Rais Mkapa ndiye aliyefuta huo utukufu wa Rais!
Nyerere alikataa kuitwa mtukufu na viongozi wote waliofanya nae kazi wanasema hivyo, hata nukuu zake zipo anazokataa utukufu.

Achana na stori za kina Mohamed Said
 
Acha kutulisha matango pori, Nyerere alipenda Kuheshimiwa ila alitaka kuku aminisha wewe kuwa hapendi kuitwa mheshimiwa , Alikwenda kazini ndani ya Merceses,kwanini hakupanda landrover kama mengine ya STG ?, aliishi kwnye surburbs ndani ya mansion , kwanini asinge ishi Magomeni kama wengine , watoto walenda shule nje ya Nchi , Urusi or Cuba , wanao jua nguo alizo vaa zilikuwa na quality kubw ana alijua quality vizuri na alifia kwnye Hospitali expensive huko London susitudanganye kwamba hakupenda kuheshimiwa .
Dah!Mbona una gubu hivyo?🤣🤣🤣🤣
 
Leo tunao akina Mtukufu, Dr,Rais na Amiri jeshi mkuu Jakaya Kikwete
 
Nyerere alikataa kuitwa mtukufu na viongozi wote waliofanya nae kazi wanasema hivyo, hata nukuu zake zipo anazokataa utukufu.

Achana na stori za kina Mohamed Said

Wewe unatumia simulizi za watu wakati sisi wengine tumeshuhudia na kusikia kwa masikio yetu kwenye shughuli za kitaifa. Watambulishaji na wasoma risala wote walikuwa wakisema, “Mtukufu Rais…”
 

Lissu alisema Nyerere alizowea kuishi kwa uongo, ni bora huyo mzee mumuache tu apumzike zake na nidhamu tuliyojiwekea ya kutokumkosoa.
 
Sasa tuna hizi mbwa mh,dakitari muandamizi ya uchumi mkubwa aliyebobea,mubunge na kamanda ya mugambo kitaifa mh pumbukali masulupwenye.Mbwembwe nyiiingi matokeo mbegu ya mchicha
 
Wewe unatumia simulizi za watu wakati sisi wengine tumeshuhudia na kusikia kwa masikio yetu kwenye shughuli za kitaifa. Watambulishaji na wasoma risala wote walikuwa wakisema, “Mtukufu Rais…”
Wafuasi wa ile imani mnamatatizo na hayataisha hadi mwisho! Mbegu mliyopandikizwa ni mzigo katika ubongo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom