Nyerere Day; CCM Ijitafakari Ijitafakari Kuondoka Kwake Mioyoni mwa Watanzania.

Chakaza

JF-Expert Member
Mar 10, 2007
39,794
71,214
Wakati Watanzania wakikumbuka miaka 20 ya uwepo wa CCM bila ya mwanzilishi wake Mwl J.K.Nyerere chama hicho kikongwe kilipaswa kukaa chini na kujipima mbona kimeondoka mioyoni mwa Watanzania na kutoka kuwa chama cha siasa (maridhiano) na kubakia kuwa Chama dola (mabavu)?
Mfano mwepesi kabisa ni hili zoezi la uchaguzi wa serikali za mitaa, imekuwaje watu hawataki kujiandikisha mpaka imebidi vitumike vitisho kwa watumishi mfano waalimu wakajiandikishe?
Hivi imefikia hali ya kulazimishana kujiandikisha kupiga kura wakati zamani siku zilionekana hazitoshi kwa wingi wa wanaojiandikisha?
Hii inaonyesha kuwa watu wenye mapenzi na CCM wanaweza kuwa chini ya 20% kulingana na turn up ya hiari ya uchaguzi.
Sasa jee wale mamia na maelfu wanaojitokeza kuonyesha ni wanaccm ni "wajasiriamali wa kisiasa?"
Wakati tukielekea 2020 kwenye uchaguzi mkuu, huu wa serikali za mitaa upinzani ilikuwa kete muhimu kwao kuamua kutangaza kutoshiriki kwa kutaja sababu zao ili zitekelezwe haraka. Lakini tumeona wapinzani kadhaa ndio wanapiga kampeni ili watu wajiandikishe wasidharau na kesho wanalia wao.
CCM ya Magufuli iangalie inaangukia wapi? Ubabe na kujimwambafai havita wapeleka kokote zaidi ya kujipoteza kwenye ramani ya kisiasa na kubaki kuwa chama cha polisi na TISS.
 
Ni kweli uliyosema lakin suala la kususia uchaguzi sio sawa.Waendeleee kushiriki ili madudu yao yawe wazi kisha uchaguzi wa mwakani utaona watakaojiandikisha uchaguzi mkuu mil 10.hawafiki.

Moja ya mambo yaliyofanya uchaguzi huu kudorora ni pamoja na uhuni wa NEC 2015 pamoja na kasoro zote zingine kwa pamoja zinapelekea hata vijijini kufunguka macho kwa hiyo uchaguzi uendelee ili macho ya wengi zaidi yatoe ukungu.
 
Mambo kama haya hayajawahi kutokea huko siku za nyuma.
Ni ishara ya kutokubalika
tapatalk_1571021627565.jpeg
 
Sidhani kama kuna nafasi iliyobakia ya kuishauri CCM kama chama. CCM inajitambulisha kama chama dola. Inajiona siyo tu inaunda serikali, bali ina hati miliki ya rasilimali nchi na watu pia. Tumeshuhudia serikali na CCM wakishirikiana kuua upinzani na kuwasumbua hata raia wa kawaida wanaotoa mawazo yao tu.

Ni hahati nbaya tu kuwa vyama vya siasa vya Tanzania hata vile vikubwa na vyenye ushawishi, ni mali ya mwenyekiti. Mfano CUF baada ya CCM kufanikiwa kumrudisha Lipumba chama kilikufa hapo hapo. CCM na serikali wanaendeleza harakati za kumtoa mwenyekiti wa CHADEMA wakiamini kuwa wakifanikiwa na chama kitakuwa kimekufa.

Wanapokosea CCM ni kujiaminisha kuwa wakiua upinzani na mawazo mbadala basi AUTOMATICALLY wao watapendwa. Ni sawa na mtu anayefikiri jirani yake anayeonekana kufanikiwa katika biashara zake, basi akifa au biashara yake ikiyumba basi yeye ambaye hajafanikiwa automatically atafanikiwa. UKOSEFU WA AKILI.

CCM imefika mahali viongozi wake wanazunguka na kuwatukana wananchi eti walikosea kuchagua upinzani, eti hawataletewa maendeleo na CCM hata kama wanalipa kodi. Eti hata maji wakawadai hao wapinzani. CCM wakekuwa majuha. Mimi nikupe wewe pesa za kodi kisha maendeleo nikadai upinzani ambao hawakusanyi kodi????? CCM ni imelaaniwa.
 
Haya mambo tushaongea mpaka tukachoka. Kuna mbunge aliwahi kusema ipo siku wananchi watachoka na kuingia mtaani wenyewe sasa hapo ndio mtaelewa ukipanda mahindi usitegemee kuvuna mapera. Chuki wanayopandikiza kwa watu ni kubwa.
 
Ni wazi sasa wananchi wanahitaji uongozi mpya nje ya CCM. Hivyo basi ni nafasi ya upinzani kujiimarisha kuhakikisha wanashika dola.
 
Back
Top Bottom