Ninja
JF-Expert Member
- Feb 5, 2010
- 348
- 535
Wanadamu tumekuwa tukihangaika siku zote kupata mambo mema na hasa hasa mambo yanayotafutwa zaidi duniani ni mapenzi, pesa, mali, maisha bora, maisha marefu, maendeleo na amani na utulivu.
Mambo yafuatayo yametamkwa na wengi kama 'ingredients' za dawa ya kupata mahitaji yote kama yalivyotajwa hapo juu.
Hekima, busara, maarifa, elimu, ujuzi, akili, kipaji, ufahamu, mbinu na werevu. Hizi zimetajwa maeneo mbalimbali kuwa ni nyenzo zenye thamani kuliko fedha, mali na mengineyo kwa kuwa ndio chanzo cha fedha, mali na mengineyo.
Je ni kuna ukweli wowote kwenye kauli hizi?
Je maana halisi ya nyenzo hizi ni nini? Kuna tofauti gani baina ya kila moja?
Je ni mchanganyiko upi ni bora zaidi unapochanganya nyenzo hizi ili kuleta matokeo bora zaidi?
Je ni kwa jinsi gani kila moja ya hizo hupatikana? mfano unawezaje kupata busara? au werevu hutokana na nini?
Je unapimaje kuwa mtu fulani, au wewe mwenyewe, au kiongozi fulani ana mchanganyiko ulio bora wa hayo? au pengine 'formula' imekataa kabisa ni 0+0+0?
Mambo yafuatayo yametamkwa na wengi kama 'ingredients' za dawa ya kupata mahitaji yote kama yalivyotajwa hapo juu.
Hekima, busara, maarifa, elimu, ujuzi, akili, kipaji, ufahamu, mbinu na werevu. Hizi zimetajwa maeneo mbalimbali kuwa ni nyenzo zenye thamani kuliko fedha, mali na mengineyo kwa kuwa ndio chanzo cha fedha, mali na mengineyo.
Je ni kuna ukweli wowote kwenye kauli hizi?
Je maana halisi ya nyenzo hizi ni nini? Kuna tofauti gani baina ya kila moja?
Je ni mchanganyiko upi ni bora zaidi unapochanganya nyenzo hizi ili kuleta matokeo bora zaidi?
Je ni kwa jinsi gani kila moja ya hizo hupatikana? mfano unawezaje kupata busara? au werevu hutokana na nini?
Je unapimaje kuwa mtu fulani, au wewe mwenyewe, au kiongozi fulani ana mchanganyiko ulio bora wa hayo? au pengine 'formula' imekataa kabisa ni 0+0+0?