SCOOBY DOO
Member
- Dec 16, 2013
- 76
- 69
Hali ya uchaguzi wa Kata ya Nyasura iliyoko Bunda bado ni tete. Jana kamatakamata iliendelea na kama nilivyowataarifa jana ni kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bunda amekwenda kuchukua vijana wa Jeshi la kujenga Taifa (JKT) ndio wanaofanya zoezi la kukamata watu na maabusu yao kubwa ni kwenye Ofisi za CCM za wilaya. Leo wameendelea kukamata vijana wa CHADEMA alimradi aonekane amevaa gwanda huyo lazima abebwe.
Leo ndo vyama vyote walikuwa wakifunga kampeni zao, wakati Chadema wakifungia katika chuo cha Ualimu Bunda, CCM walifungia kwenye viwanja maalufu kwa jina la Majenmbe. Nimetembelea mikutano yote miwili. Ule wa CCM haukuwa na watu isipokuwa magali mengi wakati ule wa CHADEMA watu walikuwa wamefurika tele.
Asubuh ya leo kumekuwa na vituo vya kutosha ambavyo CCM walikuwa wakitumia kugawa rushwa, nilijitahidi kupita katika vituo viwili ambavyo niliwakuta akina mama kama hamsini mpaka sitini wakipewa kiasi cha Sh elfu mbili kila mtu na kupewa ahadi ya kuongezewa zaidi, wakati nikiwa kwenye kituo hicho mara niliona gari ambalo nililitambua ni la Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mara likija ilibidi nisepe.
Mpaka sasa daftari la kituo kimoja cha kupigia kura halionekani. Dalili za vurugu zinaendelea kuonekana kuwepo, nimepata message kwamba kuna mahala wanagawa pesa ngoja niende afu nitawajulisheni.
Leo ndo vyama vyote walikuwa wakifunga kampeni zao, wakati Chadema wakifungia katika chuo cha Ualimu Bunda, CCM walifungia kwenye viwanja maalufu kwa jina la Majenmbe. Nimetembelea mikutano yote miwili. Ule wa CCM haukuwa na watu isipokuwa magali mengi wakati ule wa CHADEMA watu walikuwa wamefurika tele.
Asubuh ya leo kumekuwa na vituo vya kutosha ambavyo CCM walikuwa wakitumia kugawa rushwa, nilijitahidi kupita katika vituo viwili ambavyo niliwakuta akina mama kama hamsini mpaka sitini wakipewa kiasi cha Sh elfu mbili kila mtu na kupewa ahadi ya kuongezewa zaidi, wakati nikiwa kwenye kituo hicho mara niliona gari ambalo nililitambua ni la Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Mara likija ilibidi nisepe.
Mpaka sasa daftari la kituo kimoja cha kupigia kura halionekani. Dalili za vurugu zinaendelea kuonekana kuwepo, nimepata message kwamba kuna mahala wanagawa pesa ngoja niende afu nitawajulisheni.