kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
Wakati huo huo, watu wawili akiwemo msimizi mmoja wa uchaguzi kutoka kata ya Segerea wanadaiwa kukamatwa na nyaraka kadhaa za tume ya uchaguzi, ikiwamo mihuri nje ya kituo cha kujumlisha kura cha Anatoglou jijini Dar es Salaam.
Habari zilizolifikia gazeti hili jana usiku zimeeleza kuwa watu hao walitoka kununua chakula walikamatwa kwa nyakati tafauti majira ya saa 3:00 usiku nje ya kituo hicho wakiwa na nyaraka hizo ambazo ziliwekwa kwenye chakula walichokuwa wamebeba.
Tukio hilo lilizua zogo katika kituo hicho kilichozungukwa na maelfu ya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakishinikiza matokeo ya jimbo hilo yatangazwe.
Afisa huyo wa uchaguzi alikamatwa majira ya saa 3:00 usiku jana alipokuwa akirudi kununua chakula. Aliposhukiwa kuwa na nyaraka hizo, alipekuliwa na kukutwa nazo.
"Aliporudi walimuuliza umebeba nini? Akajibu "Chakula." chanzo cha habari kilieleza na kuendelea:
Waliendelea kumhoji "Tutaamini vipi kama umebeba chakula tu? Tunaomba tukupekue."
Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, wafuasi hao walianza kumpekua afisa huyo kukuta pamoja na chakula, karatasi za matokeo zenye mihuri ya Nec.
Gazeti hili lilifika eneo la tukio majira ya saa 6:00 usiku na kukuta hali ikiwa imetulia huku askari wanne wa kutuliza ghasia (FFU) wenye silaha wakiwa wamezunguka kituo hicho huku mamia ya wananchi wakisubiri matoke katika eneo hilo.
Jitihada za gazeti hili kumpata kamanda wa polisi mkoa wa Ilala Faustine Shilogile jana usiku zilishindikana baada ya simu zake za mikononi kuzimwa.
Katika hatua nyingine wagombea ubeunge wa CUF na Chadema waliliambia gazeti hili kuwa wamewasilisha malalamiko yao NEC, kutaka uchaguzi huo urudiwe kabla matokeo hayajatangazwa.
Mpendazoe wa Chadema na Timangale Mussa (CUF), walisema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona kuwa uchaguzi huo umegubikwa na kasoro nyingi tangu mwanzo wa mchakato wake.
Msimamizi wa Uchaguzi Manispaa ya Ilala, Gabriel Fuime alikirikupokea malalamiko hayo lakini akasema hayakuwasili kwa barua h
Habari zilizolifikia gazeti hili jana usiku zimeeleza kuwa watu hao walitoka kununua chakula walikamatwa kwa nyakati tafauti majira ya saa 3:00 usiku nje ya kituo hicho wakiwa na nyaraka hizo ambazo ziliwekwa kwenye chakula walichokuwa wamebeba.
Tukio hilo lilizua zogo katika kituo hicho kilichozungukwa na maelfu ya wafuasi wa Chadema waliokuwa wakishinikiza matokeo ya jimbo hilo yatangazwe.
Afisa huyo wa uchaguzi alikamatwa majira ya saa 3:00 usiku jana alipokuwa akirudi kununua chakula. Aliposhukiwa kuwa na nyaraka hizo, alipekuliwa na kukutwa nazo.
"Aliporudi walimuuliza umebeba nini? Akajibu "Chakula." chanzo cha habari kilieleza na kuendelea:
Waliendelea kumhoji "Tutaamini vipi kama umebeba chakula tu? Tunaomba tukupekue."
Kwa mujibu wa mtoa taarifa huyo, wafuasi hao walianza kumpekua afisa huyo kukuta pamoja na chakula, karatasi za matokeo zenye mihuri ya Nec.
Gazeti hili lilifika eneo la tukio majira ya saa 6:00 usiku na kukuta hali ikiwa imetulia huku askari wanne wa kutuliza ghasia (FFU) wenye silaha wakiwa wamezunguka kituo hicho huku mamia ya wananchi wakisubiri matoke katika eneo hilo.
Jitihada za gazeti hili kumpata kamanda wa polisi mkoa wa Ilala Faustine Shilogile jana usiku zilishindikana baada ya simu zake za mikononi kuzimwa.
Katika hatua nyingine wagombea ubeunge wa CUF na Chadema waliliambia gazeti hili kuwa wamewasilisha malalamiko yao NEC, kutaka uchaguzi huo urudiwe kabla matokeo hayajatangazwa.
Mpendazoe wa Chadema na Timangale Mussa (CUF), walisema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona kuwa uchaguzi huo umegubikwa na kasoro nyingi tangu mwanzo wa mchakato wake.
Msimamizi wa Uchaguzi Manispaa ya Ilala, Gabriel Fuime alikirikupokea malalamiko hayo lakini akasema hayakuwasili kwa barua h