GAGL
JF-Expert Member
- Aug 5, 2010
- 390
- 395
Wanajamvi nchi hii ina mengi sana ya kutafakari kiujumla na kwa kumwangalia mtu mmoja mmoja. Bila shaka kila mtu hapa mwenye umri usiozidi miaka thelethini anamjua vizuri Nyambari Nyangwine na umaarufu wake alioupata kutokana na mchango wake hasi katika elimu ya Tanzania. Huyu jamaa alileta mtindo wa vitabu vya maswali na majibu ambavyo vim eharibu kabisa uelewa wa wanafunzi, maana badala ya kusoma vitabu vizuri vilivyoandikwa na maprofesa waliobobea, watoto wengi wamekuwa watumwa wa mitihani kwa kukesha wakimsoma nyangwine aliyekopi maswali yote ya mitihani ya taifa halafu akayaita kitabu. Huyu jamaa katika serikali ya watu makini, anastahili adhabu kali kwa kuchangia kuharibu elimu yetu.