TUNTEMEKE
JF-Expert Member
- Jun 15, 2009
- 4,587
- 579
Mwandishi na msambazaji wa vitabu nchini, Bwana Nyambari Nyangwine, kwa siku nyingi amekuwa akiendeleza harakati zake za kuteuliwa kugombea ubunge katika jimbo la Tarime kupitia CCM. Na kundi la aliyekuwa mbunge wa Tarime Bw. Kisyeri Chambiri limeamua kumuunga mkono. wakati huohuo Kanali Msitaafu wa jeshi, Kanali Kichonge (miaka 65) naye alitangaza December mwaka jana kuwa atagombea ubunge Tarime kupitia CCM, Kanali Kichonge ambaye ni Ndugu ya Mkuu wa wilaya ya Kwimba Bw.Ryoba Kangoye ambaye alishindwa katika uchaguzi mdogo wa Tarime inasemekana ataungwa mkono na kundi la Christopher Gachuma, ambaye ni Mjumbe wa NEC CCM na Mkurugenzi wa Nyanza Bottling, na ikumbukwe kuwa uhasama wa makundi ya Chambiri na Gachuma ndiyo yalimpa Mh. Chacha Zakayo Wangwe nguvu baada ya kuwa na uhasama mkubwa na kupelekea kundi la Gachuma kumuunga mkono Chacha Wangwe na kumshinda Chambiri, na katika uchaguzi mdogo kundi la Chambiri liliwaunga CHADEMA kwani Bw. Ryoba Kangoye ambaye ni kambi ya Gachuma ndiyo alikuwa mgombea na alihusika kumhujumu Chambiri mwaka 2005, na CCM ndio chama chenye nguvu Tarime lakini mara zote uwepo wa makundi haya ndio yanaipa CHADEMA nguvu ya kupita katikati.
je mwaka huu kutokana na wagombea hao wa CCM kuendelea kujikita katika makundi hasimu, iwapo mmojawao atateuliwa nini kitatokea?, kwani pia ikumbukwe kuwa CHADEMA Tarime nayo imegawanyika katika makundi matatu yanayowaunga mkono Mh, Mwera, Mwita Waitara na John Heche, huku kukiwa na uadui mkubwa toka kwa hao wagombea watarajiwa hadi kwa wafuasi wao kitu ambacho kinatishia mustakabali wao na tayari Mh. Mwera alikwishashitaki kwa viongozi wakuu wa CHADEMA kuwa Diwani Heche na Mwita Waitara wanamdharau na kumwita ni dhaifu kama mwanamke.
je mwaka huu kutokana na wagombea hao wa CCM kuendelea kujikita katika makundi hasimu, iwapo mmojawao atateuliwa nini kitatokea?, kwani pia ikumbukwe kuwa CHADEMA Tarime nayo imegawanyika katika makundi matatu yanayowaunga mkono Mh, Mwera, Mwita Waitara na John Heche, huku kukiwa na uadui mkubwa toka kwa hao wagombea watarajiwa hadi kwa wafuasi wao kitu ambacho kinatishia mustakabali wao na tayari Mh. Mwera alikwishashitaki kwa viongozi wakuu wa CHADEMA kuwa Diwani Heche na Mwita Waitara wanamdharau na kumwita ni dhaifu kama mwanamke.