Waziri kivuli
JF-Expert Member
- Nov 30, 2016
- 2,987
- 3,450
Rais Magufuli akizungumza na Wananchi wa Wilaya ya Nyamongo mkoani Mara amewaamuru Waziri wa madini na Mkuu wa Mkoa kumtafuta mtu aliyetajwa kwa jina la King'anya ambaye ndiye mhusika wa mfuko wa kusaidia Wilaya hiyo toka kwa kampuni ya Acacia uitwao North Mara Trust Fund.
Hii ni baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri kumtaja Bwana King'anya kuwa ndiye anayejua kiasi gani kipo kwenye mfuko huo maana ndiye anayewasiliana na Acacia. Mkurugenzi akasema makazi yake yako Nyamwaga lakini wananchi wakapaza sauti kuwa "YUPO".
Katika kumuulizia King'anya, mmoja wa wananchi aliropoka na kupelekea Rais kusema, "Tatizo humu vichaa ni wengi. King'anya ndio signature zake ziko huko sasa wewe unaitwa Charles, unaweza kuingia kwenye mtego usio wako ukaacha mke wako tena mdogo akaja akaolewa na King'anya"
Hadi Rais anaondoka Nyamongo Bwana King'anya alikuwa hajaonekana.
Hii ni baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri kumtaja Bwana King'anya kuwa ndiye anayejua kiasi gani kipo kwenye mfuko huo maana ndiye anayewasiliana na Acacia. Mkurugenzi akasema makazi yake yako Nyamwaga lakini wananchi wakapaza sauti kuwa "YUPO".
Katika kumuulizia King'anya, mmoja wa wananchi aliropoka na kupelekea Rais kusema, "Tatizo humu vichaa ni wengi. King'anya ndio signature zake ziko huko sasa wewe unaitwa Charles, unaweza kuingia kwenye mtego usio wako ukaacha mke wako tena mdogo akaja akaolewa na King'anya"
Hadi Rais anaondoka Nyamongo Bwana King'anya alikuwa hajaonekana.