MwanaPekee
JF-Expert Member
- Jul 18, 2014
- 382
- 385
Lazaro Nyalandu naye inaonekana amefanya kosa linalofanana kabisa na kosa lililofanywa na akina Lowassa na Lembeli. Ni kosa la kudhani kwamba unapendwa sana na unamashabiki wengi ambao wataambatana na wewe popote utakapokuwa. Ni kosa la kuona kwa “hakuna mtu mwingine” zaidi yako atakayeweza kufanya kile ulichokuwa ukikifanya katika ubora uleule au hata zaidi yako. Ni kosa la “miscalculation” na kuwa “overoptimistic” juu yako mwenyewe.
Kilichowapata Lowassa na Lembeli sote tunajua. Sasa wamepotea kabisa katika uringo wa siasa, hakuna anayewataja tena. Watu waliodhani kwamba wangewafuata kule waliko, waliamua kubaki ndani ya hema la CCM ambako waliona ni salama zaidi badala ya kwenda wasikokujua. Hakika lilikuwa ni kosa kubwa la kujivika “Umungu Mtu” lililopelekea kufa kabisa kisiasa.
Cha ajabu sana tena sana, Lazaro naye amecheza mchezo huo kwa namna ile ile ulivyochezwa na L&L. Mwalimu Nyerere alipata kusema, kuna wakati mtu unajiita au kuitwa vile unavyojiita au kuitwa kwa sababu ya mfumo uliopo ndani yake; nje ya huo mfumo si wewe tena; akitumia maneno “Nje ya Muungano hakuna Mzanzibari ila kuna Muunguja na Mpemba”. Hawa 3L’s wameshindwa kuliona hilo kabisa, kwamba wanatazamwa vile walivyo wakiwa ndani ya mfumo uliowajenga, nje ya hapo they are not the same. Zaidi ya hapo Lazaro alishindwa kukumbuka kwamba, yeye katika uringo wa siasa aliibuka tu kama uyoga, hakuwa na background strong sana kama akina Lowassa ambao pia wamepotezwa, lakini bado akashupaa shingo na kudanganyika kwamba ataendelea kuwa on top hata ndani ya mfumo mpya. Goodbye forever Lazaro, tutai-miss sana sauti yako Bungeni.
Kilichowapata Lowassa na Lembeli sote tunajua. Sasa wamepotea kabisa katika uringo wa siasa, hakuna anayewataja tena. Watu waliodhani kwamba wangewafuata kule waliko, waliamua kubaki ndani ya hema la CCM ambako waliona ni salama zaidi badala ya kwenda wasikokujua. Hakika lilikuwa ni kosa kubwa la kujivika “Umungu Mtu” lililopelekea kufa kabisa kisiasa.
Cha ajabu sana tena sana, Lazaro naye amecheza mchezo huo kwa namna ile ile ulivyochezwa na L&L. Mwalimu Nyerere alipata kusema, kuna wakati mtu unajiita au kuitwa vile unavyojiita au kuitwa kwa sababu ya mfumo uliopo ndani yake; nje ya huo mfumo si wewe tena; akitumia maneno “Nje ya Muungano hakuna Mzanzibari ila kuna Muunguja na Mpemba”. Hawa 3L’s wameshindwa kuliona hilo kabisa, kwamba wanatazamwa vile walivyo wakiwa ndani ya mfumo uliowajenga, nje ya hapo they are not the same. Zaidi ya hapo Lazaro alishindwa kukumbuka kwamba, yeye katika uringo wa siasa aliibuka tu kama uyoga, hakuwa na background strong sana kama akina Lowassa ambao pia wamepotezwa, lakini bado akashupaa shingo na kudanganyika kwamba ataendelea kuwa on top hata ndani ya mfumo mpya. Goodbye forever Lazaro, tutai-miss sana sauti yako Bungeni.