Nyalandu auponda mfumo wa uteuzi wa Wagombea Urais ndani ya CHADEMA. Ataka uwekwe mfumo ulio wazi na wa kidemokrasia wa kuwapata Wagombea

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Kada wa CHADEMA, Lazaro Nyalandu amekitaka Chama chake cha CHADEMA kiweke mfumo ulio wazi na wa kidemokrasia wa kuwapata Wagombea katika ngazi zote. "CHADEMA inapaswa kuweka mfumo wenye kuonyesha utaratibu mahsusi ambao upo wazi na wa kidemokrasia. .... hadi Mwezi Juni mwaka huu uwe umekamilika kabla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu 2020."

Nyalandu alisema kuwa, nafasi ya Urais ni muhimu hivyo wanaotaka kugombea ni vyema wawe na uwezo wa kuwafikia wapiga kura ili anayeshinda kwenye kura za maoni awe na nafasi kubwa ya kupambana na Mgombea wa CCM.

Mtazamo huu wa Nyalandu unaonyesha wazi kuwa hauamini kabisa Mfumo wa uteuzi wagombea wa CHADEMA kutokana na kughubikwa na dhuruma na upendeleo bila kujali uwezo wa Mgombea husika.
Inawezekana Nyalandu keshanusa harufu ya kutokuwa na "chake" mbele ya wababe na masalia wa CHADEMA. Probably, Yule kingpin aliyemvutia hadi kuhamia Upinzani anawekewa mizengwe ili asigombee Urais kupitia CHADEMA.


IMG_0623.JPG
 
Kada wa CHADEMA, Lazaro Nyalandu amekitaka Chama chake cha CHADEMA kiweke mfumo ulio wazi na wa kidemokrasia wa kuwapata Wagombea katika ngazi zote. "CHADEMA inapaswa kuweka mfumo wenye kuonyesha utaratibu mahsusi ambao upo wazi na wa kidemokrasia. .... hadi Mwezi Juni mwaka huu uwe umekamilika kabla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu 2020."

Nyalandu aliisema kuwa, nafasi ya Urais ni muhimu hivyo wanaotaka kugombea ni vyema wawe na uwezo wa kuwafikia wapiga kura ili anayeshinda kwenye kura za maoni awe na nafasi kubwa ya kupambana na Mgombea wa CCM.

Mtazamo huo wa Nyalandu unaonyesha wazi kuwa hauamini kabisa Mfumo wa uteuzi wa CHADEMA kutoka na kughubikwa na dhuruma na upendeleo bila kujali uwezo wa Mgombea husika.

View attachment 994762
sidhani kama hii itakusaidia sana. Jaribu ingine !
 
Katiba ya nchi na ya chama chake inampa uhuru wa kutoa maoni na uzuri maoni yenyewe ni ya kujenga
Kwa nini usiseme tu ukweli kuwa, amegundua mfumo wao ni mbovu na hana uhakika wa yeye kupita ama anayempenda kupita kwenye mchujo wa Chama kutokana na kutokuwepo kwa mfumo unaoeleweka?
 
CHADEMA haina makasuku wa kuamini kila propaganda kama hicho chama chakavu, mnapoteza muda afadhali ungetunga propaganda yenye akili kidogo si ya dalasa la pili kama hii.
 
Kwa hiyo na wewe unakiri wazi kuwa mfumo wa CHADEMA ni mbovu siyo, ama wewe hauoni tatizo bali umeona mtu kutoa maoni ndiyo tatizo na siyo kutatua tatizo lililopo?
Huwa naamini wewe jamaa una akili ndogo sana. ushahidi ni unayoandika hapa,..... hakuna ppote kwenye katiba ya ccm walipoandika kuwa raisi aongoze miaka 10... mbona huizungumzii issue ya membe vs bashiru?
 
Ili huyu kichaa tuliyenaye aondoke ifikapo 2020, tunalazimika kumbebesha Tundu Lissu bendera ya CHADEMA, na SI mwingine. Kwa TL, kichaa lazima asepe.
 
Hivi huko uvccm huwa hamuwezi kutofautisha kati ya kuponda na kushauri au kati ya kupinga na kushauri? au basi tu kwa kuwa aliyetoa mawazo sio wa upande wako basi unaliona kwa njia tofauti
 
Back
Top Bottom