Of course, mleta mada amegundua sasa kwa sababu ndicho kipindi ambacho Lazaro Nyalandu ameenda Kenya kumjulia hali Tundu Lissu!! Mbaya zaidi, imeripotiwa hivi punde kwamba ni Nyalandu huyo huyo anawasiliana na wafadhili wake ili kuwezesha safari ya Tundu Lissu kupelekwa US!Kwa hiyo ndio mmegundua leo uhujumu uchumi wa maliasili za taifa ulitokea wakati wa Nyalandu na sio kipindi kingine chochote? Kwamba uhujumu uchumi uliowahi kutokea Tanzania ni katika maliasili tu tena wakati Nyalandu akiwa waziri na sio katika sekta au eneo lingine lolote wala katika kipindi kingine chochote katika Tanzania? Ndugu, hizo aina ya siasa mnazotamani kuzipandikiza nchi hii ni hatari sana kuliko bomu la hydrogen.