boniuso
JF-Expert Member
- Mar 13, 2013
- 680
- 852
UKIBADILI NAMNA UNAVYO TAZAMA VITU NA VITU UNAVYOTAZAMA HUBADILIKA
Kinachotokea sio tatizo ila tafsiri unayoweka juu yake ndio inaweza kuuwa tatizo
Kikwazo chochote kinachotokea huwa kinakuja kuboresha sehemu ya maisha yetu
Usitazame vikwazo kwa ubaya wake tazama vikwazo kwa mazuri yake
Kila kitu hutokea kwa sababu na ikiwa hujui sababu bado sababu ipo
Watu huwa wanahukumu matokeo badala ya kuuliza sababu ya matokeo husika
Ukiona matokeo yeyote yawe mazuri au mbaya tambua kuwa zipo sababu nyuma yake
Usipojua sababu ya matokeo fulani huwezi kurekebisha dosari za matokeo husika
Watu wengi huwa wanalaumu wenzao kwa maamuzi wamefanya au hawakufanya ila hawana muda kujua siri iliyopo nyuma ya pazia
Usiwe kama watu wengi ukiona matokeo huyaelewi uliza sababu ya matokeo hayo bila kutoa hukumu haraka
Kufikiri ni kazi sana ndio sababu watu wenye wanahukumu haraka
Usihukumu jambo kwa kuangalia upande wako limeathiri kiasi gani bali angalia jambo kupitia upande wa tatizo
Ukiangalia maumivu unayopitia utaona haustahili kupata maumivu lakini ukiangalia kosa lako au fundisho lenye kupatikana katika maumivu hayo utaona sehemu ya kurekebisha
Ikiwa huoni unapokosea huwezi kujirekebisha na utapata matokeo yaleyale
Binadamu hawezi kujifunza anapoamini anajua tayari
Unaweza kupoteza uwapendao,unaweza kupoteza fedha, unaweza kupoteza kazi,unaweza kutengwa,unaweza kunyimwa misaada katika dhiki,unaweza kupewa ahadi na zikavunjwa ila yote hutakiwi kusema kwanini napatikana na haya
Badala yake jiulize chanzo cha hayo yote ni kitu gani
Ukijua chanzo cha tatizo unaweza kukabiliana na tatizo
Usipojua chanzo cha matatizo ni vigumu kukabiliana na matatizo kwa sababu huwezi kujua wapi sahihi pa kuanzia
Wengi wakipata ugumu kwenye maisha huona kama hawastahili kupata ugumu huo
Ukweli ni kuwa matatizo huwa yanakuja yenyewe wala hayana mualiko
Furahia haiwezi kujileta yenyewe hivyo usipotafuta sababu ya kufurahi huwezi kufurahia maisha yako
Bila kujali nini umefanya au hukufanya mpaka umefika hapo ulipo huna sababu ya kujichukia kwa uamuzi ulifanya au hukufanya
Siku mbaya zinakupa kukupa masomo na siku nzuri zinakupa kumbukumbu za furaha
Huwezi kuthamini ushindi bila kushindwa
Huwezi kuthamini afya bila maradhi
Huwezi kuthamini upendo wa dhati bila kupata usaliti
Huwezi kuthamini akiba bila kuona madhara ya kutoweka akiba
Hivyo kila kitu hutokea kwa sababu
Usifanye siku mbaya kama vile maisha yako yote ni mabaya
Hakuna binadamu ambaye hafanyi makosa hivyo kukosea ni kawaida sana
Ikiwa unapitia kipindi kigumu kumbuka kuwa kuna mtu tayari amepitia nyakati ngumu hapo awali na aliweza kuvuka hivyo jiulize aliweza vipi kuvuka kisha na wewe vuka
Kurudia kumbukumbu za maisha ya zamani kila wakati mpaka unaona maisha ya zamani pekee ndio yalitakiwa kudumu ni kupoteza muda
Huwezi kufurahia maisha ikiwa unaona maisha ya miaka ya nyuma ndio mazuri huku ya sasa unaona hukustahili kuishi
Hakuna maisha yenye kudumu
Ukiona upo kwenye furaha ujue matatizo yapo njiani na ukiona maisha ni magumu sana ujue nafuu ipo njiani
Maisha siku zote ni mfululizo wa matatizo kama mawimbi ya bahari
Kwa maana mawimbi yapo makubwa kwa madogo lakini haiwezekani mawimbi kukosekana baharini
Fursa ni kama dala dala ikikupata moja nyengine ipo njiani
Ukitazama sana fursa umepoteza utaona wewe ni mbaya sana,mwenye mikosi,asiwe na jema n.k lakini kutazama mabaya tu katika maisha yako huzidisha maumivu
Huwezi kujisikia vizuri wakati muda wote unakumbuka matatizo yako badala ya mazuri yako
Hauna matatizo yote ya ulimwengu hivyo tabasamu
Wakati mwengine utapoteza watu ambao uliamini kuwa hao ndio wangefanya maisha yako kuwa mazuri
Kuna wakati unaweza kupoteza kazi nzuri ambayo unaona kama kazi pekee duniani ambayo bila kazi hiyo huwezi kuishi
Kuona maisha yako yatakuwa magumu sana kwa sababu huna kitu fulani au kwa sababu umepoteza mtu au kitu muhimu kutazidisha maumivu kwako
Huwezi kufurahia maisha ikiwa unaona matatizo yako muda wote
Tazama mafunzo katika kila ugumu usitazame kwa nini wewe ndio unapata ugumu huo
Hakuna mtu mwenye mahusiano yenye furaha saa 24,wala mwenye kujiamini kwa 100% kila binadamu huwa anatilia shaka uwezo wake na kipaji chake pale haoni matokeo mazuri huku juhudi ameweka kubwa sana
Kumbuka mafanikio hupimwa kwa mchakato sio matokeo
Ukipima mafanikio kwa matokeo utakata tamaa haraka sana
Huwezi kudhibiti matokeo bali unaweza kuongeza au kupunguza juhudi zako
Kupata kitabu cha
1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)
3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy)
4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)
6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)
+255766862579
+255622414991
Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam
Kinachotokea sio tatizo ila tafsiri unayoweka juu yake ndio inaweza kuuwa tatizo
Kikwazo chochote kinachotokea huwa kinakuja kuboresha sehemu ya maisha yetu
Usitazame vikwazo kwa ubaya wake tazama vikwazo kwa mazuri yake
Kila kitu hutokea kwa sababu na ikiwa hujui sababu bado sababu ipo
Watu huwa wanahukumu matokeo badala ya kuuliza sababu ya matokeo husika
Ukiona matokeo yeyote yawe mazuri au mbaya tambua kuwa zipo sababu nyuma yake
Usipojua sababu ya matokeo fulani huwezi kurekebisha dosari za matokeo husika
Watu wengi huwa wanalaumu wenzao kwa maamuzi wamefanya au hawakufanya ila hawana muda kujua siri iliyopo nyuma ya pazia
Usiwe kama watu wengi ukiona matokeo huyaelewi uliza sababu ya matokeo hayo bila kutoa hukumu haraka
Kufikiri ni kazi sana ndio sababu watu wenye wanahukumu haraka
Usihukumu jambo kwa kuangalia upande wako limeathiri kiasi gani bali angalia jambo kupitia upande wa tatizo
Ukiangalia maumivu unayopitia utaona haustahili kupata maumivu lakini ukiangalia kosa lako au fundisho lenye kupatikana katika maumivu hayo utaona sehemu ya kurekebisha
Ikiwa huoni unapokosea huwezi kujirekebisha na utapata matokeo yaleyale
Binadamu hawezi kujifunza anapoamini anajua tayari
Unaweza kupoteza uwapendao,unaweza kupoteza fedha, unaweza kupoteza kazi,unaweza kutengwa,unaweza kunyimwa misaada katika dhiki,unaweza kupewa ahadi na zikavunjwa ila yote hutakiwi kusema kwanini napatikana na haya
Badala yake jiulize chanzo cha hayo yote ni kitu gani
Ukijua chanzo cha tatizo unaweza kukabiliana na tatizo
Usipojua chanzo cha matatizo ni vigumu kukabiliana na matatizo kwa sababu huwezi kujua wapi sahihi pa kuanzia
Wengi wakipata ugumu kwenye maisha huona kama hawastahili kupata ugumu huo
Ukweli ni kuwa matatizo huwa yanakuja yenyewe wala hayana mualiko
Furahia haiwezi kujileta yenyewe hivyo usipotafuta sababu ya kufurahi huwezi kufurahia maisha yako
Bila kujali nini umefanya au hukufanya mpaka umefika hapo ulipo huna sababu ya kujichukia kwa uamuzi ulifanya au hukufanya
Siku mbaya zinakupa kukupa masomo na siku nzuri zinakupa kumbukumbu za furaha
Huwezi kuthamini ushindi bila kushindwa
Huwezi kuthamini afya bila maradhi
Huwezi kuthamini upendo wa dhati bila kupata usaliti
Huwezi kuthamini akiba bila kuona madhara ya kutoweka akiba
Hivyo kila kitu hutokea kwa sababu
Usifanye siku mbaya kama vile maisha yako yote ni mabaya
Hakuna binadamu ambaye hafanyi makosa hivyo kukosea ni kawaida sana
Ikiwa unapitia kipindi kigumu kumbuka kuwa kuna mtu tayari amepitia nyakati ngumu hapo awali na aliweza kuvuka hivyo jiulize aliweza vipi kuvuka kisha na wewe vuka
Kurudia kumbukumbu za maisha ya zamani kila wakati mpaka unaona maisha ya zamani pekee ndio yalitakiwa kudumu ni kupoteza muda
Huwezi kufurahia maisha ikiwa unaona maisha ya miaka ya nyuma ndio mazuri huku ya sasa unaona hukustahili kuishi
Hakuna maisha yenye kudumu
Ukiona upo kwenye furaha ujue matatizo yapo njiani na ukiona maisha ni magumu sana ujue nafuu ipo njiani
Maisha siku zote ni mfululizo wa matatizo kama mawimbi ya bahari
Kwa maana mawimbi yapo makubwa kwa madogo lakini haiwezekani mawimbi kukosekana baharini
Fursa ni kama dala dala ikikupata moja nyengine ipo njiani
Ukitazama sana fursa umepoteza utaona wewe ni mbaya sana,mwenye mikosi,asiwe na jema n.k lakini kutazama mabaya tu katika maisha yako huzidisha maumivu
Huwezi kujisikia vizuri wakati muda wote unakumbuka matatizo yako badala ya mazuri yako
Hauna matatizo yote ya ulimwengu hivyo tabasamu
Wakati mwengine utapoteza watu ambao uliamini kuwa hao ndio wangefanya maisha yako kuwa mazuri
Kuna wakati unaweza kupoteza kazi nzuri ambayo unaona kama kazi pekee duniani ambayo bila kazi hiyo huwezi kuishi
Kuona maisha yako yatakuwa magumu sana kwa sababu huna kitu fulani au kwa sababu umepoteza mtu au kitu muhimu kutazidisha maumivu kwako
Huwezi kufurahia maisha ikiwa unaona matatizo yako muda wote
Tazama mafunzo katika kila ugumu usitazame kwa nini wewe ndio unapata ugumu huo
Hakuna mtu mwenye mahusiano yenye furaha saa 24,wala mwenye kujiamini kwa 100% kila binadamu huwa anatilia shaka uwezo wake na kipaji chake pale haoni matokeo mazuri huku juhudi ameweka kubwa sana
Kumbuka mafanikio hupimwa kwa mchakato sio matokeo
Ukipima mafanikio kwa matokeo utakata tamaa haraka sana
Huwezi kudhibiti matokeo bali unaweza kuongeza au kupunguza juhudi zako
Kupata kitabu cha
1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)
3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy)
4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)
6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)
+255766862579
+255622414991
Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam