NUTAS iliishia wapi?

ZeMarcopolo

Platinum Member
May 11, 2008
14,017
7,220
Mwishoni mwa miaka ya 90 viongozi wa wanafunzi wa vyuo Tanzania walianzisha wazo zuri la kuunda chama cha wanafunzi wote Tanzania kuanzia shule za msingi mpaka vyuo vikuu (NUTAS - National Union of Tanzanian Students Associations).

Draft constitution ilitengenezwa halafu ukachaguliwa uongozi wa muda uliopewa jukumu la kukamilisha utengenezaji wa katiba.Miongoni mwa viongozi hao ni wana JF kadhaa. Baada ya hapo habari za NUTAS hazikusikika tena!!!

Matumaini niliyoyaona kwenye NUTAS ni kwamba kingeweza kuwa chombo chenye ushawishi mkubwa wa kutetea maslahi ya wanafunzi na kuepusha migomo ambayo kwenye vyuo vingi vya serikali imekuwa ni kama sehemu rasmi ya ratiba.

Je ni nini kiliisibu mikakati ya kuanzisha NUTAS.
 
siwezi kuamini kama forum nzima haina hata mwanachama mmoja na NUTAS....wazee mpooo ?? naombeni mjitokeze !!
 
siwezi kuamini kama forum nzima haina hata mwanachama mmoja na NUTAS....wazee mpooo ?? naombeni mjitokeze !!


Wapo ila nimeshaona dalili kuwa hawako proud na kilichotokea. Wangekuwa na wakumlaumu wangekuwa washamwaga milawama kibao tu. Kabla ya kulaumu utendaji wa wengine jamani tujipime na sisi je tunatimiza majukumu tuliyoyakubali toka kwa jamii?
 
Kama hawataki kujitokeza,, then tutaanza kutajana majina na shule tulizotoka humu ohooo; Tunauliza tena.....Vijana Mpoooo???
 
Kama hawataki kujitokeza,, then tutaanza kutajana majina na shule tulizotoka humu ohooo; Tunauliza tena.....Vijana Mpoooo???

Hicho nadhani ndio tutakacholazimika kufanya.
Mzee wa UK upo, au umekamatwa tena na polisi?
 
Haya na kule nyanda za juu mashariki (Boston) vipi hadi majina mshkaji; RN atakuruhusu kuja kutupa mawili matatu....Au mtume mtu basi atupe updates....
 
Mbunge wa madini tutakuelewa iwapo uko busy na mandalizi ya bunge la bajeti. Ila ukipata kamuda tafadhali NUTAS na zile pesa za wafadhili zimeishia wapi?
 
Naona hata shirika la simu bongo (Celtel) kitengo cha Mauzo wanaweza kutoa tamko lao kuhusiana na hili.
 
Mama wa maendeleo ya jamii, vipi mbona kimya? Ile barua mliyoahidi kututumia mbona haifiki, tuendelee kusubiri?
 
Bussiness Times; maarufu sana kwa kuandika articles; ingekuwa vizuri sana wakatuwekea hili katika articles zao...Maana wana waandishi wanalifahamu hili vilivyo.
 
Bussiness Times; maarufu sana kwa kuandika articles; ingekuwa vizuri sana wakatuwekea hili katika articles zao...Maana wana waandishi wanalifahamu hili vilivyo.

Yakhe na nyinyi Unguja huko vipi? au mlibadilisha kibao mkaanza mikakati ya kuanzisha NUZAS? Naona siku hizi ndevu umeamua kunyoa zote, kulikoni?
 
Yakhe na nyinyi Unguja huko vipi? au mlibadilisha kibao mkaanza mikakati ya kuanzisha NUZAS? Naona siku hizi ndevu umeamua kunyoa zote, kulikoni?
Walijaribu mimi sikuwemo lakini, walikoishia sijui, ila naweza nikakuelekeza kwa mtu ambaye anafahamu vizuri wapi waliishia na mikutano yao na kumuogopa Komando Salmini; ......Alwatani wangu wa Reading....Mnyamazishe mdau huyu naona anafukuafukua mengi...

Mimi naweka za sunna tu, ndo ishara ya ubeberu kikwetu, 'sifungui mjadala kuhusiana na hilo lakini'
 
Walijaribu mimi sikuwemo lakini, walikoishia sijui, ila naweza nikakuelekeza kwa mtu ambaye anafahamu vizuri wapi waliishia na mikutano yao na kumuogopa Komando Salmini; ......Alwatani wangu wa Reading....Mnyamazishe mdau huyu naona anafukuafukua mengi...

Mimi naweka za sunna tu, ndo ishara ya ubeberu kikwetu, 'sifungui mjadala kuhusiana na hilo lakini'

Kuna mjanja mmoja alikuwa kwenye harati kama za NUTAS halafu akachagua upande mzuri wa coin, sasa hivi kapewa jukumu la kuhakikisha mipaka ya nchi iko salama.

Kuna mwingine alifichwa kwa miezi sita, aliporudi amekuja na gia eti yeye mpinzani! Nikiangalia huwa nacheka sana jinsi watu wanavyochezeana akili.Nikisema kuna vyama feki watu wanasema mimi SIPENDI UPINZANI, kumbe mimi najaribu kuwa-alert tu.

Ila hapa nilipo nacheka jinsi watu walivyoamua kuuchuna kama wamemwagiwa maji ya barafu.
 
Ndio hivyo lakini mkuu pengine ilikuwa ni mojawapo ya masharti ya kupiga chini mkakati; "Tukishaondoka hapa tusisikie mtu anaongelea tena kuhusu hili, ni kuuchuna tu".
 
Kuna mjanja mmoja alikuwa kwenye harati kama za NUTAS halafu akachagua upande mzuri wa coin, sasa hivi kapewa jukumu la kuhakikisha mipaka ya nchi iko salama.

Kuna mwingine alifichwa kwa miezi sita, aliporudi amekuja na gia eti yeye mpinzani! Nikiangalia huwa nacheka sana jinsi watu wanavyochezeana akili.Nikisema kuna vyama feki watu wanasema mimi SIPENDI UPINZANI, kumbe mimi najaribu kuwa-alert tu.

Ila hapa nilipo nacheka jinsi watu walivyoamua kuuchuna kama wamemwagiwa maji ya barafu.

...Naona wanabodi wameamua kukausha au labda hawakusoma hapa bongo...
Nilikuwa mwanafunzi enzi hizo ila sikuwahi kuwa close na hivi vitu, unajue kipindi kile wengine hatukuwa wanafunzi nadharia maana kila kukicha zilikuwa zinakuja sera zisizotekelezeka hasa ktk masuala ya elimu hivyo wengine tukajikita kusaka elimu na mambo ya ukada tukawaachia wapepetaji....


enewei mkuu mwaga Dataz. Kina nani hao na kwa nini unadhani wanabodi wameamua kuuchuna???
 
Mimi na Zema...tunajaribu kuwabipu ili angalau wajue kama bado tunakumbuka, lakini we waache tu, tutaanza kutaja na shule watokazo, then vyeo vyao, halafu yatafuata majina kamilikamili hapa.
NASEMA TENA VIJANA MPOO?
Haya Moja......mbili.....tatu.....ikifika kumi tunaongeza data moja zaidi, au unasemaje Zemarcopolo?
Hatutonyamaza hadi watoe tamko..
 
Inaonenaka hata Zemarcopolo naye anawaachia hawa jamaa...Sasa mimi naanza na hili...
kama unajijua ulisoma Azania form V na VI mwaka 1995 na 96 ulifanya NECTA May 1997 ukapata DIV 2 ya point 11 halafu ukaenda UD sijui ulifikajefikaje lakini....Ukawa unaenda pale bwenini na majigambo makubwaa eti uko UD injiniaring ukiwa na 110 nyeupe yenye namba zinazoanzia na SU 7xxxx, sasa hivi uko TANROADS kitengo cha maendeleo.....please tuambie yale mafaili ya nukuu za mikutano yako wapiii????
 
Inaonenaka hata Zemarcopolo naye anawaachia hawa jamaa...Sasa mimi naanza na hili...
kama unajijua ulisoma Azania form V na VI mwaka 1995 na 96 ulifanya NECTA May 1997 ukapata DIV 2 ya point 11 halafu ukaenda UD sijui ulifikajefikaje lakini....Ukawa unaenda pale bwenini na majigambo makubwaa eti uko UD injiniaring ukiwa na 110 nyeupe yenye namba zinazoanzia na SU 7xxxx, sasa hivi uko TANROADS kitengo cha maendeleo.....please tuambie yale mafaili ya nukuu za mikutano yako wapiii????

Huyo alikabidhiwa mafaili na mzee wa Applied Social Psychology ambaye alifundisha pugu kabla ya kwenda mlimani na sasa ananyemelea udaktari huko Uingereza. Kaka vipi mbona umeamua kuuchuna juu ya hili? Unanipa wasiwasi katika swala zima la intergrity. Kila siku unaingia hapa JF mbona hili swali umeamua kulidiss, au nalo hujalielewa???
Nimshathibitisha kuwa haupo kituo cha polisi wala hujashikiliwa na chombo chochote cha dola kwa hiyo njoo utoe majibu, tafadhali.
 
Back
Top Bottom