Nusrat Hanje kaonyesha kwanini vijana wa upinzani wanateulika zaidi

Oct 13, 2018
35
259
Na Thadei Ole Mushi.

Vijana wengi wa CCM ni vigumu kupimika kwa kuwa hata kwa wateuzi hawajui vijana hawa Wana uwezo Gani kwa kuwa mtindo wao ndani ya Chama hauwapi Fursa ya kuonyesha Wanajua nini.

Vijana wa CCM wamekumbwa na jini la kusifia kuanzia asubuhi hadi jioni as long as Kiongozi wake kasema au yupo Mbele yake.

Leo kwenye Mkutano wa Mama SAMIA alioongea na vijana hata wale waliopewa Fursa ya kuizungumza Mbele ya Rais na mawaziri wake wameshindwa ku address shida zao na wakaishia kusifia aidha kumsifia Rais au kusifia Miradi inayotekelezwa na Serikali.

Ni katika Mkutano huo vijana wameshindwa kumweleza Rais kuhusu shida ya Ajira kwa vijana na kwa data zilizopo ni Kuwa vyuo vikuu na vyuo vya Kati kila mwaka humwaga wahitimu mtaani zaidi ya 600,000 huku wanaofanikiwa kupenya kwenye Soko la ajira wakiwa 50,000 tu.

Au vijana mmesahau?Tarehe 13/06/2014 Vijana zaidi ya elfu 10,000 walijitokeza kuomba ajira wizara ya mambo ya ndani (Uhamiaji) nafasi 70 tu na hawakuzipata. Tarehe 12/12/2014 vijana zaidi ya 10,000 walijitokeza kuomba nafasi 50 za kazi TRA. Hii nayo mnaikumbuka. Sio haya wangelitakiwa kuongea na Mama?

Ni Vijana hawa hawa wameshindwa kumwambia Rais kuwa Kuna Fursa za kiteknolojia zinadidimizwa na Waziri wake kwa kushindwa kushusha Bei za Mabando, kushindwa kuruhusu vijana kufungua online tv, kushindwa kuruhusu vijana wapiga picha kushindwa kupiga picha kwa Drones hadi walipie na sasa wameletewa Kodi ya Vifurushi vya simu. Na eneo Hili ni muhimu sana katika kujiajiri....

Ni vijana hawa hawa wameshindwa kuomba mikopo ya vyuo vikuu inayokatwa asilimia 15 ipunguzwe.... Ili angalau wanachokipata wale walioajiriwa wanufaike nacho.

Ni Vijana hawa hawa wameshindwa kumuomba Rais aongeze mikopo kwenye Halmashauri zetu hasa ile inayohusu vijana.

Ni vijana hawa hawa wameshindwa kumwomba Rais kwa vijana wanaoshighulika na Kilimo angalau riba ya kuingiza pembejeo zipunguzwe ili kuvutia wengi kujiingiza kwenye Kilimo kama sehemu ya kupambana na tatizo la ajira.

Vijana wanasubiri Nani awasemee? Matatizo yao ni Mengi Sana Ila Nani awasemee....

Mkutano wa vijana na Rais ulitangazwa muda Mrefu kwa nini hawakujiandaa kwenda kumweleza Rais shida zao na way foward?

Nusrat Hanje kaibuka Tena kidedea Mbele ya Vijana wa CCM. Naanza Kuelewa kwa nini JPM alikuwa akichukua vijana wa Upinzani na kuwapa madaraka. Hakuna Zoezi gumu kama la kupima uelewa wetu sisi vijana wa CCM. Tunawapa tabu Sana wazee wa Vetting 😂😂😂😂.

Walichofanikiwa ni Suti walizovaa ziliwapendeza.

Ole Mushi
0712702602

images (13).jpeg
 
Yaani ulivyoandika ni kama vile wote wamemsikiliza huyo Hanje.

Anyway, kumbe na wewe ni CCM vile vile.
 
Dada kaongelea vijana kuwa na jukwaa moja la kitaifa lisilojali vyama wanavyotoka.

Kaongelea vijana kuwa wamoja ili wanachokiongea au kukitaka kifanyike kiwe na msingi wa umoja.
 
Alichokifanya Hanje ni kupaza tu sauti iliyopuuzwa kwa muda mrefu, suala la Jukwaa la Vijana lishaongelewa sana hasa katika Serikali ya awamu ya nne. Labda umpe sifa kwa kukumbushia hilo.

Kuhusu hao vijana wa CCM unaowashtumu sidhani kama una uhalali wa kufanya hivyo hasa ukizingatia nawe ni walewale, pengine usichonacho ni jukwaa tu la kusimamia kama hao wenzako.

Kuna wakati ulikuwa unahimiza watu wa Kilimanjaro wachague Wabunge kutoka CCM tupu ili mkoa ukumbukwe na Rais Magufuli. Kwa akili za hivi huwezi jitofautisha na hao unaowanyooshea kidole.
 
Uviko hata waongee point gani,mapokeo kwa jamii si mazuri.

Kama vipi muwambie UVIKO 19 waitishe mkutano kama wataungwa mkono.
Mnyika kama alisaini fomu zakwenda bungeni good.

Hao na sabaya hawana tofauti,mda utafika tu hata huku mitaani watapigwa mitama kwa usaliti
 
UVCCM ndio wanasababisha matatizo mengi sana ya vijana kutokutatuliwa kwasababu ya kushindwa kutumia nafasi yao ambayo ni muhimu sana..
Kweli inabidi wabadilike au tubadilike maana vijana, wamama na wababa wa Leo wengi ni wasomi na siyo watu wa wakupewa maneno ya kisiasa bila vitendo.

Zaidi wasipoona maendeleo watamuangalia Raisi hivyo Vijana kama nguvu kazi ya kuona haraka ilitakiwa Leo waje na maono hata ya kujitolea kwenye miradi iliyosemwa na serikali iwaandalie fungu la kazi na sehemu za kulala.

Mfano hizo shule kila Kata na zahanati, masoko ya chinga wangeomba maeneo ya kudumu na kujenga wenyewe vyumba vizuri, stendi za pikipiki na bajaji maana wanashinda juani.

Sasa Leo tumeshindwa kuonyesha nguvu zetu vijana kwa Taifa na sisi tukabaki kuwa wakusindikiza wabunge wanaokuja kuomba Kura kwetu na ahadi zao tushazipima Ila tunasubiri matokeo yao kama watatimiza.
 
Nakubaliana na wewe vijana leo hawakuwa wamejipanga kwa lolote zaidi ya zawadi ya ng'ombe jike na dume kwa Mama

Dakika mbili alizotumia Nusrat ni nafasi kubwa sana ya kuongea hoja angalau tatu mbele ya Rais na si kuishia kuomba baraza la Taifa la vijana ambalo miaka mingi ndio imekuwa hoja ya vijana.

Kuanzia wasanii walio perform mbele ya Mama walitakiwa kuwa na nyimbo maalumu zilizobeba ujumbe unaopenyeza matatizo yanayowakabili vijana katika nyanja mbalimbali.

Watu serious wakipewa jukwaa hawalitumii kuimba mapenzi mbele ya Rais. Kina Bob Marley wasingekubalika na wapigania uhuru Kama wangeimba mapenzi mbele ya viongozi.

Msanii unapopewa jukwaa maalumu mbele ya jamii pamoja na kuburudisha lazima utoe ujumbe kwa Rais.

Na hii si leo tu, wasanii wote hawajui wa perform nini kwenye majukwaa maalumu Kama haya. Hii inaweza kuwa tafsiri ya kukosa ubunifu.

Ukiingia kwa undani zaidi utagundua Kama Taifa tuna tatizo mahali.

Vijana hawaandaliwi ipasavyo mashuleni na jamii inayowazunguka.

Nusrat kwa nafasi aliyopata angeweza ku present angalau hoja tatu Kama angekuwa ameziandika mapema. Kuongea mbele ya kiongozi mkuu si Jambo dogo hivyo ni risk kubwa kupanda jukwaani bila chochote ulichoandika. Ndiomaana utaona ametumia muda mrefu kurudia rudia jambo hilo hilo moja la baraza la vijana.

Wote waliopanda jukwaani naamini walipewa taarifa mapema na waliandaliwa na wazee wa protocal hivyo walikuwa na nafasi nzuri ya kuandaa hoja za kuongea zaidi ya kuimbisha watu sijui wakagongee vitu gani.

Vijana wengi wasomi wana degree kwenye vyeti lakini wameshindwa kuzihifadhi kichwani ili waweze kuzitumia kwenye mazingira yanayowazunguka.
 
Yaani vijana wetu hawa wanachoweza zaidi ni kuselebuka, badala ya kushauri serikali na kumwaga NONDO, na kutoa ushauri mzuri wa nini kinapaswa kufanywa kwa mstakabali wa vijana na taifa, badala ya kuishia kila siku kufanya mapambio ushabiki wa kisiasa kama wa Simba vs Yanga, na ndo maana hata Mama kaona tatizo na kawapa angalizo....
 
Back
Top Bottom