MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,129
- 22,030
NUSRAT HANJE: BARAZA LA VIJANA NI KUONGEZA TU GHARAMA KWA TAIFA.
Wakuu natumaini mko vizuri.
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi.. kwa pamoja mjibu "CHAMA KIENDELEE!!!"... Kwa mara nyingine nimeona nitumie akili hii kubwa niliyojaliwa na muumba kutoa maoni yangu kwenye hili jambo la kitaifa. Najivunia mawazo yangu mbalimbali kufanyiwa kazi na serikali zilizokuwepo madarakani tangu kuwepo JF. Ila naomba wale wote ambao mmekuwa mkinipigia sana simu ba kunitumia ujumbe mfupi kunisihi nitoe maoni yangu kila linapojitokeza jambo la kitaifa msiwe mnafanya hivyo kwasababu hata mimi huwa naona yanayoendelea ila muda unakuwa umebana. Pia saa nyingine inaweza tatizo inaweza isiwe muda kwasababu nimejiwekea utaratibu kwamba nikiona kuna akili kubwa nyingine ishatoa maoni niliyotaka kutoa basi huwa nakaa kimya.
Majuzi hapa wakati wa mkutano wa Mheshimiwa Rais na vijana huko Mwanza kulijitokeza maoni toka kwa mbunge kijana wa CHADEMA, Mh Nusrat Hanje. Kapendekeza kuwepo baraza la vijana la taifa. Kwangu mimi ni wazo zuri tu la kisiasa. Nampongeza sana Nusrat kama mwanasiasa wa CHADEMA kutoa hoja isiyo na upande wowote. Kisiasa itamsaidia yeye pamoja na chama chake. Kimsingi Nusrat amekiinua sana CHADEMA kwenye ule mkutano. Angalau alipunguza uhaba wa hoja nzuri mitandaoni baada ya makada waandamizi kudandia mambo yasiyo na uzito kama hili la Diamond na BET.
Nimesema hoja ya Nusrat ni ya kisiasa kwa sababu mbalimbali nilizoziona. Kwanza ili baraza liwepo lazima taifa liingie gharama za uendeshaji kama vile ofisi, magari, mishahara ya watumishi na gharama zingine zinazohusiana. Lakini kutakuwa na faida itakayotokana na baraza baada ya kuingia gharama zote? Kiukweli binafsi sioni faida yoyote kwa vijana wengi wa taifa hili kunufaika zaidi ya wachache kama kina Nusrat kuja kuwa viongozi wa hilo baraza. Na kwa siasa zetu baraza linaweza kuja kuwa baraza la wazee kwenye baraza la vijana. Yaani wale vijana wenye miaka 40 na kuendelea. Tukiachana na hoja ya gharama turudi nyuma na kujiuliza je, mabaraza kama UVCCM, BAVICHA na mengine ya vijana yameshawahi kuwa na faida yoyote kabla ya kuunda lingine? Haya mabaraza ya vyama yamekuwa na kazi zaidi ya kutetea kila linalowahusu wenyeviti wa vyama vyao na ni nadra sana kuona wanajitokeza kutetea vijana wenzao hadharani. Kijana wa kitanzania leo hii anatoka chuo akiwa na Invoice ya HESLB ikimdai mamilioni kabla ya kupata ajira yoyote. Vijana leo hii hawana unafuu wowote wanapotaka kufungua biashara zao. Kibano kutoka mamlaka ya kodi, taasisi za fedha, serikali za mitaa ni kilekile.. hakuna unafuu wowote kwa kijana aliyetoka shule. Sasa hivi tulipofikia ni kamba ajira ambayo sio rasmi lakini vijana wanaitaka ni kuwa "chawa" wa Nusrat na watu wengine wenye unafuu wa maisha.
Mimi nadhani tuachane na hizi habari za kujiongezea mzigo kwa kuunda hili baraza. Nusrat na wabunge wengine vijana waliopo bungeni wajikite kuchochea mabadiliko ya sheria zote ambazo zinambana kijana. Pia watunge zingine za kumsaidia kijana kujinasua kwenye ufukara. Hizo gharama za kuunda baraza mpeni hata Shishi baby aongeze mgahawa mwingine tufaidi biriani.
NB: nimeweka picha ya wajumbe kwenye mkutano mkuu wa chipukizi UVCCM, December 2019 ili tujikumbushe.. hao ndo chipukizi UVCCM... Tbt 🤣
Wakuu natumaini mko vizuri.
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi.. kwa pamoja mjibu "CHAMA KIENDELEE!!!"... Kwa mara nyingine nimeona nitumie akili hii kubwa niliyojaliwa na muumba kutoa maoni yangu kwenye hili jambo la kitaifa. Najivunia mawazo yangu mbalimbali kufanyiwa kazi na serikali zilizokuwepo madarakani tangu kuwepo JF. Ila naomba wale wote ambao mmekuwa mkinipigia sana simu ba kunitumia ujumbe mfupi kunisihi nitoe maoni yangu kila linapojitokeza jambo la kitaifa msiwe mnafanya hivyo kwasababu hata mimi huwa naona yanayoendelea ila muda unakuwa umebana. Pia saa nyingine inaweza tatizo inaweza isiwe muda kwasababu nimejiwekea utaratibu kwamba nikiona kuna akili kubwa nyingine ishatoa maoni niliyotaka kutoa basi huwa nakaa kimya.
Majuzi hapa wakati wa mkutano wa Mheshimiwa Rais na vijana huko Mwanza kulijitokeza maoni toka kwa mbunge kijana wa CHADEMA, Mh Nusrat Hanje. Kapendekeza kuwepo baraza la vijana la taifa. Kwangu mimi ni wazo zuri tu la kisiasa. Nampongeza sana Nusrat kama mwanasiasa wa CHADEMA kutoa hoja isiyo na upande wowote. Kisiasa itamsaidia yeye pamoja na chama chake. Kimsingi Nusrat amekiinua sana CHADEMA kwenye ule mkutano. Angalau alipunguza uhaba wa hoja nzuri mitandaoni baada ya makada waandamizi kudandia mambo yasiyo na uzito kama hili la Diamond na BET.
Nimesema hoja ya Nusrat ni ya kisiasa kwa sababu mbalimbali nilizoziona. Kwanza ili baraza liwepo lazima taifa liingie gharama za uendeshaji kama vile ofisi, magari, mishahara ya watumishi na gharama zingine zinazohusiana. Lakini kutakuwa na faida itakayotokana na baraza baada ya kuingia gharama zote? Kiukweli binafsi sioni faida yoyote kwa vijana wengi wa taifa hili kunufaika zaidi ya wachache kama kina Nusrat kuja kuwa viongozi wa hilo baraza. Na kwa siasa zetu baraza linaweza kuja kuwa baraza la wazee kwenye baraza la vijana. Yaani wale vijana wenye miaka 40 na kuendelea. Tukiachana na hoja ya gharama turudi nyuma na kujiuliza je, mabaraza kama UVCCM, BAVICHA na mengine ya vijana yameshawahi kuwa na faida yoyote kabla ya kuunda lingine? Haya mabaraza ya vyama yamekuwa na kazi zaidi ya kutetea kila linalowahusu wenyeviti wa vyama vyao na ni nadra sana kuona wanajitokeza kutetea vijana wenzao hadharani. Kijana wa kitanzania leo hii anatoka chuo akiwa na Invoice ya HESLB ikimdai mamilioni kabla ya kupata ajira yoyote. Vijana leo hii hawana unafuu wowote wanapotaka kufungua biashara zao. Kibano kutoka mamlaka ya kodi, taasisi za fedha, serikali za mitaa ni kilekile.. hakuna unafuu wowote kwa kijana aliyetoka shule. Sasa hivi tulipofikia ni kamba ajira ambayo sio rasmi lakini vijana wanaitaka ni kuwa "chawa" wa Nusrat na watu wengine wenye unafuu wa maisha.
Mimi nadhani tuachane na hizi habari za kujiongezea mzigo kwa kuunda hili baraza. Nusrat na wabunge wengine vijana waliopo bungeni wajikite kuchochea mabadiliko ya sheria zote ambazo zinambana kijana. Pia watunge zingine za kumsaidia kijana kujinasua kwenye ufukara. Hizo gharama za kuunda baraza mpeni hata Shishi baby aongeze mgahawa mwingine tufaidi biriani.
NB: nimeweka picha ya wajumbe kwenye mkutano mkuu wa chipukizi UVCCM, December 2019 ili tujikumbushe.. hao ndo chipukizi UVCCM... Tbt 🤣