Nukuu za Katibu wa itikadi na Uenezi CCM wakati akizungumza leo katika Uzinduzi wa Chanjo ya Uviko 19 Ikulu Jijini Dar Es Salaam.
"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hatua hii muhimu ndani ya Taifa letu. CCM inampongeza Mwenyekiti na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 ibara za 83(o) na 84."
"Tuliahidi CCM itaimarisha huduma za Afya kwa watanzania sambamba na kuimarisha mifumo na miundombinu ya kuwakinga dhidi magonjwa ya mlipuko ikiwemo UVIKO-19. Alilofanya Rais Samia leo ni utayari wake na nia yake thabiti katika kuwatumikia watanzania na kuliongoza Taifa. "
"Uongozi ni kuonesha njia ndivyo alivyofanya Rais Samia na ndio maana viongozi na wasaidizi wake tumemuunga mkono kupata chanjo hii ya UVIKO 19 hapa ikulu. Tuwaombe wananchi waendelee kupata taarifa sahihi na wafanye uamuzi sahihi wa kupata chanjo hii. Kinga ni bora kuliko Tiba."
Shaka Hamdu Shaka
Katibu wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi
Ikulu Dar es Salaam
28 Julai 2021.
"Tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa hatua hii muhimu ndani ya Taifa letu. CCM inampongeza Mwenyekiti na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndugu Samia Suluhu Hassan kwa kusimamia kikamilifu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 ibara za 83(o) na 84."
"Tuliahidi CCM itaimarisha huduma za Afya kwa watanzania sambamba na kuimarisha mifumo na miundombinu ya kuwakinga dhidi magonjwa ya mlipuko ikiwemo UVIKO-19. Alilofanya Rais Samia leo ni utayari wake na nia yake thabiti katika kuwatumikia watanzania na kuliongoza Taifa. "
"Uongozi ni kuonesha njia ndivyo alivyofanya Rais Samia na ndio maana viongozi na wasaidizi wake tumemuunga mkono kupata chanjo hii ya UVIKO 19 hapa ikulu. Tuwaombe wananchi waendelee kupata taarifa sahihi na wafanye uamuzi sahihi wa kupata chanjo hii. Kinga ni bora kuliko Tiba."
Shaka Hamdu Shaka
Katibu wa Halmshauri Kuu ya CCM Taifa Itikadi na Uenezi
Ikulu Dar es Salaam
28 Julai 2021.