Nukuu za Katibu Mwenezi CCM Taifa akiongea baada Rais Samia kuwasili akitokea ziara nje ya nchi, Jumapili 20 Februari 2022

budget

Member
Feb 23, 2015
42
27
NUKUU ZA KATIBU MWENEZI TAIFA SHAKA HAMDU SHAKA AKIONGEA BAADA MHE RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUWASILI AKITOKEA ZIARA, JUMAPILI 20 FEBRUARI 2022

" CCM inaridhishwa na juhudi za kisera zitokanazo na upeo, uthubutu na juhudi zinazochukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika medani za Kimataifa" Shaka Mwenezi Taifa

"Kazi inayofanywa na Rais sio ndogo kwani amefanikiwa kuithibitishia dunia msimamo wa taifa, sera za serikali yake kama fahari ya Tanzania na AFRIKA" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia licha ya kuonyesha kwake upeo, maarifa na ufahamu mpana, aliweka bayana msimamo wa nchi yake wenye dhamira ya kudumisha kuendeleza ushirikiano wa kikanda na Kimatafa" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia kila alipopita akikutana na wakuu wa nchi wenzake pia akikutana na makundi mbali mbali na kutoa hotuba za kizalendo akiweka msisitizo wa mashirikiano ya kikanda na kimataifa na kumfanya ajipapambanue Kimatafa" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia ni alama mpya ya Nchi yetu na kioo cha Afrika kwenye medani za kimataifa, amekuwa mchapakazi anayesimamia utekelezaji wa sera zilizomo kwenye ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 bila kuchoka na kwa ujasiri mkubwa" Shaka Mwenezi Taifa

"Chama cha Mapinduzi toka awali hakikukosea kumfanya kuwa Makamo wa Rais na sasa ni Rais. CCM hakina hofu naye hata aliposhika Urais baada ya kifo cha Hayati Dkt Magufuli na kwa jinsi anavyoendelea kuchapakazi amethibitisha kuwa ni kiongozi mwenye uwezo na uelewa huku akimudu vyema kutekeleza majukumu yake na kuonyesha dhamira aliyonayo kwa wananchi wake" Shaka Mwenezi Taifa

"Watanzania wamejawa furaha na matumaini kadri wanavyomuona kiongozi wao akihangaika huku na huku .Amefanikiwa kukubalika kimataifa pia akiaminiwa na jumuiya za kimataifa, taasisi za fedha na mashirika ya kimaendeleo duniani huyu ndio Mama mpambanaji Samia" Shaka Mwenezi Taifa.

"Sera ya Mambo ya nje ya Tanzania imelenga kuendeleza diplomasia ya uchumi baada ya kupata mafanikio makubwa ya kujitangaza kimataifa, kuelezea sera na misimamo yake tokea awamu ya kwanza hadi ya sita" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia amejenga ukaribu na viongozi wa mataifa yenye uchumi imara duniani baada kufanikiwa kukutana na marais wenzake kadhaa kutokana na msingi uliowekwa watangulizi wake" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia itakumbukwa alianza kuzuru nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki kabla hajatembea mataifa ya ulaya na Marekani. Amelihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pia kukutana na jumuiya za kimataifa hakika dhamira yake ya kuifungua nchi katika mawanda ya kidplomasia inakwenda vyema " Shaka Mwenezi Taifa

"Rais hatazuiwa kwenda mahali popote, atafanya hivyo kwa sababu dunia ya sasa si ile ya Rais kujifungia anapaswa kuingia kwenye mawindo ya diplomasia ya uchumi. Ulimwengu wa leo ni kijiji kimoja kinachotegemeana na wala si muda wa kujitenga kazi iendelee" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia amekuwa akishiriki kwenye meza na majukwaa mbalimbali ya majadiliano ya kisiasa, kibiashara na ya kiuchumi kwa manufaa ya watu wake Taifa kutokana na juhudi hizo ameweza kufanikisha na kupata misaada ya fedha za maendeleo ya kisekta ambayo itasukuma mbele sekta za umma kilimo, afya, elimu mazingira, mapambano dhidi ya uviko 19 na mabadiliko ya tabia nchi" Shaka Mwenezi Taifa.

IMG_20220220_182841_062.jpg
 
Haka kabwana nakakubali Sana ila sasa asijekuwa kama J.Malema.

Kwani namuona ana sera za Kitaifa zaidi japo hajajipambanua kiupana wake kwenye mambo ya uchumi na uongozi.

Hata hivyo hongera kwake,CCM ina watu wengi wazuri.
 
Unashindwaje kuwa mzalendo kwa sifa zote hizo anazopewa rais Samia.

#Mama mpambanaji samia
 
"Watanzania wamejawa furaha na matumaini kadri wanavyomuona kiongozi wao akihangaika huku na huku .Amefanikiwa kukubalika kimataifa pia akiaminiwa na jumuiya za kimataifa, taasisi za fedha na mashirika ya kimaendeleo duniani huyu ndio Mama mpambanaji Samia" Shaka Mwenezi Taifa.
Duh!
Siasa na unafiki ni kama uji na mgonjwa!!!
 
Duh!
Siasa na unafiki ni kama uji na mgonjwa!!!
Kwa kweli mm sijajawa na furaha kabisa maana kampuni niliyokuwa nafanya kazi ilikimbia mwaka mmoja baada ya jiwe kuingia madarakani kutokana na kutokuwa na Imani kuhusu uwekezaji wao na mpaka Jana nimeongea nap Wala hawana mpango wa kurudi. Sasa kama Sina kazi naanzaje kujawa na furaha..
 
Kwa kweli mm sijajawa na furaha kabisa maana kampuni niliyokuwa nafanya kazi ilikimbia mwaka mmoja baada ya jiwe kuingia madarakani kutokana na kutokuwa na Imani kuhusu uwekezaji wao na mpaka Jana nimeongea nap Wala hawana mpango wa kurudi. Sasa kama Sina kazi naanzaje kujawa na furaha..
Ndo ajabu..
Badala ya kusema kikundi cha wana ccm kimejawa furaha na matumaini, wanasema watanzania!
 
"Watanzania wamejawa furaha na matumaini kadri wanavyomuona kiongozi wao akihangaika huku na huku .Amefanikiwa kukubalika kimataifa pia akiaminiwa na jumuiya za kimataifa, taasisi za fedha na mashirika ya kimaendeleo duniani huyu ndio Mama mpambanaji Samia" Shaka Mwenezi Taifa.
 
Siasa na unafiki ndani ya ccm ni sawa na bundi na usiku!
Waliokuwa wakimsifu mwendazake na kumpa sifa nyingi kuliko hata Mwenyezi Mungu ndio haohao wanamponda leo!
Haohao ndio wanamsifia mama SSH kwa 'mbeleko na weledi' mkubwa na ndio haohao watakaomponda kesho!
 
NUKUU ZA KATIBU MWENEZI TAIFA SHAKA HAMDU SHAKA AKIONGEA BAADA MHE RAIS SAMIA SULUHU HASSAN KUWASILI AKITOKEA ZIARA, JUMAPILI 20 FEBRUARI 2022

" CCM inaridhishwa na juhudi za kisera zitokanazo na upeo, uthubutu na juhudi zinazochukuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika medani za Kimataifa" Shaka Mwenezi Taifa

"Kazi inayofanywa na Rais sio ndogo kwani amefanikiwa kuithibitishia dunia msimamo wa taifa, sera za serikali yake kama fahari ya Tanzania na AFRIKA" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia licha ya kuonyesha kwake upeo, maarifa na ufahamu mpana, aliweka bayana msimamo wa nchi yake wenye dhamira ya kudumisha kuendeleza ushirikiano wa kikanda na Kimatafa" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia kila alipopita akikutana na wakuu wa nchi wenzake pia akikutana na makundi mbali mbali na kutoa hotuba za kizalendo akiweka msisitizo wa mashirikiano ya kikanda na kimataifa na kumfanya ajipapambanue Kimatafa" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia ni alama mpya ya Nchi yetu na kioo cha Afrika kwenye medani za kimataifa, amekuwa mchapakazi anayesimamia utekelezaji wa sera zilizomo kwenye ilani ya Uchaguzi ya CCM 2020-2025 bila kuchoka na kwa ujasiri mkubwa" Shaka Mwenezi Taifa

"Chama cha Mapinduzi toka awali hakikukosea kumfanya kuwa Makamo wa Rais na sasa ni Rais. CCM hakina hofu naye hata aliposhika Urais baada ya kifo cha Hayati Dkt Magufuli na kwa jinsi anavyoendelea kuchapakazi amethibitisha kuwa ni kiongozi mwenye uwezo na uelewa huku akimudu vyema kutekeleza majukumu yake na kuonyesha dhamira aliyonayo kwa wananchi wake" Shaka Mwenezi Taifa

"Watanzania wamejawa furaha na matumaini kadri wanavyomuona kiongozi wao akihangaika huku na huku .Amefanikiwa kukubalika kimataifa pia akiaminiwa na jumuiya za kimataifa, taasisi za fedha na mashirika ya kimaendeleo duniani huyu ndio Mama mpambanaji Samia" Shaka Mwenezi Taifa.

"Sera ya Mambo ya nje ya Tanzania imelenga kuendeleza diplomasia ya uchumi baada ya kupata mafanikio makubwa ya kujitangaza kimataifa, kuelezea sera na misimamo yake tokea awamu ya kwanza hadi ya sita" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia amejenga ukaribu na viongozi wa mataifa yenye uchumi imara duniani baada kufanikiwa kukutana na marais wenzake kadhaa kutokana na msingi uliowekwa watangulizi wake" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia itakumbukwa alianza kuzuru nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki kabla hajatembea mataifa ya ulaya na Marekani. Amelihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pia kukutana na jumuiya za kimataifa hakika dhamira yake ya kuifungua nchi katika mawanda ya kidplomasia inakwenda vyema " Shaka Mwenezi Taifa

"Rais hatazuiwa kwenda mahali popote, atafanya hivyo kwa sababu dunia ya sasa si ile ya Rais kujifungia anapaswa kuingia kwenye mawindo ya diplomasia ya uchumi. Ulimwengu wa leo ni kijiji kimoja kinachotegemeana na wala si muda wa kujitenga kazi iendelee" Shaka Mwenezi Taifa

"Rais Samia amekuwa akishiriki kwenye meza na majukwaa mbalimbali ya majadiliano ya kisiasa, kibiashara na ya kiuchumi kwa manufaa ya watu wake Taifa kutokana na juhudi hizo ameweza kufanikisha na kupata misaada ya fedha za maendeleo ya kisekta ambayo itasukuma mbele sekta za umma kilimo, afya, elimu mazingira, mapambano dhidi ya uviko 19 na mabadiliko ya tabia nchi" Shaka Mwenezi Taifa.

View attachment 2125191
Mbona hajaongelea suala la ssh kukutana na TL..haoni kama hafanyi kazi yake..soon atakosa kibarua huyu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom