Nukuu niliyoipenda mwaka 2009

Al Zagawi

JF-Expert Member
Mar 17, 2009
2,461
1,446
i. Katika Siasa

  1. ......Katika zama zetu hizi za hadaa, muonekano ndio ukweli na wanaofanya mambo yanayoendana na mantiki na wakaruhusiwa kuendelea kuwa katika nafasi zao ni wachache. Rahisi imekuwa ndiyo sarafu, miigizo imechukua nafasi ya halisi na bazazi sasa ni Imam!....Jenerali Ulimwengu, Raia Mwema, Nov 11-Nov 17,2009
ii. Lugha na fasihi
  1. Elimu ilipokuwa haijulikani duniani mvi zilihesabiwa kuwa alama ya hekima. Fikira hii ilikuwa njema sana, lakini wakati wake umepita wala haurudi tena. Sasa kama mtu hakuelimishwa, mvi zake hazihesabiwi kuwa dalili ya hekima. Jambo lisilobadilika ni kuwa kila mzee anastahili heshima ya kila kijana siku zote.....Kusadikika, Shaaban Robert
  2. Jibu likisadifu swali, shaka huondoka.......Kusadikika, Shaaban Robert
iii. Mapenzi na burudani
  1. .....Sasa alitamani Peterson atokee, amshukuru tena, shukrani halisi,toka katika uvungu wa moyo wake, si kwa ajili ya kumpa tunu hizo za zenye thamani tu, hasa kwa kuwa yeye alikuwa binadamu wa kwanza ambaye alionyesha kila dalili ya kumtamani, kumpenda na kumthamini kama binadamu halisi....Dar Es Salaam usiku, Ben R. Mtobwa
nimechokoza mada wakuu...najua mnazo nyingi....karibuni jukwaani tubadilishane maarifa........
 
"Moja ya mkakati ambao tumeandaa ni kwamba kama CCM haitashinda Busanda TRA itakuja hapa kuhakiki kama huwa mnalipa kodi ya mapato, kama hamtafanya hivyo tutahakikisha tunawanyangaya leseni kwani CCM ndiyo yenye serikali"

Waziri wa Nishati na madini William Ngeleja akihutubia wananchi wa Katoro wakati wa kampeni za ubunge Busanda.

Very interesting ina maana bila kampeni TRA hawafanyi kazi yao.
 
"Moja ya mkakati ambao tumeandaa ni kwamba kama CCM haitashinda Busanda TRA itakuja hapa kuhakiki kama huwa mnalipa kodi ya mapato, kama hamtafanya hivyo tutahakikisha tunawanyangaya leseni kwani CCM ndiyo yenye serikali"

Waziri wa Nishati na madini William Ngeleja akihutubia wananchi wa Katoro wakati wa kampeni za ubunge Busanda.

Very interesting ina maana bila kampeni TRA hawafanyi kazi yao.

kimantiki, jibu ni ndiyo mkuu..
 
Bazazi sasa ni imam........

Hapo jenerali alikuwa ametulia ile mbaya.
 
Nukuu za Mwalimu Julius K. Nyerere
"those who receive this privelege have the duty to repay the sacrifice which others have made they are like the man who has been given all the food available in a starving village in order that he might have strength to bring supplies from a distant place. if he takes this food and does not bring help to his brothers, then he is the traitor..." (nukuu hii imebandikwa jengo la utawala wa chuo kikuu cha dar es salaam likiwa na lengo la kuhamasisha uzalendo kwa wasomi)

"In Tanganyika we believe that only evil, Godless men would make the color of a man's skin the criteria for granting him civil rights."Julius Kambarage Nyerere addressing British Governor-General Richard

"The African is not 'Communistic' in his thinking; he is -- if I may coin an expression -- 'communitary'."Julius Kambarage Nyerere as quoted in the New York Times Magazine on 27 March 1960.

"Having come into contact with a civilization which has over-emphasized the freedom of the individual, we are in fact faced with one of the big problems of Africa in the modern world. Our problem is just this: how to get the benefits of European society -- benefits that have been brought about by an organization based upon the individual -- and yet retain African's own structure of society in which the individual is a member of a kind of fellowship."Julius Kambarage Nyerere as quoted in the New York Times Magazine on 27 March 1960.

"We, in Africa, have no more need of being 'converted' to socialism than we have of being 'taught' democracy. Both are rooted in our past -- in the traditional society which produced us."Julius Kambarage Nyerere, from his book Uhuru na Umoja (Freedom and Unity): Essays on Socialism, 1967.

"No nation has the right to make decisions for another nation; no people for another people."Julius Kambarage Nyerere, from his A Peaceful New Year speech given in Tanzania on 1 January 1968.

"In Tanzania, it was more than one hundred tribal nits which lost their freedom; it was one nation that regained it."Julius Kambarage Nyerere, from his Stability and Change in Africa speech given to the University of Toronto, Canada, 2 October 1969.

"If a door is shut, attempts should be made to open it; if it is ajar, it should be pushed until it is wide open. In neither case should the door be blown up at the expense of those inside."Julius Kambarage Nyerere, from his Stability and Change in Africa speech given to the University of Toronto, Canada, 2 October 1969.
"You don't have to be a Communist to see that China has a lot to teach us in development. The fact that they have a different political system than ours has nothing to do with it."Julius Kambarage Nyerere, as quoted in Donald Robinson's The 100Most Important People in the World Today, New York 1970.

"...intellectuals have a special contribution to make to the development of our nation, and to Africa. And I am askin understanding that they should possess, should be used for the benefit of the society of which we are all members."Julius Kambarage Nyerere, from his book Uhuru na Maendeleo (Freedom and Development), 1973.

Vipi unazionaje hizo?



 
"moja ya mkakati ambao tumeandaa ni kwamba kama ccm haitashinda busanda tra itakuja hapa kuhakiki kama huwa mnalipa kodi ya mapato, kama hamtafanya hivyo tutahakikisha tunawanyangaya leseni kwani ccm ndiyo yenye serikali"

waziri wa nishati na madini william ngeleja akihutubia wananchi wa katoro wakati wa kampeni za ubunge busanda.

Very interesting ina maana bila kampeni tra hawafanyi kazi yao.

kumbe huyu bwana uzuzu magic aliuanza mapema sana.
Dah... Kweli hii ni kauli mbovu kabisa kuisikia tangu nimezaliwa.
Ndio maana anagombana na walinzi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom