NSSF yaendelea kuwaliza Wananchi waliofungua madai ya mafao yao

Old pirate

Member
Nov 20, 2018
28
24
Jamani ili suala la NSSF limekuwa ni tatizo kubwa sana japo watu wamelifumbia macho ķama hawalioni. Tulizoea zamani unapokosa kazi hasa hizi kampuni zetu za private kimbilio lilikuwa ni vimichango hivi tulojikusanyia wakati tukiwa kazini.

Lakini kwa sasa hali ni mbaya sana unakosa ajira unakimbilia NSSF balaa unalokutana nalo huko utasema unaomba mkopo na s mali yako wahudumu wana majibu ya maudhi kweli kweli mpaka unajiuliza nani anawapa jeuri hawa?

Utapangwa miezi mitatu mitatu kuja kutahamaki miaka imekatika wala ata hawajali hilo, Namba yao ya ofisi 0800756773 imekuwa kama pambo haipokelewi kamwee hata ushinde unaipiga siku nzima na wakipokea hakuna la maana watalokueleza kwanini hupati fedha zako hali ya kuwa taratibu zote umetimiza.

KWA KWELI NI MAUMIVU MAKALI TUNAYOPITIA WAATHIRIKA WA HILI.

Una familia huna hela zako bado unashinda njaa wao wanaona sawa ni uzandiki mkubwa dhuruma yakinifu SERIKALI itutazame kwa jicho la huruma tunapita kwenye hali ngumu sana mpaka unajuta kuwa Mtanzania.

Serikali imetulazimisha kuchukua 33% ya mshahara wa mwisho tumekubali kishingo upande maana hatuna maamuzi juu ya fedha zetu lakini hili nalo limekuwa ni gumu kutekelezeka najiuliza ikitokea umekufa ndiyo basi tena maana angali hai lakini hali inakuwa hivi vipi ukiaga dunia na mtu akajifanya kudai stahiki zako anaweza pewa kesi ata ya uhujumu uchumi ili akome kabsa eeh Mwenyez Mungu tusaidie haki yetu ipatikane dhuluma hii ni uonevu mkubwa.
 
Mkuuu pole sana na haya matatizo.
Nimeumia kwa jinsi ulivyoelezea hiii inshu lkn pia kwa namna unavyotaabika. Kuna ushauri umetolewa happo juu kuhusu kumuona Mwenyekiti wa Bodi au MD hakika ukiwaendea ukawapa sura nzima ya yale unayopitia watakufanyia wepesi ktk malipo yako.

Note; kwasasa shirika lina hali mbaya kifedha kwahiyo malipo hufanyika kwa awamu hivyo ukiwafuata hao huenda ukawekwa kwenye recently batch.
 
Asanteh kwa ushauri mkuu ni maumivu sana tunayopitia
Mkuuu pole sana na haya matatizo.
Nimeumia kwa jinsi ulivyoelezea hiii inshu lkn pia kwa namna unavyotaabika. Kuna ushauri umetolewa happo juu kuhusu kumuona Mwenyekiti wa Bodi au MD hakika ukiwaendea ukawapa sura nzima ya yale unayopitia watakufanyia wepesi ktk malipo yako.

Note; kwasasa shirika lina hali mbaya kifedha kwahiyo malipo hufanyika kwa awamu hivyo ukiwafuata hao huenda ukawekwa kwenye recently batch.
 
Kwanini NSSF ionekane imefilisika wakati haifanyi biashara? Kazi yake ni kukusanya michango sasa inaenda wapi Kwani tunadai pesa zao au zetu? Mbona wanajiweka kwenye msitari wa dhuluma na kuacha msingi mkuu wa uanzishwaji wa NSSF?
 
Mimi wamenipa hiyo 33% kwa taabu sana baada ya miezi 6 wameacha na kazi bado sijapata nikawafuata wakasema mimi ni professional niendelee kutafuta kazi. Fao la kukosa ajira hawanipi tena na wamesema yaliyobaki ni mpaka nifikishe miaka 55.
Sina namna nimebaki tu mtaani najiuliza nani ataweza kutukomboa na janga hili?
Ningepewa changu kwasasa kingeniwezesha kujiajiri ili niache kufikiria zile ajira za kuajiriwa
 
Mimi wamenipa hiyo 33% kwa taabu sana baada ya miezi 6 wameacha na kazi bado sijapata nikawafuata wakasema mimi ni professional niendelee kutafuta kazi. Fao la kukosa ajira hawanipi tena na wamesema yaliyobaki ni mpaka nifikishe miaka 55.
Sina namna nimebaki tu mtaani najiuliza nani ataweza kutukomboa na janga hili?
Ningepewa changu kwasasa kingeniwezesha kujiajiri ili niache kufikiria zile ajira za kuajiriwa. Ajira zenyewe za shida nani atatusaidia sisi watoto wa maskini?
 
Back
Top Bottom