NSSF wanajihami, eti wanatoa mikopo kwa wafanyakazi kupitia SACCOS

MPadmire

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
3,928
3,225
NSSF wanacheza faulu. Kweli Watanzania tunaonewa.

NSSF wametangaza masharti ya mikopo kwa Wafanyakazi, duuu it is impossible.

NSSF imefilisika kabisa, No money.

Bora kukopa benki kuliko NSSF.

NSSF wanasema watu wakope kupitia SACCOS.
 
NSSF wanacheza faulu. Kweli Watanzania tunaonewa.

NSSF wametangaza masharti ya mikopo kwa Wafanyakazi, duuu it is impossible.

NSSF imefilisika kabisa, No money.

Bora kukopa benki kuliko NSSF.

NSSF wanasema watu wakope kupitia SACCOS.
Ili baadaye muambie hakuna sababu ya kusema kuwa mnahitaji hela zenu mkanze maisha kipindi mkiwa hamna kazi.Sasa kile kisingizio kuwa mnaendanazisha biashara au kununu ardhi na kujenga watasema unaweza yapata hayo kupitia mikopo.Yaani hela yako uikope kwa riba.
 
Wanajikosha tu hawana lolote, mbona mikopo imekuja baada ya watu kupaza sauti kuwa michango ya wanachama inatumika ndivyo sivyo bila wachangiaji kunufaika.
 
nssf ni janga lingine!! sijui sheikh yahya aliweka mapepo yake na huko nssf?? serikali imefukiza mapepo, unategemea nini??
 


Swali lake la pili, ninadhani lina mantiki kwamba, hawa wanachama wangepewa mikopo wakiwa bado kazini ili kuwaendelea. Hili ninajibu kwamba, Shirika letu la NSSF nimeliona na ndiyo maana limeshaanza kuangalia uwezekano kwa kupitia SACCOS za Wanachama kwenye maeneo yao ya kazi, kuwakopesha kupitia SACCOS na hili limeanza kufanyiwa kazi. Lingine ni kwamba, Shirika linaangalia utaratibu wa kuwakopesha wanachama wake waweze kujenga nyumba kwa kupitia katika mamlaka, baada ya mamlaka ya NSSF kuweka utaratibu kwamba, tunaweza tukawakopesha Wanachama mikopo ya kujenga nyumba, lakini hii inahitaji utaratibu ambao unatakiwa udhaminiwe au uidhinishwe na mamlaka ya usimamizi na udhibiti wa hifadhi za jamii. Pindi hili likifanyika, NSSF itaangalia uwezekano wa kuwakopesha kwa ajili ya ujenzi wa nyumba, yaani michango yao ile iwe ni dhamana ya kuweza kukopeshwa katika mabenki mbalimbali.

Hili lilikuwa 2011 na unaweza kuta 2014 majibu yakawa hayo hayo .

Dr.Dau na timu yako acheni kuwafukarisha wanachama.
Wawezesheni wanachama wenu,acheni ndoto hizi za Majumba ya 50,000,000ts and above.
Wanachama wenu wengi hawawezi hizo nyumba za bei kubwa jengeni nyumba za kati ya 20-30Millioni kwenye maeneo yaliyopangika,kwa Mtindo huo mtawasaidia wanachama wengi na watawezakuachana na kupanga humu Mjini.
 
Usanii mtupu NSSF.

NSSF walitoa masharti magumu sana kwa Mwanachama kupata Mkopo.

NSSF wanafanya usanii ili waendelee kufanya ufisadi, wanajenga magorofa ambayo hayana tija kwa wanachama. Wanaingia miradi yenye hasara kubwa.

Ni ngumu mwanachama kupata mkopo kupitia NSSF. Unakuta mwanachama ana millioni 5 mpaka 15, yaani NSSF haiwezi kumdhamini mwanachama apate mkopo kupitia benk?

Shame to NSSF administration
 
Wafanyakazi wanatakiwa kupata riba/month ya hela yao iliyowekezwa nssf.leo uwaanbia wao wakatwe riba na sacos?
 
Kuliko mteja akope benki akatwe riba ya 25% na bado hajaamua kuacha kazi, si bora apate mkopo wa 10%?

sio lazima mfanyakazi astaafu kwanza ndo ajenge nyumba ama kufungua kabiashara kake

ndio pia mfanyakazi anapaswa kupata riba ya amana yake huko NSSF. Ni suala la mahesabu tu/accounts

Kuchelewesha kulipa fao la kujitoa ni tatizo pia
 
Back
Top Bottom