fikirikwanza
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 7,452
- 3,065
Hii nchi imekuwa ya amani pengine sio amani bali utulivu kwa muda sasa, kwa maaana mtanzania sio mtu wa kung'ang'ania jambo hata kama linagusa maisha yake ya kila siku. Ipo mifano mingi yakiwemo kodi kubwa kwenye bidhaa na ushuru, mishahara nk. Matumizi mabaya ya madaraka kwa waliokabdhiwa dhamana sasa limekuwa janga kubwa kwa taifa. Ukweli kwamba karibu serikali yote iko lege lege hakumaninishi huu udhaifu ni halali kwa kila mtu na taasisi za serikali.
NSSF: Chombo kilichoanzishwa kwa sheria ya bunge sasa ni mwiba kwa wanachama wake na wananchi kwa ujumla:
1. Kupata mafao imekuwa kazi ngumu kuliko kutafuta pesa na kuhakikisha unachangia kupitia makato kwenye mishahara yako
2. Baada ya kufanya mchakato wa kumlipa mtu chake kuwa mgumu na wenye harufu ya rushwa, wakaja na kali kuliko eti hakuna kuchukua fedha yako mpaka umri wa kustaafu (wanajua kila MTz atafikisha umri huo, hivyo asubiri), hizi ni siasa, wizi au akili ndogo??? watendaji wa NSSF mtajipambanua vipi juu ya hili??
3. Baada ya wananchi kuja juu tamko la kipuuzi la kuzuia fao la kujitoa likafutwa, malipo ya kujitoa yakaanza tena.Mchezo mpya ukabuniwa, lazima uwe mjinga kidogo ili kufanikisha wizi na udanganyifu. Hesabu zitakosewa tena kwa alimia 80% wa wananchama ili kuleta tafurani wakati wa malipo.
4. Wataandaa hesabu feki, hata kama wanaona kuna hela imebaki kwenye akaunti yako, hawatauliza utalipwa sehemu ya pesa yako, iliyobaki wanasubiria iwapo utafuatalia au la, je kama hujui namna ya kufuatilia unafanyaje? kama hujui mahesabu wanafanyikaje unafanyaje? wanabakisha fedha hizo kwa madhumuni gani? HUU ni wizi au makosa ya kibinadamu? watendaji WAKUBWA WANAELEWA HILI AU LA? hawaifahamu ofisi wanayoiongoza?
5. Ili kufanikisha matakwa yao, mawasiliano ya simu-simu zao kila ukipiga zinatumika laini zaidi ya 20, email-ama hawajasoma vya kutosha hawajui kutumia au ni kiburi cha kuharalisha mambo yako, matatizo mengi kuliko majibu mara email haijafika-mara wakikujibu zinabounce ili mradi majibu yawe ya mdomo kuandika hawataki, dunia ya leo mtu anaomba aandikiwe barua itumwe kwa posta? hao ndo NSSF.
6. WANAWEKEZA MICHANGO YA WATEJA MPAKA MTEJA ANAINGIA HASARA, je uwekezaji unaomwingiza hasara mteja ni kwa faida ya nani? KAMA hutoi riba au unatoa 1-2% per annum, bila kujadili kiasi cha fedha mtu anacho inakuwaje? benki zenyewe wanatoa hadi 15% kutokana na wingi wa fedha, NSSF 1-2% kweli hii? kwa nini unawekeza hadi mteja hapati haki yake? tunawekeza hela ya mteja au ziada?? yaani baada ya mteja kupata hela yake kujumlisha faida angalau 5-10% per year; zinazobaki kweli ni ziada zinawekezwa; Ina maana mteja wa leo anaibiwa ili sijui wa lini aje kufaidi. AKILI NI NDOGO, serikali haijaagiza hivyo, WATENDAJI WA NSSF lazima muuonesha kuwa akili mnazo na mnaweza kuzitumia kwa manufaa ya wanachama wote; sio ili mradi mipango hata kama ni mibovu
TUNACHANGISHWA KWA LAZIMA NA KUZUNGUSHWA KUPEWA MICHANGO YETU HADI LINI? Kila kona tatizo ni hilo hilo, Kwani lazima mtu hangaishwe kabla ya kuchukua michango yetu??? KWA HALI HII RUSHWA ITAKUWA KUBWA NDANI YA NSSF, Vyombo vimulike suala hili.
Nawasilisha
NSSF: Chombo kilichoanzishwa kwa sheria ya bunge sasa ni mwiba kwa wanachama wake na wananchi kwa ujumla:
1. Kupata mafao imekuwa kazi ngumu kuliko kutafuta pesa na kuhakikisha unachangia kupitia makato kwenye mishahara yako
2. Baada ya kufanya mchakato wa kumlipa mtu chake kuwa mgumu na wenye harufu ya rushwa, wakaja na kali kuliko eti hakuna kuchukua fedha yako mpaka umri wa kustaafu (wanajua kila MTz atafikisha umri huo, hivyo asubiri), hizi ni siasa, wizi au akili ndogo??? watendaji wa NSSF mtajipambanua vipi juu ya hili??
3. Baada ya wananchi kuja juu tamko la kipuuzi la kuzuia fao la kujitoa likafutwa, malipo ya kujitoa yakaanza tena.Mchezo mpya ukabuniwa, lazima uwe mjinga kidogo ili kufanikisha wizi na udanganyifu. Hesabu zitakosewa tena kwa alimia 80% wa wananchama ili kuleta tafurani wakati wa malipo.
4. Wataandaa hesabu feki, hata kama wanaona kuna hela imebaki kwenye akaunti yako, hawatauliza utalipwa sehemu ya pesa yako, iliyobaki wanasubiria iwapo utafuatalia au la, je kama hujui namna ya kufuatilia unafanyaje? kama hujui mahesabu wanafanyikaje unafanyaje? wanabakisha fedha hizo kwa madhumuni gani? HUU ni wizi au makosa ya kibinadamu? watendaji WAKUBWA WANAELEWA HILI AU LA? hawaifahamu ofisi wanayoiongoza?
5. Ili kufanikisha matakwa yao, mawasiliano ya simu-simu zao kila ukipiga zinatumika laini zaidi ya 20, email-ama hawajasoma vya kutosha hawajui kutumia au ni kiburi cha kuharalisha mambo yako, matatizo mengi kuliko majibu mara email haijafika-mara wakikujibu zinabounce ili mradi majibu yawe ya mdomo kuandika hawataki, dunia ya leo mtu anaomba aandikiwe barua itumwe kwa posta? hao ndo NSSF.
6. WANAWEKEZA MICHANGO YA WATEJA MPAKA MTEJA ANAINGIA HASARA, je uwekezaji unaomwingiza hasara mteja ni kwa faida ya nani? KAMA hutoi riba au unatoa 1-2% per annum, bila kujadili kiasi cha fedha mtu anacho inakuwaje? benki zenyewe wanatoa hadi 15% kutokana na wingi wa fedha, NSSF 1-2% kweli hii? kwa nini unawekeza hadi mteja hapati haki yake? tunawekeza hela ya mteja au ziada?? yaani baada ya mteja kupata hela yake kujumlisha faida angalau 5-10% per year; zinazobaki kweli ni ziada zinawekezwa; Ina maana mteja wa leo anaibiwa ili sijui wa lini aje kufaidi. AKILI NI NDOGO, serikali haijaagiza hivyo, WATENDAJI WA NSSF lazima muuonesha kuwa akili mnazo na mnaweza kuzitumia kwa manufaa ya wanachama wote; sio ili mradi mipango hata kama ni mibovu
TUNACHANGISHWA KWA LAZIMA NA KUZUNGUSHWA KUPEWA MICHANGO YETU HADI LINI? Kila kona tatizo ni hilo hilo, Kwani lazima mtu hangaishwe kabla ya kuchukua michango yetu??? KWA HALI HII RUSHWA ITAKUWA KUBWA NDANI YA NSSF, Vyombo vimulike suala hili.
Nawasilisha