Nssf ndio fahari yangu hapa tanzania, vukeni mipaka sasa.

mmteule

JF-Expert Member
Oct 3, 2011
5,500
12,826
wanajamvi wenzangu, hapa tzie tunayo mifuko kadhaa ya hifadhi za jamii nssf ikiwa mojawapo. Nawapongeza sana wafanyakazi mpaka mkurugenzi wake kwa weledi wao na kasi yao ya kuwekeza katika nchi yetu. Mimi kama mtanzania wa kawaida ninafurahia sana kuanzia ujenzi wa hostel za mabibo, sua, ujenzi wa nyumba za bei rahisi kinyerezi, ujenzi wa majengo mengi mengi kama vitega uchumi. Kiukweli nawapongeza sana.
Hayo yote tisa na sasa wameamua kujikita kwenye ujenzi wa daraja la kigamboni ambalo litapunguza kero ya vivuko kwa wakazi wa dar es salaam.
Funga kazi ambayo imenivutia zaidi ni kuamua kuwekeza kwenye uzalishaji wa nishati ya umeme ili kuwaondolea watanzania adha wanayoipata... Sina cha kuwapa ila nawaomba wachape kazi isije ikawa tembo akisifiwa........
Wito wangu kwenu kama mtanzania mwenzenu, naomba sana sasa mvuke mipaka, msijifungie hapa hapa, msiige mabenki yetu wala viwanda vyetu au niseme utamaduni wetu wa uoga nendeni nje ya mipaka muwekeze na muitangaze nchi yetu. Mungu wabariki nssf
 
Umetumwa eh kuja kuwafagilia JF? Hayo mambo wanayowekeza si wanafidika mbona wanachama hawapati hata interest kwenye fedha zao? Katiba mpya inakuja hatutaki kuonewa sasa hii mifuko ya jamii kama hawatawapa interest wateja wao bora hizo fedha ziingizwe kwenye fixed account ya bank tu na si kwa kina dau kama umetumwa mwambie hili.
 
Me bana ... Nssf nawafagilia sana ... Ni moja ya taasisi zinazofanya mambo na ya kaonekana... Asiye wakubali atakuwa na chuki zake binafsi
 
Nssf wanatakiwa kuwekeza kwenye kumbukumbu za wanachama wao na sio kwenye mambo ambayo serekali inayokusanya kodi inatakiwa kuyafanya. Kama wewe mwanachama kachukue taarifa yako ya hesabu uone madudu yaliyomo humo.
 
Nssf wanatakiwa kuwekeza kwenye kumbukumbu za wanachama wao na sio kwenye mambo ambayo serekali inayokusanya kodi inatakiwa kuyafanya. Kama wewe mwanachama kachukue taarifa yako ya hesabu uone madudu yaliyomo humo.

Umeona eh nilifatilia pale 77 kwenye maonyesho yani nilijuta kwa nini niliingia huko bora lile jingine nasikia mafao ni wiki 2 tu na si miezi sita kama hawa viazi
 
Umetumwa eh kuja kuwafagilia JF? Hayo mambo wanayowekeza si wanafidika mbona wanachama hawapati hata interest kwenye fedha zao? Katiba mpya inakuja hatutaki kuonewa sasa hii mifuko ya jamii kama hawatawapa interest wateja wao bora hizo fedha ziingizwe kwenye fixed account ya bank tu na si kwa kina dau kama umetumwa mwambie hili.

KING KONG umekosea sana, tatizo we kila kitu unafikiria kwa kutumia masaburi.... sina interest na hata simjui yeyote hapo nssf ila ni mtazamo tu wewe dogo wa mawazo.
 
KING KONG umekosea sana, tatizo we kila kitu unafikiria kwa kutumia masaburi.... sina interest na hata simjui yeyote hapo nssf ila ni mtazamo tu wewe dogo wa mawazo.

''No research no right to speak'' Nenda pale ubungo pick randomly wateja kama kumi upate maoni yao kuhusu huduma, mazingira ya ofisi hiyo, mafao yanayotolewa ikilinganishwa na mategemeo yao. Halafu ndio uje kuongea hapa. Pia ulizia mgawanyiko wa wafanyakazi wa kampuni hiyo kuna wateule kama wewe na watwana, na kigezo kinachotumika kuweka tabaka hiziu mbili ndani kampuni hii ya umma. TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO BORA! HAKIKA HISTORIA ITAWAHUKUMU WASIO TENDA HAKI.
 
''No research no right to speak'' Nenda pale ubungo pick randomly wateja kama kumi upate maoni yao kuhusu huduma, mazingira ya ofisi hiyo, mafao yanayotolewa ikilinganishwa na mategemeo yao. Halafu ndio uje kuongea hapa. Pia ulizia mgawanyiko wa wafanyakazi wa kampuni hiyo kuna wateule kama wewe na watwana, na kigezo kinachotumika kuweka tabaka hiziu mbili ndani kampuni hii ya umma. TANZANIA ITAJENGWA NA WENYE MOYO BORA! HAKIKA HISTORIA ITAWAHUKUMU WASIO TENDA HAKI.

Mwambie mwambie mwanamapinduko dogo kapewa hela aje kuisifia nssf ndani ya JF
 
Ngoja ifikie wakati ukadai malipo yako ndio utawajua hao Nssf ni nani
 
Mimi naona nssf wanafanya vizuri kama kuna kasoro zozote kuhusu maslahi ya wanachama ni jukumu la wanachama kwa umoja wao kushirikiana na uongozi wa nssf kutatua. Nawapongeza nssf kuwekeza kwenye umeme hamjachelewa ongeza bidii. wekezeni kwenye umeme wa angalau Mg 1000 mtawasaidia watz. Tuachane na akina aggre _ko, symbi _ni na dowa _ns.
 
Back
Top Bottom