NSSF mnawatesa Wajawazito wa Fao la Uzazi; Customer Care mbovu ofisi za Ubungo

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669
Ni week ya sasa Wajawazito katika ofisi mbalimbali za jiji la Dar es Salaam hawapati huduma,iwe Ubungo au Ilala kwa wakazi wa Dar es Salaam.

Inaenda karibu week ya pili sasa kwa wajawazito ukienda kwenye ofisi za NSSF kwa ajili ya Fao la Ujauzito ni kero tupu,sababu mara mtandao unasumbua mara hatupokei hizo form.

Kitengo cha Huduma kwa Wateja Ofisi za NSSF Ubungo Plaza ni ovyo na aibu tupu.Unaenda unamkuta mwanamke badala ya kumuhudumia mwanamke mwenzake aliye katika matazamio kwa upole na ukarimu,inakuwa ni lugha ya ukali na ghadhabu.

Mtu mfanyakazi,anachangia pesa zake lakini ni usumbufu mtupu.Lugha wanayotoa wahudumu ambao walipaswa kutoa lugha nzuri na ya staha ni kinyume chake,watu wapo ofisini kama wamelazimishwa.

Ifikie mahali wahudumu katika hizi ofisi watambue kuwa wapo hapo si kwa ajili yao na hawalipwi mishahara sababu wanakaa tu,bali ni kwasababu wanahudumia wateja ambao ndio wafanyakazi wanaochangia pesa hizo.

Kila unapooenda unakutana na lugha za "mtandao hakuna,hatujui utarudi lini" au "Forms za fao la uzazi hatupokei kwa sasa,jinsi ya kujaza kaulize huko walikokuambia kuwa tunatoa fao la uzazi".

NSSF kama wadau wa wafanyakazi wanatakiwa kuwajali wateja wao,kutoa huduma nzuri na kuwa na lugha nzuri kwa wateja.

NSSF shughulikieni tatizo la hicho mnachoita "mtandao" ili watu wapate huduma kwa wakati,wapeni semina wafanyakazi(hasa tawi la Ubungo kwa Dsm) namna ya kuongea na kuhudumia watu.Wawe na lugha nzuri kwa wateja.

Mfanyakazi mshahara mdogo na bado manyanyaso kwa NSSF makubwaaa,mtatuua walimu kwa stress jamani
 
Hao ni kawaida yao. Ofisi zao mikoa mingi wako hivyo hivyo. Ili wakulipe hilo fao ni hadi ugombane nao, uwatikise ndo wanakulipa.
Hela yenyewe wamepunguza siku hizi, ni tuhela tudogo ila hadi mtibuane kweli kweli. Jamaa wanaboa sana.
 
Dawa yao hao watolewe tuajiriwe sie wenye lugha nzuri
Hii ndo permanent solution
 
Wanahangaisha sana wateja wao na tena wana lugha ya
Wakulaumiwa ni CCM kutokana na upeo mdogo wa kuona mambo wakaiunganisha mifuko imebaki miwili tu, matokeo yake hakuna ushindani wa kibiashara, they can do what want but yet they are sure of getting new customers
 
NSSF TEMEKE pale sokoni ILALA NI Tatizo tena kuna changamoto kubwa tu,

NSSF wana bima ya afya kwa wananchama, hiyo BIMA ilivyo kama kifurushi mawasiliano, unaenda hospitali ukiwa mgonjwa unaambiwa huduma hakuna kifurushi chako kimekwisha, nenda kwenye OFISI YA NSSF uka update.

Mgonjwa unajiuliza inakuwaje kwa mwanachama HAI anaechangia michango kila mwezi anakosa huduma ya matibabu?

Ukienda ofisi ya NSSF TEMEKE unapokerewa na wanafunzi waliopo mafunzoni "FIELD" ukweli awa vijana wanajituma sana tena wana ari ya kufanya kazi watakuandikisha jina lako na kulipeleka kwa maafisa wenye dhamana ya kukusaidia kupata KIBALI CHA MATIBABU.

Kibali hiki kinatolewa na mama mmoja mweupe hivi anaitwa MADAM SARAH, huyu mama kuanzia saa 3 asubuhi anakuja kupitisha kibali kwenda mkurugezi saa 9 jioni. Yaani bila kujua kama mwanachama au mtegemezi wake anaumwa anahitaji matibabu.

mbaya zaidi hawana hata chembe ya huruma kwa wanachama wao, wanapofika kupata huduma katika ofisi zao, yaani kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana wanajifungia ofisi eti wanakikao.

ikifika saa 7 mchana wanaenda kula lunch, awa watu ni hatari sana.
 
NSSF TEMEKE pale sokoni ILALA NI Tatizo tena kuna changamoto kubwa tu,

NSSF wana bima ya afya kwa wananchama, hiyo BIMA ilivyo kama kifurushi mawasiliano, unaenda hospitali ukiwa mgonjwa unaambiwa huduma hakuna kifurushi chako kimekwisha, nenda kwenye OFISI YA NSSF uka update.

Mgonjwa unajiuliza inakuwaje kwa mwanachama HAI anaechangia michango kila mwezi anakosa huduma ya matibabu?

Ukienda ofisi ya NSSF TEMEKE unapokerewa na wanafunzi waliopo mafunzoni "FIELD" ukweli awa vijana wanajituma sana tena wana ari ya kufanya kazi watakuandikisha jina lako na kulipeleka kwa maafisa wenye dhamana ya kukusaidia kupata KIBALI CHA MATIBABU.

Kibali hiki kinatolewa na mama mmoja mweupe hivi anaitwa MADAM SARAH, huyu mama kuanzia saa 3 asubuhi anakuja kupitisha kibali kwenda mkurugezi saa 9 jioni. Yaani bila kujua kama mwanachama au mtegemezi wake anaumwa anahitaji matibabu.

mbaya zaidi hawana hata chembe ya huruma kwa wanachama wao, wanapofika kupata huduma katika ofisi zao, yaani kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana wanajifungia ofisi eti wanakikao.

ikifika saa 7 mchana wanaenda kula lunch, awa watu ni hatari sana.
Yaani hawa NSSF ni ugoro mtupuuuuu....unaweza ukatandika mtu makofi.Ni bora waseme kama Fao la Uzazi au Bima ya Matibabu haipo ili ijulikane moja,ila sio huu uhuni
 
Back
Top Bottom