NSSF kutumia Tsh 400 bil kuzalisha megawati 300: Yajitahidi kuchukua KIWIRA

Je, wenye pesa zao wamewapa NSSF ruhusa ya kutumia pesa zao nyigi kiasi hicho au ndiyo yale maamuzi ya chini ya meza?
 
NSSF kufua umeme huu ndiyo suruhisho la tatizo hili? je hapa tunatibu core problem au tunazima moto? Action plan iliyotolewa na wizara je itamaliza tatizo hili na tulisahau kabisa?

Bado tuna kazi ya kufanya wadugu, tufike mahala tuwe serious kwa mambo yanayogusa maisha ya kila siku ya watu
 
Swala kubwa la kujiuliza ni kwa nini serikali imeamua kutumia NSSF na siyo TANESCO? Well Dau anaeleweka kwa mizengwe yake tangu pale alipoua watoto wasio na hatia kule Tabora kwenye miradi yake ya Pwagu na Pwaguzi vile vile kwa kuwa kinara wa kumtajirisha Manji. Kama hiyo haitoshi subirini mtaona huu ni mwanya na njia ya kumtajirisha moja kwa moja mmiliki wa Dowans (JK) pamoja na RA bila kumsahau EL. Mbinu zote hizi zinahalalishwa hasa baada ya kuweza kumuweke Zitto mfukoni mwao.

Je nani mwenye maamuzi ya mwisho NSSF? Je nani anamchagua DG wa NSSF ie Dau ... .... ... kawekwa na nani? Je ni kwa nini serikali inakimbilia kwa NSSF na kuwaacha TANESCO ambao ndio wenye utaalam kwenye mambo ya umeme?

Well tusubiri majibu ya vifisadi dagaa GT, Mdondoaji et al.
 
Hivi karibuni pamekuwepo Shinikizo la NSSF kutaka kuwekeza kwenye mradi wa Kiwira. Swali ninalojiuliza NSSF wana expertise gani katika masuala ya uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe? Swali la msingi ninalojiuliza je NSSF wanaye strategic partner mwenye ujuzi na uzoefu wa uendeshaji wa miradi ya aina hii? Kwa mujibu wa taarifa za kwenye media haionekani kama wanaye partner wa aina hiyo unless kama ni siri.


Uzoefu, unaonyesha Pension Funds zote duniani, huwa haziwekezi kwenye miradi mkubwa as lead investor. Mara nyingi Pension Funds zinawekeza kwenye miradi iliyo viable, na yenye wawekezaji wengine wenye uzoefu na aina ya shughuli inayofanyika. Wajibu wa Pension Funds ni ku identify miradi ambao ROI (Return of Investment) sio ya kutilia mashaka na risk iliiyo very minimal….kwani wanawekeza jasho la mfanyakazi ambaye analitegemea katika maisha yake ya baada ya kustaafu. Hivyo, NSSF ilipowekeza kwa kununua hisa za NMB zilizouzwa kwenye soko la Hisa nchini, au kwenye Unit Trust of Tanzania au miradi mingine yoyote iliyo lucrative kama vile TWIGA CEMENT, ilikuwa ni sahihi kabisa etc. Kwani tunajua microfinance industry inakua nchini; na tunajua harakati za ujenzi zinazidi kupanuka nchini hivyo demand ya cement kwa miaka mingi ijayo itakuwepo.



Uwekezaji kwenye miradi ya umeme ni very risky na ROI ni ya muda mrefu na endapo mipango thabiti nay a kueleweka haipo, inaweza kuwa mradi wa hasara kubwa. Hivyo idea ya NSSF kuwekeza as LEAD AND SOLE INVESTOR, ni wazo BAYA. Mtu yeyote anayelipigia debe wazo la aina hii….lazima atakuwa ana maslahi binafsi nyuma yake na sio maslahi ya PENSIONERS wanao contribute kwenye mfuko wao.



Isitoshe, NSSF wana track record ya kuchangamkia miradi mbalimbali as AS LEAD INVESTOR wakati hawana technical expertise katika eneo husika , matokeo yake mpaka leo miradi hiyo haija take-off. Chukulia mfano wa MRADI WA DARAJA LA KIGAMBONI…mpaka leo mwaka wa 5, bado upo kwenye makaratasi…na mpaka sasa wamekwishabadilisha Consultants mara mbili….na bado mradi haujulikani utaanza lini. Vivyo hivyo, NSSF hao hao….tokea miaka 4 iliyopita walisema wanawekeza kwenye mradi wa Hospitali (at least mradi huu walikuwa na strategic partner-Appollo Hospitals ya India); lakini kwakuwa wao ndio walikuwa LEAD INVESTOR, mpaka leo mradi huo hauja take-off; na majuzi wakati wa power crisis waliongelea mradi wa umeme wa dharura….mpaka leo (pamoja na udharura) hakuna lolote lililokwishafanyika.



Rai yangu kwa NSSF, waachane na papara za kuwekeza kila mahala simply b’se potfolio yao ni kubwa….hizo ni fedha za wafanyakazi…….wawe makini sana na maeneo wanayowekeza….sio leo wanarukia kununua majenereta ya umeme, kesho mchuchuma, kesho kutwa tutaambiwa wanataka kujenga airport……miradi hii haina tija kwa wanachama wenye mfuko wao.




For once, waweze kwenye miradi ambayo wananchama wake wanaweza kunufaika hata kabla ya kustaafu kama vile ujenzi wa low cost housing ambazo wanachama wake wanaweza kukopeshwa na kukatwa pole pole….walau wawe na security ya makazi…
 
Tatizo la umeme Tanzania litaendelea milele kama laws & regulations zitaendelea kama zilivyo sasa,shida ya umeme Tanzania sio vyanzo vya uzalishaji,tuna kila kitu kuanzia mabwawa,makaa(coal),natural gas,wind etc ambavyo vina uwezo kuliko mahitaji yetu,then capital sio issue kuna pesa kuliko zinazohitajika kufanikisha hiyo miradi yote,ukija kwenye technology nayo sio issue,can you imagine TANESCO walishindwa simple task ya kununua gas turbine na kuishia kulipa billions bila umeme na drama mwaka wa 5 sasa kuburuzana mahakamani...solutions ni very simple kill TANESCO monopoly,ruhusu fair play then create serious & independent regulatory body to enforce standards,safety,fairness etc,kwa sasa only TANESCO ndio anaweza kuuza umeme ile nchi hakuna mtu mwingine anaruhusiwa,no way serious investor ataweka billions zake on the line asubiri incompetent & corrupt TANESCO wamwambie namna ya kuuza umeme wake,hakuna cha NSSF wala serikali watatutoa gizani tukiendelea na sheria zetu,kill TANESCO monopoly then ruhusu fairplay is the only way.
 
...solutions ni very simple kill TANESCO monopoly,ruhusu fair play then create serious & independent regulatory body to enforce standards,safety,fairness etc,kwa sasa only TANESCO ndio anaweza kuuza umeme ile nchi hakuna mtu mwingine anaruhusiwa,no way serious investor ataweka billions zake on the line asubiri incompetent & corrupt TANESCO wamwambie namna ya kuuza umeme wake,hakuna cha NSSF wala serikali watatutoa gizani tukiendelea na sheria zetu,kill TANESCO monopoly then ruhusu fairplay is the only way.

Kuna kitu wanaita natural monopoly TANESCO kwa sasa wanahiyo advantage, umeme unahitajika lakini hayo makampuni binafsi yatapitisha umeme wao kupitia pylons zipi au kuna wireless technology ya kusambaza umeme.

Na huwezi kusema kila kampuni linalo taka leta umeme lipitishie pylons zake nchi nzima all over again it is unrealistic (mitaa itajaa mi-pylons). Kwa kuwa Tanesco ina miliki pylons nyingi it is only natural it holds that monopoly. Mpaka hapo serikali itakapojenga mitaro nchi nzima ndio makampuni ya umeme yaneweza shindana kwa kupitisha waya zao kwenye mitaro ya serikali vinginevyo Tanesco itaendelea kuwa na monopoly na investors kuendelea kushirikiana nayo kwa namna fulani mainly most places that are in need of electricity Tanesco have their pylons there already.
 
na uje huo umeme kwani mgao unaumiza sana uchumi.mipango ya muda mrefu ndiio itatoa ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili
 
Wacha,

Wenye maamuzi ya mwisho NSSF ni board of trustee ambayo imeundwa na vyama vya wafanyakazi unaweza kwenda kuwauliza maswali mengine pia kwani wao pia hufanya uteuzi wa DG wa NSSF. Mengine siwezi kukujibu waulizeni NSSF
 
Nyie subirini tu...

Upande wangu sikutaka ku-deal na hili la Kiwira kwani tulipoanzisha ile kampeni ya kuirudisha Kiwira mikononi mwa Watanzania hatukuambiwa tunawaonea watu. Lakini sasa inaonekana wameamua kufanya wanavyotaka kufanya kwa sababu wanaweza.
Hivi hawa NSSF si warudi hatua chache tu nyuma kwanza waangalie ni nani anachangia huo mfuko (subscribers) na ana hali gani kimaisha na kimapato!!!!??? Inasikitisha, badala ya kujiingiza kwenye miradi yenye maswali mengi kama haya inayoweza kupelekea matatizo ya shirika huko mbeleni (tunaona serikari yenyewe ilivyo kosa mwelekeo kwa kujiingiza huko) na badala yake hicho kilichopo kwanza waweke subsidies (kama gawio vile) angalau 20% ya faida kwa wanachama. Maana nasikia wanasema wana akiba ya miaka 40 (40 years!!!???) wakati zaidi ya 70% wa wanachama wake (wachangiaji) hawana hata uhakika wa saving ya mwaka mmoja! Tutaona mengi
 
na uje huo umeme kwani mgao unaumiza sana uchumi.mipango ya muda mrefu ndiio itatoa ufumbuzi wa kudumu wa tatizo hili
400b kwa 300mw sio mpango mzuri wa muda mrefu ukichukulia kuwa ni makaa ya mawe!
 
Hivi karibuni pamekuwepo Shinikizo la NSSF kutaka kuwekeza kwenye mradi wa Kiwira. Swali ninalojiuliza NSSF wana expertise gani katika masuala ya uzalishaji wa umeme wa makaa ya mawe? Swali la msingi ninalojiuliza je NSSF wanaye strategic partner mwenye ujuzi na uzoefu wa uendeshaji wa miradi ya aina hii? Kwa mujibu wa taarifa za kwenye media haionekani kama wanaye partner wa aina hiyo unless kama ni siri.


Uzoefu, unaonyesha Pension Funds zote duniani, huwa haziwekezi kwenye miradi mkubwa as lead investor. Mara nyingi Pension Funds zinawekeza kwenye miradi iliyo viable, na yenye wawekezaji wengine wenye uzoefu na aina ya shughuli inayofanyika. Wajibu wa Pension Funds ni ku identify miradi ambao ROI (Return of Investment) sio ya kutilia mashaka na risk iliiyo very minimal….kwani wanawekeza jasho la mfanyakazi ambaye analitegemea katika maisha yake ya baada ya kustaafu. Hivyo, NSSF ilipowekeza kwa kununua hisa za NMB zilizouzwa kwenye soko la Hisa nchini, au kwenye Unit Trust of Tanzania au miradi mingine yoyote iliyo lucrative kama vile TWIGA CEMENT, ilikuwa ni sahihi kabisa etc. Kwani tunajua microfinance industry inakua nchini; na tunajua harakati za ujenzi zinazidi kupanuka nchini hivyo demand ya cement kwa miaka mingi ijayo itakuwepo.



Uwekezaji kwenye miradi ya umeme ni very risky na ROI ni ya muda mrefu na endapo mipango thabiti nay a kueleweka haipo, inaweza kuwa mradi wa hasara kubwa. Hivyo idea ya NSSF kuwekeza as LEAD AND SOLE INVESTOR, ni wazo BAYA. Mtu yeyote anayelipigia debe wazo la aina hii….lazima atakuwa ana maslahi binafsi nyuma yake na sio maslahi ya PENSIONERS wanao contribute kwenye mfuko wao.



Isitoshe, NSSF wana track record ya kuchangamkia miradi mbalimbali as AS LEAD INVESTOR wakati hawana technical expertise katika eneo husika , matokeo yake mpaka leo miradi hiyo haija take-off. Chukulia mfano wa MRADI WA DARAJA LA KIGAMBONI…mpaka leo mwaka wa 5, bado upo kwenye makaratasi…na mpaka sasa wamekwishabadilisha Consultants mara mbili….na bado mradi haujulikani utaanza lini. Vivyo hivyo, NSSF hao hao….tokea miaka 4 iliyopita walisema wanawekeza kwenye mradi wa Hospitali (at least mradi huu walikuwa na strategic partner-Appollo Hospitals ya India); lakini kwakuwa wao ndio walikuwa LEAD INVESTOR, mpaka leo mradi huo hauja take-off; na majuzi wakati wa power crisis waliongelea mradi wa umeme wa dharura….mpaka leo (pamoja na udharura) hakuna lolote lililokwishafanyika.



Rai yangu kwa NSSF, waachane na papara za kuwekeza kila mahala simply b'se potfolio yao ni kubwa….hizo ni fedha za wafanyakazi…….wawe makini sana na maeneo wanayowekeza….sio leo wanarukia kununua majenereta ya umeme, kesho mchuchuma, kesho kutwa tutaambiwa wanataka kujenga airport……miradi hii haina tija kwa wanachama wenye mfuko wao.




For once, waweze kwenye miradi ambayo wananchama wake wanaweza kunufaika hata kabla ya kustaafu kama vile ujenzi wa low cost housing ambazo wanachama wake wanaweza kukopeshwa na kukatwa pole pole….walau wawe na security ya makazi…

Wazo zuri sana la lowcost housing ila nikuulize life expectancy ya mtanzania ni miaka mingapi? Pili makato ya hifadhi katika mshahara wa mfanyakazi kwa average ni kiasi gani? Tatu vp unaweza kutufahamisha NSSF watapambana vp na tabia sugu ya watu wasiolipa madeni ambao wameyatia hasara kubwa mabenki kwa kukopa lakini hawalipi. Kwa afadhali benki zinawekeza katika short terms investment wanaweza kufidia zile hasara NSSF wakipata hasara ndio imekula kwao. Sasa tufahamishe NSSF waweke mikakati gani kupambana na utapeli wa watanzania wa kukopa halafu hawarudishi?

Mwisho kabisa umejuaje hizi investments sio viable what determines an investment to be viable or not? Hata kama ROI is of the long term what determines the risk of a portolio sio duration of an investment but rather a level risk exposure au sometimes known as a Sharpe Ratio. Ikiwa kama risks ni ndogo katika hizo project but ROI ni kubwa je waache hiyo investment for the sake of just kwakuwa ni of long term nature? What if it is long and sustainable rather than short but risky unadhani ni vema waache ile waende kati short term investment just kwakuwa ni za muda mfupi?
 
Back
Top Bottom