kishegheni
Member
- Mar 6, 2012
- 21
- 85
NSSF imeteua Kampuni binafsi ya PROPER CONSULT kusimamia majengo yake na kuwataka wapangaji kufanya malipo kwenye Akaunti binafsi ya Kampuni hiyo iliyoko CRDB kinyume maelekezo ya Serikali kuwa malipo yote ya Serikali yafanyike kwa kutumia Control Number ili pesa zote ziingie Serikalini.
Hapa kuna harufu ya ufisadi.
1) NSSF wameteua kampuni kusimamia majengo bila kufuata Sheria ya manunuzi ya umma ya kupata hii Kampuni, hivyo kuna dalili ya rushwa.
2) NSSF wamekuwa kila mwaka wanatenga kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya matengenezo ya nyumba zake na zinatumika lakini matengenezo hayafanywi ndani wala nje, wapangaji wanaambiwa wafanye matengenezo wenyewe. Swali ni kuwa hizo pesa za matengenezo zinatumika kufanyia nini kama sio ufisadi.
Shirika hili la umma linapaswa kuchunguzwa na Takukuru na wizara ya Fedha kuhusu ufisadi huu na harufu ya rushwa.
Hapa kuna harufu ya ufisadi.
1) NSSF wameteua kampuni kusimamia majengo bila kufuata Sheria ya manunuzi ya umma ya kupata hii Kampuni, hivyo kuna dalili ya rushwa.
2) NSSF wamekuwa kila mwaka wanatenga kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya matengenezo ya nyumba zake na zinatumika lakini matengenezo hayafanywi ndani wala nje, wapangaji wanaambiwa wafanye matengenezo wenyewe. Swali ni kuwa hizo pesa za matengenezo zinatumika kufanyia nini kama sio ufisadi.
Shirika hili la umma linapaswa kuchunguzwa na Takukuru na wizara ya Fedha kuhusu ufisadi huu na harufu ya rushwa.