Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,462
- 39,929
Shirika la Hifadhi ya Jamii limekuwa au niseme limegeuzwa kuwa Shirika la Uwekezaji la Hifadhi ya Jamii. Na kwa jinsi ambavyo linaendeshwa bila ya shaka linasukumwa na kutafuta faida na ni faida hii ambayo linapata imekuwa ikiwekezwa kwenye miradi mbalimbali. Hili si tatizo.
Hata hivyo kwenye mashirika ambayo yanafanya kazi kwa ajili ya faida (for profit companies) yanarudisha sehemu ya faida yake kwa wanahisa (shareholders) wake. Inaweza kurudishwa kama gawio (dividends) kila mwaka kufuatana na kanuni ambayo shirika limejiwekea.
NSSF inakadiriwa kuwa na wanachama karibu 600,000 hadi mwezi Juni mwaka huu likiwa na mali yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni moja ambayo inakadiriwa kukua kwa haraka hadi mwaka 2013. Kwa mujibu wa sera zao za uwekezaji NSSF hutenga asilimia 75 ya fedha zao kwenda kwenye uwekezaji na asilimia 25 kwenda kwenye mafao na gharama za uendeshaji. Ni wazi kuwa 2/3 ya fedha zinazoweza kuwekezwa zinawekezwa kwenye kile ambacho kinaonekana ni 'high yield' investments.
Je ipo haja ya kuligawa shirika hili na kuhakikisha upande unahusiana na hifadhi ya jamii (mafao kwa wanachama) unaendeshwa tofauti na upande unaohusika na uwekezaji? Je kuna uwezekano wa kuhakikisha kuwa huo upande wa uwekezaji unaendesha kama kampuni nyingine ya faida ambapo wanachama wa NSSF ndio wanakuwa wanahisa wa shirika hilo na ambao watalipewa gawio kila shirika linapotengeneza faida kabla halijaamua kuwekeza fedha kama faida?
Swali hili ni muhimu kwa sababu kwa mtu ambaye anachangia NSSF na bado hajaanza kupata mafao mbalimbali au hajatumia mafao yoyote kwa mwaka hapati faida yoyote ya kifedha kutokana mchango wake ambao unatumika kutengeneza faida kwa shirika. Na kama mtu atakuwa amechangia kwa miaka mitano au zaidi na labda amepata fao la msiba, n.k au aambiwe asubiri hadi kuretire kuanza kupewa shilingi themanini elfu kila mwezi baada ya kuchangia shirika kwa miaka thelathini au ishirini naona ni unyonyaji wa aina yake.
Ni muhimu kwa wanachama kufaidika kifedha (monetary benefit) na uwekezaji wa NSSF kila mwaka. Na namna pekee ya kuwafanya wanachama nao wanufaike ni kuhakikisha kuwa NSSF (bila ya shaka na mashirika mengine ya pensheni) inaweka utaratibu wa kuwagia wanachama wake ama kwa kutengeneza account au kuchangia kwenye akaunti ya mwanachama kiasi cha faida fedha ambazo mwanachama anaweza kuzitoa wakati wowote nje ya zile za pensheni.
Jambo la kwanza ambalo linahitaji kufanyika kwa haraka ni kubadili sheria ili NSSF isiwezeke fedha za wanachama kwenye miradi yenye kutarajia faida bila kuhakikisha kuwa sehemu ya faida inayopatikana inawarudia wanachama kama gawio siyo kama sehemu kiduchu ya mafao.
Swali la Ugomvi: Je CDM ina sera gani kuhusu NSSF na uwekezaji wa NSSF kwa sababu tayari tunajua sera ya CCM ni kutumia NSSF pale ambapo serikali imeshindwa au haina fedha au pale ambapo serikali inataka fedha ya haraka haraka kuikoa mbele ya wananchi.
Hata hivyo kwenye mashirika ambayo yanafanya kazi kwa ajili ya faida (for profit companies) yanarudisha sehemu ya faida yake kwa wanahisa (shareholders) wake. Inaweza kurudishwa kama gawio (dividends) kila mwaka kufuatana na kanuni ambayo shirika limejiwekea.
NSSF inakadiriwa kuwa na wanachama karibu 600,000 hadi mwezi Juni mwaka huu likiwa na mali yenye thamani ya zaidi ya dola bilioni moja ambayo inakadiriwa kukua kwa haraka hadi mwaka 2013. Kwa mujibu wa sera zao za uwekezaji NSSF hutenga asilimia 75 ya fedha zao kwenda kwenye uwekezaji na asilimia 25 kwenda kwenye mafao na gharama za uendeshaji. Ni wazi kuwa 2/3 ya fedha zinazoweza kuwekezwa zinawekezwa kwenye kile ambacho kinaonekana ni 'high yield' investments.
Je ipo haja ya kuligawa shirika hili na kuhakikisha upande unahusiana na hifadhi ya jamii (mafao kwa wanachama) unaendeshwa tofauti na upande unaohusika na uwekezaji? Je kuna uwezekano wa kuhakikisha kuwa huo upande wa uwekezaji unaendesha kama kampuni nyingine ya faida ambapo wanachama wa NSSF ndio wanakuwa wanahisa wa shirika hilo na ambao watalipewa gawio kila shirika linapotengeneza faida kabla halijaamua kuwekeza fedha kama faida?
Swali hili ni muhimu kwa sababu kwa mtu ambaye anachangia NSSF na bado hajaanza kupata mafao mbalimbali au hajatumia mafao yoyote kwa mwaka hapati faida yoyote ya kifedha kutokana mchango wake ambao unatumika kutengeneza faida kwa shirika. Na kama mtu atakuwa amechangia kwa miaka mitano au zaidi na labda amepata fao la msiba, n.k au aambiwe asubiri hadi kuretire kuanza kupewa shilingi themanini elfu kila mwezi baada ya kuchangia shirika kwa miaka thelathini au ishirini naona ni unyonyaji wa aina yake.
Ni muhimu kwa wanachama kufaidika kifedha (monetary benefit) na uwekezaji wa NSSF kila mwaka. Na namna pekee ya kuwafanya wanachama nao wanufaike ni kuhakikisha kuwa NSSF (bila ya shaka na mashirika mengine ya pensheni) inaweka utaratibu wa kuwagia wanachama wake ama kwa kutengeneza account au kuchangia kwenye akaunti ya mwanachama kiasi cha faida fedha ambazo mwanachama anaweza kuzitoa wakati wowote nje ya zile za pensheni.
Jambo la kwanza ambalo linahitaji kufanyika kwa haraka ni kubadili sheria ili NSSF isiwezeke fedha za wanachama kwenye miradi yenye kutarajia faida bila kuhakikisha kuwa sehemu ya faida inayopatikana inawarudia wanachama kama gawio siyo kama sehemu kiduchu ya mafao.
Swali la Ugomvi: Je CDM ina sera gani kuhusu NSSF na uwekezaji wa NSSF kwa sababu tayari tunajua sera ya CCM ni kutumia NSSF pale ambapo serikali imeshindwa au haina fedha au pale ambapo serikali inataka fedha ya haraka haraka kuikoa mbele ya wananchi.