Masanilo
Platinum Member
- Oct 2, 2007
- 22,286
- 4,493
prof. Mlambiti wa chadema ndie mshindi na kinachosubiriwa ni nec ulanga kumtangaza, tarafa za malinyi na ngoheranga historically ndio ngome thabiti za ccm lakini 2010 wameamua kuchagua mtu na siyo chama, msingi wa taarifa yangu jamvini unategemea fact hizi.
tarafa za ngoheranga na malinyi zina kata tano katika hizo tano ccm wameshinda 4 na chadema 1 hiyo ni udiwani, kwenye ubunge kura 75 % zote zimeenda chadema, maana prof ameshinda almost 99 polling station za tarafa hizi isipokuwa vijiji vya ihowanja na mbalinyi. Hapa ameshinda sana kwa sababu ya majeraha ya kura za maoni hususani vijana waliojitokeza kumuangusha dkt.ngasongwa baada ya wao nao kuchakachuliwa na tabibu mponda kwa nguvu ya celina kombani na ccm wilaya wakaiasi ccm na kumpigia debe prof. Mlambiti, kosa lingine ni kitendo cha mgombea wa ccm tabibu hadji mponda ni kuitenga na kuidharirisha kambi ya ngasongwa ktk kampeni zake kwa imani kuwa yassin njayagha na simon ngonyani watamsaidia hali ikawa ni tofauti sana maana hao aliowategemea ndio waliotuma majeshi ya kummaliza. Alisituka kuitafuta shuka alfajiri kuwa jamaa wanammaliza tena baada ya ujio wa kingunge jimboni aliyeagiza wagombea wote ktk kura za maoni warudi jimboni na kumtaka dkt ngasongwa akaokoe jahazi, bahati mbaya dkt ngasongwa akiwa ktk safari ya kuitikia wito akapata ajali njiani na kumfanya kukosa sehemu kubwa ya kampeni za lala salama ingawaje ndio aliwaokoa madiwani wa ngoheranga, biro na ihowanja. Dakika za lala salama ccm waliliona tatizo na kuwataka njaygha na ngonyani wakasafishe sumu walioipanda jimboni kama wasemavyo waswahili siku ya kufa nyani vijana hao wakiwa ktk gari moja walipata ajali sehemu ileile ambayo dkt ngasongwa alipatwa na ajali na kujikuta wanarudi mjini ifakara kwa matibabu na kumuacha tabibi hadji mponda akipata sapoti toka kwa alhaj ngasongwa ili kuirejesha malinyi ccm.
tarafa ya mtimbira takwimu zaonyesha kuna kata 6 katika hizo chadema ameshinda mbili lakini kura za ubunge zimegawanyika 55% ccm na 45 chadema, hii imetokana na uzawa wa wagombea wote wawili, wote wanatoka tarafa hiyo na ni wapogoro vidabagha tabibu hadji mponda kwa mtimbira yeye ni mhamiaji lakini prof ni mzawa halisi wa mtimbira, kinachosumbua hapa ni wanamtimbira kuwekwa njia panda ila advantage imekwenda kwa prof.mlambiti na chadema, tarafa ya lupiro kuna kata tano chadema wamezinyakua 2, katika ubunge kura zimegawanyika kwa 55 chadema na ccm 45, hii imetokana na majeruhi wa kura za maoni ccm ndg njayagha ambaye ni mzaliwa wa lupiro kumuunga mkono prof.mlambiti .
mtaji mkubwa hapa ni kura za maoni ndani ya ccm, uongozi wa ccm mkoa na wilaya ulielekeza nguvu ya kumng'oa hasimu wao mkuu dkt ngasongwa wakiamini kuwa tatizo lao ulanga magh ni ngasongwa wakasahau kura jimboni humo ni za mtu si chama. Katibu wa ccm alikula 5m toka mgombea wa ccm anayeshindwa uchaguzi sasa na kijana ngonyani na mkiti alikula mzigo kwa wagombea wa udiwani karibu wote ++yassin njayagha.
kwa msingi huo prof.mlambiti ndio chaguo la ulanga magharibi 201-15.
ktk hali hii ccm ulanga 2012 inatakiwa ifanyiwe overhaul halisi kuelekea 2015,ccm tujipange upya 2015.
Nimekuogopa wewe unadata mno!